Mastory ya Bey
Uhusiano usio na afya ni ule ambao wahusika wapo kutoa shida zao au changamoto zao kupitia hisia zao,yani kila mtu ana shida zake,sasa wapi pakuzitolea ni kupitia kwa mwenzake,kwa maana nyingine kila mtu anamtafuta mtu wa kumbwagia shida zake
Kinyume na mahusiano yenye afya nzuri,mahusiano yenye afya nzuri kila mtu anajijua ana shida na changamoto,na yupo tayar kutatua shida zake mwenyewe au kwakusaidiwa na partner wake,hapa kila mtu anakuwa responsible na shida zake
Katika mahusiano yenye afya mbaya,mhusika mmoja anaamini na kutarajia kwamba mhusika mwingine anawajibika kutatua shida zake au changamoto zake,kinyume chake matarajio hayo yasipo timizwa basi ugomvu na shida zinaanzia hapa
Utasikia fulani anajua nina shida moja mbili tatu lakini mpaka sasa hajafanya juhudi zozote kuzitatua,yani yeye anajiweka mbali na utatuzi wa shida zake,badala ya yeye awe sehemu ya mchakato,anajiona kuna mtu anastahili kutatua shida zake
Mtu anatakiwa amsaidia partner wake pale anapojisikia kufanya hivyo,na sio afanye kwa kulazimishwa,unapofanya jambo kwa kulazimishwa hayo yanakuwa tena sio mapenzi,inakuwa ni kitu kingine
Na anayesaidia naye unakuta hasaidii kwa kuwa anajisikia kufanya hivyo kwa mapenzi,bali kwasababu ili apate mapenzi au upendo toka kwa partner wake,kwahiyo utaona kwamba kiuhalisia hakuna mapenzi hapo,ila ni kitu kingine kabisa kinacho waunganisha watu
Huyu asipotatulisha shida anaona hatendewi haki au ana dhulumiwa,na kwa upande wa pili huyu anayesaidia,anajiona kwamba ana paswa kutatua shida za mwenzake kwasababu inatakiwa iwe hivyo
Haya ni makosa makubwa sana,katika mahusiano yoyote yale kila mhusika anatakiwa ajue kwamba anawajibika kutatua shida na changamoto zake,na hata kama msaada unakuja basi ni sehemu ya msaada tu,na asifikiri kwamba anapaswa kusaidia kwa asilimia mia moja
Na kama akisaidiwa kwa asilimia mia hakuna ubaya,maadamu anajua kwamba hapo awali hayo yalikuwa majukumu yake hiyo imetokea kama zali tu
Lingine mahusiano yenye afya yana mipaka kwa kila mmoja,yani kila mhusika ana uhuru wa kufanya mambo fulani bila kupata kikwazo toka kwa mwingine,maadamu tu yanakuwa sio chanzo cha mfarakano katika mahusiano hayo
Mfano kama kila mmoja wao ana hobby fulani basi awe huru kufurahia hilo pasina kikwazo chochote,mfano kama mume anapenda mpira basi mke anatakiwa asiwe kikwazo juu ya hilo,maadamu haendi kuangalia sehemu ambazo zinaweza leta mtihani
Lakini mahusiano yasiyo na afya nzuri mara nyingi hakuna mipaka kwa wahusika,mathalani mume au mke anaweza kuwa na marafiki wema tu,lakini pasina sababu yoyote unakuta mmoja wao,anamtaka mwenzake asitishe urafiki huo
Kama kweli umeona marafiki wa mumeo au mkeo sio wazuri una haki ya kufanya hivyo,kwasababu mara nyingi watu huathirika na tabia za marafiki zao,ndio maana kuna ule msemo unasema,ukitaka kujua tabia ya mtu fulani basi angali tabia za marafiki zake
Kwahiyo kama hakuna ubaya wowote ambao umeuona toka kwa marafiki wa mwenza wako,basi heshimu mipaka ya mwenzio,na yeye vile vile,mpeane nafasi kila mtu awe huru kuwa na marafiki wema
Kwa kumalizia,mahusiano yenye afya ni yale ambayo kila mmoja atawajibika kwa changamoto zake na shida zake,msaada uje tu kama sehemu ye nyongeza
Pili huyu anayesaidia,asijisikie kwamba analazimishwa au analazimika kusaidia jambo flani,bali afanye kwa kuwa anataka kufanya hivyo bila shinikizo lolote lile,na hayo ndio mapenzi
Na asitoe msaada kwasababu ili apate jambo fulani,akifanya hivyo atakuwa amefanya kwa shinikizo ili apate jambo fulani
Mahusiano ya kweli yapo huru na wahusika wanajisikia wako huru ama kwa kufanya maamuzi fulani au wanakuwa pamoja bila masharti yoyote yale