P_ mawenge
CORONA lyrics
Asubuhi natazama taarifa ya habari, wanatangaza kuna janga jipya la hatari.../
Tuokoe vizazi kwa kuvipa tahadhari, corona virus ukipita kaa mbali.../
Umeishaua sana watu elfu na mamia, kila taifa sasa ndugu zetu wanalia.../
Si marekani china hadi kwetu tanzania, tumuombe sana allah yesu na maria.../
Kirusi cha corona kikizama kwenye mwili, mpaka kugundua na kuanza kuona dalili.../
Imachukua siku mbili hadi wiki mbili, umakini uzingatiwe jamani tusikariri.../
Unasambaa kwa kukohoa na kugusana, hasa maeneo ambayo watu wana songamana.../
Kushika vitu bila kuzingatia usalama, na hata kwa nguo pia ikiwa tukivaliana.../
Dalili zake homa na pia kuumwa kichwa, maumivu makali ya koo na kitapika.../
Kikohozi kibichi na kuhema kwa tabu, ukiwa na sifa hizo unahitaji matibabu.../
Tujitahidi sana kuzifata tahadhari, ukijihisi ni muhimu kwenda hospitali.../
Ufanyiwe uchunguzi wa kina na daktari, na ukikutwa utibiwe kabla haijafika mbali.../
Tusalimie watu bila kushikwa mikono, tuepuke mabusu ya kugusisha midomo.../
Tukikohoa ni muhimu kuzima midomo, hadi janga la corona likishafika kikomo.../
Wanafunzi shuleni masomo yamesitishwa, hakuna matamasha wala semina kabisa.../
Masokoni vyakula na mavazi yameadimika, duniani sasa kila kitu kimevurugika.../
Shukrani sana kwa kila mtu anayepambana na corona kutunusuru afya zetu
Written by Scars
Good night