Hii picha inaongea nini?

Hii picha inaongea nini?

Kiswahili kinafundishwa sehemu nyingi huko duniani ni swala la kupata exposure tu huyo utamuonea wivu.
Duniani wapi na nchi gani?
Kuhusu kufundisha Kiswahili ktk nchi za kigeni ambazo hazitumii Kiswahili kama lugha ya mawasiliano, wa-Tanzania wengi Wana mapungufu makubwa ya kuweza kuwa Walimu wa Kiswahili huko nje, kwa sababu Wana tatizo na uelewa wa kutosha (fluency) wa kuongea Lugha ya kufundishia, yaani Kiingereza (Most of Tanzanians are not fluent in Speaking and Writing in English language). Hiki ni kikwazo kikubwa sana kwa wa-Tanzania kupata ajira za Ualimu wa kufundisha Kiswahili huko nje ya nchi, that's why hata Serikali ya Afrika ya Kusini imetoa ajira za Walimu wa kufundisha Kiswahili nchini humo kwa walimu kutoka nchini Kenya, wala siyo kwa wa-Tanzania.
 
Yeah! Wewe fikiria familia imewekeza millions of money kwa ajili yako halafu unarudi nyumbani na joho tu bila ajira wala pesa. Inauma sana kwa kweli.
Unasema picha inazungumza . Kwa fikra na mtazamo wako unaona hiyo picha inasema "Familia imetumia millions"?

...hebu tuambie, kinacho kuuma ni nini haswa? Eti unajali?
 
Duniani wapi na nchi gani?
Kuhusu kufundisha Kiswahili ktk nchi za kigeni ambazo hazitumii Kiswahili kama lugha ya mawasiliano, wa-Tanzania wengi Wana mapungufu makubwa ya kuweza kuwa Walimu wa Kiswahili huko nje, kwa sababu Wana tatizo na uelewa wa kutosha (fluency) wa kuongea Lugha ya kufundishia, yaani Kiingereza (Most of Tanzanians are not fluent in Speaking and Writing in English language). Hiki ni kikwazo kikubwa sana kwa wa-Tanzania kupata ajira za Ualimu wa kufundisha Kiswahili huko nje ya nchi, that's why hata Serikali ya Afrika ya Kusini imetoa ajira za Walimu wa kufundisha Kiswahili nchini humo kwa walimu kutoka nchini Kenya, wala siyo kwa wa-Tanzania.
Wewe unayejua hicho Kiingereza Fluently unafanya nini zaidi ya kutukana tu hapa?

Umefanya nini haswa kubadilisha taswira hiyo?

Una makelele mengi tu! yap yap all talk, lakini huna tiba. Huna alternative wala suluhisho.
 
Hii picha inaongea mambo mengi sana. Wazungu wanasema a picture speaks louder than words. Nikiiona hii picha nahudhunika mno, hasa kwa ajili ya vijana wa kitanzania wanaohitimu vyuoni makumi kwa maelfu kila mwaka.

Maisha ya kiafrika ni magumu sana. Unaweza ukute hata elimu yenyewe aliyoipata haiwezi kumpa uwezo wa kurudisha alichokitoa ama kubadilisha hayo maisha ya nyumbani kwao. Kibaya zaidi familia zetu pia zinaamini kuwa ukishapata degree basi wewe ndio tegemeo la ukoo , ndio maana vijana wengi huwa wanakimbia nyumbani.
View attachment 2843100
Picha ni Feki na Imechongwa kuvutia hisia za watu.

Picha ikishakuwa feki, basi na maudhui yake ni feki. This is a typical Misinformation. Ni taarifa ya uongo na ni potofu. Maudhui haya yamelenga kudhalilisha na kunyanyasa.

Tafakari
Kama kweli mmeleta picha hiyo kwa nia nzuri, kwanini msiweke Jina, Kijiji, au shule aliye hitimu na kupata shahada gani ili aweze kusaidiwa kupata ajira? Tafakari
Kwanini wengi wenu mnakandia tu?
 
Vijana wengine wanajisomea tu ilmradi wapate digrii wakidhani kitaeleweka mbele kwa mbele. Nawaona vijana wengi waliohitimu Bachelors za Education wapo vijiweni wanaendesha bodaboda.

Kusema kweli kuna haja ya serikali kubadili mtaala wa elimu na kuondoa masomo ya kipumbavu kama vile Kiswahili, Civics, History na masome mengine ya kipuuzi ili kuwapa wanafunzi nafasi ya kujikita kwenye masomo ya maana.
Kwa msingi uliotumia tunaweza sema wewe unayo hiyo Degree inayoeleweka. Na ni kama tu, unayo! Umeitumia kufanya nini kuwakwamua vijana hapo mtaani kwako?
 
Wanasiasa wana dharau sana. Na utakuta nafasi chache zilizopo serikalini wanawapa watoto wao huku watoto wa masikini wakiendelea kulia na kusaga meno. Inauma sana.
Usidanganye watu hapa

....na
Inasikitisha sana kuona kijana kama wewe unabwatuka tu na kusambaza sumu kwa vijana wenzako bila ya kujali madhara unayo yasambaza

Ipo siku utayajutia. Ngoja uzao wako waje wasome hapa ndio utaelewa sumu zako.
 
Hapo sasa. Sijui atajiajirije wakati mtaji wote ameuacha chuoni. Kuna kijana wetu mmoja tumemsomesha pale UDSM digrii ya BA Kiswahili. Baada ya kuhitimu akapata ajira ya kuolewa na kuzalishwa mtoto. Hadithi ikawa imeishia hapo.

Wewe fikiria familia yenyewe ya kimasikini tumejipinda kumsomesha kwa miaka yote 3 halafu ajira anayopata ni kuolewa kwa mahari ya Tsh laki 8. Na bado anadaiwa mkopo na serikali. Ama kweli jehanamu ni hapa hapa Tanganyika.
Mbona nimesikia kuwa ualimu wa kiswahili siku hizi ni dili maana nchi zote jirani zinaanza kufundisha kiswahili?
 
Sikitiko Kubwa Maana Degree Anayo Shida Ipo Pale Pale
 
Hapo sasa. Sijui atajiajirije wakati mtaji wote ameuacha chuoni. Kuna kijana wetu mmoja tumemsomesha pale UDSM digrii ya BA Kiswahili. Baada ya kuhitimu akapata ajira ya kuolewa na kuzalishwa mtoto. Hadithi ikawa imeishia hapo.

Wewe fikiria familia yenyewe ya kimasikini tumejipinda kumsomesha kwa miaka yote 3 halafu ajira anayopata ni kuolewa kwa mahari ya Tsh laki 8. Na bado anadaiwa mkopo na serikali. Ama kweli jehanamu ni hapa hapa Tanganyika.
Shukuru angalau kaolewa na njemba kajipinda kutoa kifuta jasho! Wengine wanaishia kuzalishwa tu! Then single mother! Mbaya zaidi unaletews wajukuu hapo nyumbani
 
Picha ni Feki na Imechongwa kuvutia hisia za watu.

Picha ikishakuwa feki, basi na maudhui yake ni feki. This is a typical Misinformation. Ni taarifa ya uongo na ni potofu. Maudhui haya yamelenga kudhalilisha na kunyanyasa.

Tafakari
Kama kweli mmeleta picha hiyo kwa nia nzuri, kwanini msiweke Jina, Kijiji, au shule aliye hitimu na kupata shahada gani ili aweze kusaidiwa kupata ajira? Tafakari
Kwanini wengi wenu mnakandia tu?
Wee hujitambui! Hii picha inaonyesha hali halisi ya wahitimu wa vyuo vikuu! 💯 ndivyo ilivyo! Wengi watoka familia fukara na kurudi makwao wakiwa na majoho na cheti! Familia inakaa kushangaa "inakuaje sasa????"
 
Wewe unaongea Kwa kutumia hisia wala sio akili

Je ninani kafanikiwa Kwa kusoma science na nani kashindwa Kwa kusoma arts ,kufanikiwa maisha kuna involve mambo mengi Sana. Ni mtu mjinga pekee anaweza kutoa lawama Kama hizo.
Mkuu ni wapi nimetoa lawama?.mm nimeeleza hali halisi sijamlaumu yeyote.
 
ingawa ni picha ya kutengenezwa kwamba sio halisi ,lakini uhalisia upo hivyo katika jamii yetu.
ukosefu wa ajira sio hapa kwetu tu, sijawahi kutoka nje ya mipaka ya nchi hii lakini kazi yangu imenikutanisha na watu wengi wanaotoka kwenye mataifa makubwa yaliyoendelea huko Ulaya na Asia, kwa mujibu wao huko nako hakuna wepesi wa kupata ajira kwa kijana japo mazingira ya ukosefu wa ajira ni tofauti na sisi lakini hawana uafadhali kuliko sisi.

pia sio wakati huu tulio nao ndio ajira imekua ngumu hapana, tunaosoma hivi vitabu vya dini kuna mfalme mmoja alikua anahitaji vijana wanne wasomi hivyo akaagiza vijana karibu thelathini waingie darasani, walipo hitimu ni wanne tu walio pata ajira hao wengine hawakuhitajika kwa kua nafasi zao hazikuwepo.

ni swa na sasa hivi, elimu ya msingi ni lazima kwa kila mtoto anazaliwa katika taifa hili, kadhalika na elimu ya upili nayo imekua ya ulazima, ila kuna kuwa na mchujo kiasi, elimu ya juu nayo wanaendelea kuchuja kadhalika na elimu ya chuo nayo wanaoingia wamekua wamechujwa, mwisho kwenye ajira wanaotakiwa ni robo ya hao wote.

wanaanza elimu ya msingi 10, elimu ya upili 8 elimu ya juu 6 elimu ya chuo 4 na ajira 2.
kwa hio tunapoweka matajio 100% kwamba itapatikana ajira baada ya kuhitimu chuo ndio mwanzo wa makosa.

umuhimu wa elimu hautakuwa na mwisho hata kama matarajio ya faida ya hio Elimu yatakosena.

kwangu mimi naona sambamba na kugharamia elimu pia garamia baada ya elimu, ardhi yetu hapa Tanzania ni kubwa mno na yenye rutuba, tufanye miti, tupande mazao ya muda mrefu yanayostahimili ukame na maradhi ya mimea, tufuge wanyama kama mbuzi kuku na ngo'mbe, tujifunze ufundi , tufungue biashara ndogo ndogo na mengi mengi sana tunayoweza kufanya ili baada ya chuo isikosekane pa kuanzia.

tupunguze lawama kwa serikali japo kwa kiasi kikubwa serikali wameshindwa kuonyesha dira na mwelekeo kwa vinara wengi mwisho maumivu laumu na vilio vimekuwa vingi mno .

tusisahau pia kuzaa kwa mpangilio japo swala la uzazi ni la Mwenyezi Mungu .
 
Wee hujitambui! Hii picha inaonyesha hali halisi ya wahitimu wa vyuo vikuu! 💯 ndivyo ilivyo! Wengi watoka familia fukara na kurudi makwao wakiwa na majoho na cheti! Familia inakaa kushangaa "inakuaje sasa????"
Kwanza tu, huna uwezo wakijutambua mwenyewe unawezaje kudai kuwa sijitambui...
...wakati huwezi hata kutambua picha ni Feki? Na picha ikishakuwa feki basi na maudhui yake ni feki no matter how hard you spin it.

Pili,una ushahidi gani huyo kijana aliyeko pichani amehitimu chuo kikuu?

Wacha ufukara wa mawazo na kimtazamo. Jitathmini.
 
Katika kipindi hiki cha graduation kwenye taasisi nyingi za elimu nadhani ni wakati wahitimu na wahitimu watarajiwa wajiweke sawa kifikra wajue kabisa wanapomaliza wajue jamii ya mtaani si lelemama. Wanapokuja huku wasije na mentality za kichuo huku maisha ni mkanda ukilegeza unaadhirika. Kila la kheri kwa wote
Kwani hawa wahitimu wa chuo mnaowasema huwa wanaishi wapi? Sio hawa tunaishi nao mtaani na wanaona uhalisia wa mambo?
Sifikirii kuna mhitimu anamaliza asijue mtaani kuna nini.
 
Back
Top Bottom