Hali ya wanachuo mtaani

Hali ya wanachuo mtaani

Kuna jamaa kamaliza saut,afu karudi kwao kijijin hatak kukubaliana na hali kuwa kamaliza chuo na hana mishe,kila siku namuona anachomekea na kuvaa ksmart vikadeti vyake vya chuo na shati za mtumba

Wenzie tulishapigika kitambo sahv tunaendesha boda boda ila najua baada ya nusu mwaka atanyooka tu hasa huto tukadet tukianza kuchanika kwenye magoti
Unamuombea mwana mabaya
 
Siku hizi mitaa imepambwa na degrees za kutosha kutoka mavyuoni, Lakini cha ajabu vijana wamekua wakitia huruma kuliko hata aliyemaliza la saba, WANACHUO wengi wanapata taabu sana huku mtaani kuliko hata raia wa kawaida, kiukweli inahuzunisha. Pale kijana anapotoka chuo na matarajio makubwa Lakini ghafla maisha ya mtaa yanazima ndoto zake.

Yapi matunda ya mfumo wetu wa Elimu? Au ni uzembe wa vijana kutojituma wawapo mtaani?

#MyCountryPeople.
Kijna tangu kaanz chekechea hajui life la kujitegemea.kila ni mama/ baba afu aje mtaan ajiendesh haiwezkn,kijn tumezoea kujidekeza snaa na ubishoo mwngi
 
Hata hao wanafunzi wa veta, tumekutana nao huko kwenye Ma-field, wapo shallow sana, nadhani kinachowabeba ni ile kufanya kazi mda mrefu so wanakuwa na experience kubwa
Mwisho wa siku hata wewe na elimu yako unayoiona bora kuliko waliopitia VETA unajikuta unaambiwa ili uwe pale walipo wao na wewe onyesha kitu ambacho huna kwa wakati huo.

Ni vita,hatusemi elimu ni mbaya au haifai tatizo ukiiangalia kwa angle nyengine unakuta ni kisababishi cha upotevu wa muda na kuwajengea vijana tabaka la kuchagua kazi.
 
Majobless tumebaki kubet tu balaaa
Mimi madogo wa chuo nawaambiaga hakikisha kabla ujamaliza boom la mwsho ununue viwalo vya kutosha
Depo la mtaani huku utavaa boksa inaisha hadi inabaki na kamba kama nanga
Serikali iangalie kama inashindwa kuaccomodate graduates basi waombe mazingira vijana wakajarbu ng'ambo
hatari..
 
Sitasahau nilivyohitimu chuo mwaka 2015 na kurudi nyumbani nikiwa na mategemeo makubwa mno kupata ajira kwani wakati huo education walikuwa wanaajiriwa bila hata kutuma maombo.
Kasheshe ilikuja pale Magufuli alipotangaza walimu wa arts wapo waziada daa nilitamani kujifukia.Nikaomba private malipo hakuna unakaa miezi hata sita hujalipwa,nikauza nyumba ya ulisi nikaanzisha biashara na nikaoa biashara nayo ikafa nikarudi private mambo ni Yale Yale.kimbembe wife akapata mtomto yani haya maisha nyie acheni tu.
Namshukuru mama amenikumbuka na angalau mambo sio haba .nawatia moyo vijana chakalikeni japo Kuna kufeli ila msikae kusubili ajira fanya lolote ili uishi.
Huko mitaani Kuna raia wana roho mbaya Sana wanapenda kuona wasomi wanateseka ili wawacheke.nakumbuka walivyokuwa wananiona nahangaika naishi kwenye kaslop nikokajenga choo cha miti nimefunika matulubai wanacheeka nakusema eti nilitumbuliwa na vyeti feki.daa maisha haya

Sent from my Infinix X665B using JamiiForums mobile app
 
Ni kweli lakini kufundisha kama una GPA kubwa mnaweza itwa watano tu so chances za kutoboa bila connection ni kubwa. Ukiangalia Mitandaoni nyingi zinakua re-advertised maana hakuna applicants wenye vigezo wameomba.
Ndo hivyo yaan
 
Siku hizi mitaa imepambwa na degrees za kutosha kutoka mavyuoni, Lakini cha ajabu vijana wamekua wakitia huruma kuliko hata aliyemaliza la saba, WANACHUO wengi wanapata taabu sana huku mtaani kuliko hata raia wa kawaida, kiukweli inahuzunisha. Pale kijana anapotoka chuo na matarajio makubwa Lakini ghafla maisha ya mtaa yanazima ndoto zake.

Yapi matunda ya mfumo wetu wa Elimu? Au ni uzembe wa vijana kutojituma wawapo mtaani?

#MyCountryPeople.
Elimu imekaa kana kwamba ukimaliza ni kazini one way, badala yake mtaa unakutaka uwe na elimu ya kuchakata fursa zilizopo na kuzijeuza biashara. Hapa ndo vijana wengi wanapigwa KO.
 
Back
Top Bottom