Walete uchaguzi mdogo angalau hizo bilioni 4 zitasaidia kutuongezea kamzunguko ka hela hapa na kupunguza umaskini japo kiduchu. Tutapata wateja wa soda, maji ya kunywa, michemsho, mitura, guest houses, na hata dada poa pale Shivers. Mshkaji wa Raha Promotions atapata tenda ya matangazo ya kampeni na wapangaji wetu watapata pesa ya kutulipa kodi ya pango. Tutauza nyama choma kwa wingi (hizo wapambe watakazokuwa wanahonga wapiga kura tangu kwenye kura za maoni), waarusha watapata soko la mbuzi wao. Wapambe watapata pesa za kumalizia nyumba zao Moshono, kambi ya chupa, Kwa Mromboo nk, na vijana wetu watapata kazi za ujenzi. Na kadhalika na kadhalika. Asanteni kwa uchaguzi huu mdogo mnaotuletea.