Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Lema kavuliwa ubunge rasmi...

Hii ni taarifa rasmi toka hapa mahakamani!

Inasikitisha sana kuona nchi inaweza kuendeshwa kwa maigizo na vibweka namna hii, nchi yenye watu masikini wasiojua watakula nini, nimesoma na kusikia uwepo wa viongozi wabovu duniani lakin hawa wa TANZANIA ni aibu ya kutupwa, its really shame to be under this leadership.
 
Hii hukumu imepikwa kabisa maana ushahidi hauendani na maamuzi yaliyofikiwa. Wahuni hawa wanaweza kufanya Lema akigombea tena anaweza kuwekewa pingamizi na tume/ccm wakakubaliana na pingamizi na wakalipitisha na hatimaye tukashindwa kwa ccm kuchukua kiti bila kupingwa kiulaini.

Nimemsikia mara chache katibu wa chadema wa mkoa wa arusha akiongea jukwaani na nasikia ana uwezo sana. Ndiye anayewachezesha kwata CCM behind the scene. Nilimuona kwenye friends of chadema pale kibo palace hotel kwa kweli anaweza kuwa mbunge wa arusha mjini. Kamwe hatuwezi kukubali jimbo hili liende ccm na tutahakikisha ushindi kwa chadema. Nawaza tu!!
 
Ninachofurahi na kumshukuru Mungu ni kwamba CHADEMA ina viongozi, waabunge na wanachama wenye akili. Pia ninamshukuru Mungu kuwa Watanzania tumeshafunguka na tunaendelea kufunguka macho kuona uozo wa CCM. Ni masikitiko makubwa kuwa bado CCM inaendelea kutumia kodi za wananchi kughrimia na kuhonga ili kupitisha sera zao ambazo zimeshakataliwa. Kwa sasa serikali haina hela, shughuli za kimaendeleo na za kawaida kwa serikali katika Wizara na taasisi zake zimelalla, hakuna OC (Other Charges) ya kutosha matokeo yake watumishi wake wanaingi aofisini na kusaini vitabu. Je tutapimaje utendaji au mafanikio ya Ilani ya Chama kama serikali haifanyi kazi? Matokeo yake tunapoambiwa kuandika progress report ya robo mwaka, nusu mwaka au mwaka basi hakuna cha kuandika!!!! Pesa ya kurudia uchaguzi ingetumika kugharimia kazi jamani. It is very painful. Tuwe wazalendo. Siasa kwa upande wangu zinapingana sana na maendeleo. Sasa nasubiri pesa itakayotumika Arusha tena, si mngezipeleka kule tulikoahidi ahadi za matrilion ya hela wakati wa uchaguzi wa awamu ya nne awali na huu wa mwisho. Je 2015 tutawaaambiaje wananchi? Hebu tuchambue kwa kutumia akili na si hisia. Nawasilisha, CCM chukuen hatua. Nampongeza NCCR kwa kufuta kesi, jimbo la Kawe dhidi ya Halima Mdee. Naweza kusema Mr. Mbatia aliona mbali zaidi madhara ya uchaguzi kama Mdee angetenguliwa. Tuachane na umimi inapokuja suala la matumizi mabaya ya rasilimali na kodi za walala hoi kwenye chaguzi kisizo na mvuto. Yaani hata ubungo mnathubutu kupoteza muda wa wanasheria, mawakili wa serikali na muda wa mh. Mnyika? Acheni mbofuuuuumbofuuuuuuu.
 
CDM,CCM Mjipange kugombania jimbo hilo, kumbukeni mafisadi hawatakiwi, tunaoumia ni sisi wananchi kwa kodi zetu kutumika kwenye uchaguzi badala ya maendeleo.
 
natamani sana yule mama arudishwe au mtu yeyote wa ccm aingie katika uchaguzi huu
lazima tupambane adi Mungu mwenyewe aingilie kati,au adi mtu wa mwisho mwenye kutaka mageuzi ya kweli katika Tanzania
tumechoshwa na ushenzi wa mafisadi na wahuni wachache wa hii nchi wasiotuzidi idadi nzima ya watanzania
TUSICHOKE HASILANI TUHIMIZE NDUGU ZETU ADI KULE VIJIJINI KABISA
 
Pole Makamanda naona hukumu ya Lema imearibu sherehe yote ya Arumeru.
 
mbona hili suala la wabunge kuvuliwa uanachama limekuwa kana kwamba nchi haina matatizo ya kushughlikia ila tu ubunge mimi nashauri haya mambo ifikie hatua yasipewe wakati mwingi bali tuangalie ni jinsi gani tunaweza kulikwamua taifa kutoka katika hii khali na jambo jingine hebu tujiulize kwa nini wabunge wafanye mambo ambayo baadae yanaligharimu taifa fedha nyingi badala ya kuelekeza kwenye miradi ya maendeleo kama kweli lema kavuliwa ubunge kwa sababu ya rushwa kwa wapiga kura basi siyo tu kulipa gharama zilizotumika kuendeshea kesi bali pia afunguliwe mashitaka kama sehemu ya ukiukwaji wa utawala bora na haki za binadamu
 
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini mheshimiwa Godbless Lema wa CHADEMA avuliwa ubunge na mahakama asubuhi hii ya leo lakini mpaka sasa hakuna uvunjifu wa amani hapa town na wamesema kuwa hawakati rufaa wanasubiria uchaguzi mwingine,,ntawapa updates zaid

Huo ni wasaa mwingine kwa Chadema kupata majukwaa ya kueleza Watanzania hali halisi ya nchi. Tume itangaze uchaguzi mwingine faster mapambano yaanzE. Hizo ndo mahakama za bongo bwana! Kwa ushahidi gani wakati mashahidi walikuwa wanapishana? Kama hukumu imeshinikizwa kweli ni hatari kwani kapu la serikali halina kitu; then hayo mamilioni ya uchaguzi mdogo yatatoka wapi? Watanzania daima tusonge mbele...... Hakuna kulala.
 
Mpe tuu ng'ombe kamba ndefu itamnyonga tuu,ccm wana tabia isiyostahili kupewa tena madaraka,hata kama wametumia mahakama kumuondola mh mbunge lemah kamwe kamwe kamwe ccm haitakaa itawale ausha tena maana nguvu ya umma itaamua kama ilivyokua arumeru mashariki
 
anaruhusiwa kugombea tena?????bas lema amesimama kwa mda kua mbunge kwani safari hii atapita kwa kishindo zaidi...
 
Godbless Lema,ni kiasi gani cha gharama yote ya kesi?

niambie hapa tulipe sisi!!
 
Lema kavuliwa ubunge rasmi...

Hii ni taarifa rasmi toka hapa mahakamani!
Sipati picha uchaguzi unarudiwa, sijui Sisiemu watatoa hoja gani.... watamtumia nani.... Je? watamtumia Lusinde? sipati picha hiyo mitusi watakayoimwaga juu ya viongozi wa chadema ila Sisiemu inaenda kujimaliza!

Binafsi nafurahia sababu Chadema inakwenda kushinda mara ya pili tena zaidi ya ilivyokuwa 2010 sababu wapenzi wa chadema wanaongezeka kila uchao huku sisiemu ikipunguza wapenzi wake kwa kasi ya ajabu, na ndio maana huko Arumeru madiwani wote sisiemu, lakini wamepoteza ubunge tena wakiwa wametumia Bilions of shilings
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom