Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Natumaini kuwa uongozi wa juu wa CHADEMA una busara za kutosha kujua nani wa kumsimamisha. Tulio na kadi za kupiga kura tujitayarishe kumchagua mgombea ambaye tunamhitaji.
 
preta,wana wa nchi wansemaje,i mean wananchi wa kawaida

naona wananchi karibu wote niliokutana nao....maoni yao yanafanana.....
mbunge ni Lema (au yeyote wa Chadema)........ndivyo ilivyo kwa sasa.....
 
Tusubiri na tuone kama watatenda Haki jimboni Segerea...

Narudia tena, CCM ni mufilisi kabisa; Watashindwa katika chaguzi zote watakazorudia sasa hivi. Ubungo wana mpango kama huo waliofanya Arusha, na kule kwa Tundu Lissu wanaplan kufanya hivyo hivyo. CDM siku zote ni nguvu ya Umma. CCM itashinda mahakamani, lakini itashindwa kwa nguvu ya Umma kwenye ballot box.

Ila sipendi kabisa hizi chaguzi ndogo; kwanza zinapoteza muda, pili zinachelewesha maendeleo ya jimbo na nchi (viongozi wakuu karibu wote wanahamia jimbo husika); tatu zinakula kodi za wananchi ambazo zingeweza kufanya kazi nyingine mbadala. Hapa naungana na Mtatiro kuwa ukifika kipindi fulani baada ya uchaguzi wa mwanzo; chaguzi ndogo zote, zisitishwe hadi utakapofanyika uchaguzi mkuu.

Pole kamanda lema...lakini kwanguvu zote nasema "Aluta Continua"
 
Baada ya kuenguliwa ubunge wa Arusha,sasa bwana GODLESS LEMA anakabiliwa na pigo lingine kubwa ambalo wadadisi wa mambo wanaamini linaweza likamfanya ashindwe kutetea kiti chake na hivyo kushindwa kuingia bungeni! PIGO hilo linahusiana na yeye kuwaambia WANAARUSHA tangu achaguliwe miaka miwili iliyopita ameshawafanyia nini wanaARUSHA mpaka sasa? LEMA amekuwa akihaha huku na huko,kushiriki maandamano yasiyo na TIJA baada ya kujikita katika kuleta maendeleo na kutimiza ahadi, inadaiwa mpaka sasa lema hajafanya chochote arusha, utalii umeshuka kutokana na maandamano yake ya mara kwa mara,hili kwa kweli ni PIGO SANA KWAKE NA CHAMA KWA UJUMLA!
MYTAKE: KAMA CHADEMA WANAWEZA WAMSIMAMISHE MTU MWINGINE ARUSHA

Ushauri mwingine ukiuangalia tu unaweza tabiri alioutoa alikua wapi!!
Anyway, maliza kwanza mataputapu yako kisha usubiri pombe ipungue, waweza kuja tena that time tukakuelewa!!!
 
Wanachedema Arusha tujipange upya kwa uchaguzi mwingine
tuakikishe jimbo aliendi ccm.
BADO TUNAIMANI NA LEMA!!!!
 
Haya ni matokeo ya demokrasia na mfumo wetu. Katiba mpya ije na jibu la kuepusha chaguzi ndogo za marakwa mara.
Lema anatakiwa Bungeni ni wajibu wa wananchi wa Jimbo lake kuwapa watanzania mbunge huyu ambaye kwa vyovyote vile anawafaa wao na tanzania kwa ujumla

Reply



ARCHIBALD KIWANGO
05/04/2012 2:14am



pole sana mh. lema lakini nina imani liberated zone (moshi - arusha) itarudi kama kawaida sina shaka na wananchi wako watakurudisha tena kwa aibu kubwa kwa wapinzani wako

Reply



Richard Rwechungura
05/04/2012 2:54am



Napenda kuuliza swali, hivi kama adhabu ya mbunge aliyetoa matusi kwenye kampeni ni kutenguliwa ushindi, je aliyetukana halafu akashindwa kwenye uchaguzi adhabu yake nini?



 
CCM miaka yote hiyo wamefanya nini? umeshindwa kusema mnamuogopa lema ukaamua kuingia kwa gia hiyo.......utalii for whose interests wakati wanyama wetu wanauzwa na kusafirishwa nnje kinyemela
 
Walete CCM wagaragazwe tena, sikio la kufa kweli halisikii dawa.
 
mbona tangu uhuru kazi ya ccm ni wizi, ufisadi, na dhuluma....maendeleo machache yaliyopo ni hela za wahisani, maana nazo wameshindwa kuziiba kama kodi za wananchi
 
baada ya kuenguliwa ubunge wa arusha,sasa bwana godless lema anakabiliwa na pigo lingine kubwa ambalo wadadisi wa mambo wanaamini linaweza likamfanya ashindwe kutetea kiti chake na hivyo kushindwa kuingia bungeni! Pigo hilo linahusiana na yeye kuwaambia wanaarusha tangu achaguliwe miaka miwili iliyopita ameshawafanyia nini wanaarusha mpaka sasa? Lema amekuwa akihaha huku na huko,kushiriki maandamano yasiyo na tija baada ya kujikita katika kuleta maendeleo na kutimiza ahadi, inadaiwa mpaka sasa lema hajafanya chochote arusha, utalii umeshuka kutokana na maandamano yake ya mara kwa mara,hili kwa kweli ni pigo sana kwake na chama kwa ujumla!
mytake: kama chadema wanaweza wamsimamishe mtu mwingine arusha

lema hajashusha utalii arusha, bali ni serikali ya ccm ambao wamekua wakiwatumia polisi kupiga mabomu wananchi, na vile vile maandamano arusha yameleta tija kwani alikuwa anapigania haki kuliko kuleta maendeleo bila haki haina tija
 
hili kwa kweli ni PIGO SANA KWAKE NA CHAMA KWA UJUMLA!
MYTAKE: KAMA CHADEMA WANAWEZA WAMSIMAMISHE MTU MWINGINE ARUSHA

Basi tutakusimamisha wewe!!!!!!

Mkae mkijua kuwa yeyote atakayegombea kwa tiketi ya Upinzani na hususani CDM ushindi ni lazima tu. Tumeichoka CCM na ahadi HEWA.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Ameshindwa kwa kosa lipi? Naomba mwenye taarifa kamili atujuze.

1) Ameshindwa kwa kumdhalilisha dada wa watu

2) kutumia lugha za kibaguzi/ ubaguzi wa kikabila

3) Ametumia lugha za udhalilishaji na ubaguzi wa kidini

Inshort jamaa hafai kabisa na amesababisha kuharibu image ya CDM.
 
lema hajashusha utalii arusha, bali ni serikali ya ccm ambao wamekua wakiwatumia polisi kupiga mabomu wananchi, na vile vile maandamano arusha yameleta tija kwani alikuwa anapigania haki kuliko kuleta maendeleo bila haki haina tija


hASWAAAAAAAA!!!!!!!!

Mfano yale mabomu ya machozi pale UBUNGO DSM juzi, je, ni Mnyika alihusika pale kama siyo CCM na Polisi wao.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom