Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Lema akiongea na radio one.."nimepigikiwa simu tangu jana kuhusu uamuzi huu...na hata H.Mdee amenitaarifu mapema asubuhi kuwa amepata habari kwa mtu nyeti kuwa nimeshindwa kesi...polisi wamezingira ofisi ya mbunge alfajiri na hata mahakamani kabla ya uamuzi hii inaonyesha ilishapangwa...makamba aliongea na mtu wa ccm kumtaarifu ajiandae kwa kura za maoni....hata wakirudia uchaguzi bado nitashinda...nasubiri tamko la chama ndio niwajuze wananchi nini cha kufanya".

Hii nimeipenda .
Mh.Lema pamoja na Chadema Makao Makuu hakuna kukata rufaa.Waacha uchaguzi ufanyike August 2012.Muhimu kuanda timu nzuri ya Kampeni na pia kudai marekebisho katika daftari la wapiga kura ili vijana waliofikia umri wa 18yrs baada ya 2010 nao wapate haki ya kupiga kura.Katika hili inafaa kuwa andikisha kata hadi kata vijana wote ambao wamefikia umri wa kupiga kura na kufungua madai katika tume ya Uchaguzi mapema kabla ya muda wa Kampeni
 
Baada ya kesi iliyochukua muda mrefu, hukumu imetolewa. Ubunge wa Godbless Lema umebatilishwa, kwa hiyo jimbo la Arusha mjini ni wazi, halina mbunge. Tusubiri taratibu za uchaguzi mdogo.
 
Wilbrod Slaa


We shall overcome.!

app_2_2231777543_7567.gif
LikeUnlike · · @wilbrodslaa on Twitter · 21 minutes ago via Twitter ·

Poor him!
 
Mmelifikiria hili la Mwanasheria mkuu kukata rufaa kupinga hukumu hii? Hata Lema asipokata rufaa ili uchaguzi mwingine ufanyike haraka, Mwansheria mkuu ambaye naye alikuwa mshitakiwa anaweza kukata rufaa na kesi ikavutwa hata miaka huku Lema akiwa sio mbunge.

Hii Ze Comedy huenda hatujafika mwanzo wa mwisho wa sinema ila ndio tumefika mwisho wa mwanzo.
 
Pole Lema.
Pole CHADEMA.
Kwa wanaotaka kufahamu, Jaji Rwakibarila hakunadika Hukumu ya kesi hii; imeandikwa na Dr. Masumbuko Lamwai. Chadema wakitaka kuzuia mvua hii ya Mahakama kutoa ushindi CCM, basi mkakati wao unapaswa kumshughulikia Lamwai. Majimbo mengine ambayo matokeo ya uchagzi yatatenguliwa ni Ubungo, siyo Segerea.


Naamini hujakurupuka bali una evidence na usemayo. Inabidi huyu Dr. Masumbuko Lamwai aanze kunyatiwa na kamati ya ufundi ili aeleze kwa nini ameamua kuwasaliti waTZ kwa kuwanyanganya tonge mdomoni. Kama pia haya ni ya kweli basi uthibitisho utafutwe ili CDM iangalie what should be the next step.
 
Hii nimeipenda .
Mh.Lema pamoja na Chadema Makao Makuu hakuna kukata rufaa.Waacha uchaguzi ufanyike August 2012.Muhimu kuanda timu nzuri ya Kampeni na pia kudai marekebisho katika daftari la wapiga kura ili vijana waliofikia umri wa 18yrs baada ya 2010 nao wapate haki ya kupiga kura.Katika hili inafaa kuwa andikisha kata hadi kata vijana wote ambao wamefikia umri wa kupiga kura na kufungua madai katika tume ya Uchaguzi mapema kabla ya muda wa Kampeni

Je Mwansheria Mkuu akikata rufaa? Huenda hii ngoma bado mbichi.
 
Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kupitia CHADEMA, amepoteza kiti hicho kwa kuenguliwa na Mahakama katika kesi iliyokuwa inamkabili ya kupinga ubunge wake.Kesi hiyo iliyofunguliwa na makada watatu wa CCM, Mussa Mkanga (55), Happy Kivuyo (49) na Agnes Mollel (44) ambao walikuwa wanamtuhumu Mbunge huyo kwa kutoa kauli za udhalilishaji, matusi na kashifa kwa aliyekuwa mgombea wa Ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Dkt. Batilda Buriani.Hukumu hiyo iliyosomwa na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila.Katika hukumu hiyo, Lema hakuondolewa haki ya kugombea ubunge huo kwa kuwa kosa lililomtia hatiani ni matumizi mabaya ya lugha tofauti na ilivyodhaniwa kuwa ni vitendo vya rushwa. Uamuzi wa kugombea ama kutokugombea kiti hicho tena utatokana na maamuzi yake mwenyewe na ridhaa ya chama chake ikiwa kitamteua na kumpitisha kugombea.Taarifa za watu wa karibu zinasema kuwa Lema hatakata rufaa mahakamani juu ya hukumu ya kesi hiyo, bali atakata rufaa kupitia kura ya wananchi wa Arusha Mjini wakati wa kugombea kiti hicho. Hivyo tutarajie uchaguzi mpya ndani ya siku 90. Tanzania, nchi ya uchaguzi kila uchao...!
dats a heroic decision he has made..
 
Ooh no!
Lakini tukumbuke kwamba, hizi ndio harakati za ukombozi, zinakuwa na njia ngumu sana na zenye maumivu makali hata wakati mwingine umwagaji wa damu.
Mwaka huu naona kama mapambano ya ukombozi wa kweli wa Tanzania ndio yameziduliwa rasmi na CDM.
Naomba sana CDM isije kukata rufaa, kwani kufanya hivyo mahakama hizi za magamba zitatumia delaying tacts ili uchaguzi usirudiwe.
Aibu kubwa kuliko ie ya ARMR inakuja kwa ccm.
Aluta continua!!

uwezekano mkubwa ni CCM kukata rufaa wakitaka mahakama ya rufaa ifanye mapitio ya kesi ili Mhe. G Lema azuiliwe kugombea, watafanya hivyo kwa lengo la kuzuia uchaguzi kufanyika mapema na kuhakikisha jembe hili lisiendelee kuwalima! CHADEMA wako nuruni lakini CCM wanatembea na nguvu za giza!
 
Kuipenda ccm inakubidi uwe na akili ya mzoga wa bundi!
 
haki ya Mungu sijui ccm wanafikiria kwa kutumia nini! Hivi hawaoni kuwa wanaongeza kasi ya mabadiliko nchini? Na aliyewaroga bora aendelee kufa. Muda si mrefu watakaribia mzinga wa nyuki, na itakuwa hatma yao katika duru za siasa Tanzania
 
haswa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hii nimeipenda .
Mh.Lema pamoja na Chadema Makao Makuu hakuna kukata rufaa.Waacha uchaguzi ufanyike August 2012.Muhimu kuanda timu nzuri ya Kampeni na pia kudai marekebisho katika daftari la wapiga kura ili vijana waliofikia umri wa 18yrs baada ya 2010 nao wapate haki ya kupiga kura.Katika hili inafaa kuwa andikisha kata hadi kata vijana wote ambao wamefikia umri wa kupiga kura na kufungua madai katika tume ya Uchaguzi mapema kabla ya muda wa Kampeni

Hili la ku update daftari magamba hawatakubaliana nalo. Arumeru tumeshinda bila ku update daftari. Tunaanza na Mungu na tunamaliza na Mungu
 
Ccm hata ikisimamisha jiwe itashinda Lema hajafanya chochote tangu awe mbunge zaidi ya sifa za kijinga za kukataa dhamana na kupelekwa mahabusu!
 
Ni hukumu ya upendeleo na haina msingi!
kaka n ya upendeleo mwanzo mwisho!NA Kifup Tuwaonee Huruma Ccm Kwan Watapigwa mara7 ya uchaguz wa Awal!EE MUNGU SIKIA KILIO CHETU WATANZANIA TUMECHOKA KUDANGANYIKA!
 
Swafi sana tayarishe KOMBAT wana wa Arusha twaja kwa ajili ya kumpigia kampeni LEMA. CCM WEZI WA MALI YA UMMA
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom