Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Sheria zinasemaje? ataruhusiwa kugombea tena?

Ameruhusiwa si ataruhusiwa! Unajua jaji katoa hukumu kimtego na akamsihi Lema akate rufaa kama anaona haki haikutendeka na alifanya ivyo akijua Lema atachagua njia fupi ya kuendelea kuwa mbunge kwa kukata rufaa. Kwa bahati mbaya Lema kachagua njia ndefu ya acha uchaguzi urudiwe na atagombea tena!! Jaji kusikia hivyo Kapanic yani baada ya hukumu amekuwa biz na simu mpaka ameona ofisini hakufai amenda kukaa kwenye gari mpaka mie naondoka mahakamani bado anaongea na simu!
 
Tutaanza na Mungu tena na Tutashinda na MUNGU wao mijitusi kibao hahahahahahah (CCM wezi wakubwa wa mali ya umma)
 
duh!!! uchaguzi mdogo tena
Ya!!! Uchaguzi mdogo una manufaa makubwa kwa upande wa CHADEMA kwani chama kinazidi kujitangaza zaidi, na kila uchaguzi mdogo utakapo kuwa unafanyika ni wazi CHADEMA itaibuka mshindi.
 
magamba yanawawashaa hawaamini ya ARUMERU watashangaa ya ARUSHA MJINI halafu ya UCHAGUZI MKUU 2015
 
hukumu ya aliyekua mbunge nikiini macho kwa wananchi wa arusha...Jaman mambo haya yataisha lini...tunajua dhairi michezo ya chama tawala cha mafisasi. Nashukuru kutokua na fujo yoyote mpaka sasa na nashukuru chadema kua na uamuzi wa kutokata rufaa..jimbo la ARUSHA naomba litambulike kua ni la chadema hata kama wamemuondoa Lema....
 
Mhhhhhhh kwa hyo pesa zingine tena zinaenda kuchezewa tena ?? au hakutakuwa na kampeni tena?? Hivi kweli tutafika kwa mtindo huu??

Afadhali hizi zitatumika kihalali. Hujasikia za juzi, madawa ya bil. 5 kuisha muda MSD, ongeza milioni mia zitazotumika kuyateketeza! Hujasikia na za leo Dom, nyumba ya Waziri kukarabatiwa kwa mil 100 plus, na mamilioni mengine alotumia kuaanda sherehe rafiki zake!
 
kwa hiyo idadi ya wabunge Chadema imebaki kama ilivyo !kaingia Nasari katoka Lema!
 
Godbless Lema wewe bado ni Mh. Mbunge wetu tutapiga kura tena kudhihirishia ulimwengu wote na mafisadi wote kuwa wewe ni chaguo la wananchi wa Arusha.

Tupo Pamoja Brother.
Peopleeeeeeeeeeeeeeeeeeees Power


Kwa kuongezea hakuna kukata Rufaa ya aina yeyote na kwa msingi huo Lema anakuwa mbunge hadi atakapo apishwa tena Bungeni Hii ni kudhihirishia umma kuwa hata kama wataendelea kuwavua ubunge kina Lisu, Myika, Mbowe, Mdee, Na Nasari wa Juzi hakuna kukata Rufaa kwenye mahakama ya CCM na Mafisadi bali kwenda kwa wananchi..

Nachoona ni huyu jaji kala hela za mafisadi kashindwa kusimamia ukweli na alifikiri Lema atakata Rufaa.

Mwambieni rufaa yetu ni kwa Wananchi na Mungu tu... Kama alivyosema Nasari TUNAANZA NA MUNGU NA TUNAMALIZA NA MUNGU...

PEOPLES POWER...
 
ha ha ha naionea huruma sana ccm sasa kweli chama ndio kinaelekea kufa karibu sana sijui nani atawasikiliza sasa watu hawataki mnalazimisha mtamwongoza nani?,mnapenda kupoteza muda tu wana Arusha wamefunguka bado wanamtaka lema kwa sababu ndio chaguo lao au mnasikia raha damu ikimwagika?.
 
Lema amesema kupitia Radio One kwamba CCM na serikali nzima ilijua hukumu hii tangu wakati wa uchaguzi wa Arumeru na jana na leo asubuhi tayari aliona dalili. Aliambiwa atulize wafuasi wake kabla ya hukumu na ofisi yake ilizingirwa na polisi asubuhi leo kabla ya hukumu. Kisha viongozi mbali mbali wa polisi na CCM walishatamka kwamba atashindwa kesi na uchaguzi utarudiwa
 
maadam anabaraka za mahakama kugombea, sina shaka na lema kurudi mjengoni
 
So bad news! Anyway, kila jambo lina wakati wake na kila mwenye haki atastahili haki yake kwa wakati muafaka.

Wadau kama kuna mtu anahukumu yote please aiweke hapa ili tuijadili na tuone ikiwa kuna any merits ktk maamuzi hayo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom