Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Hivi kama Matusi yanamwondoa Lema Bungeni,Kwahiyo Mahakama Inatuthibitishia kwamba Pamoja na Kuwa Jakaya Kikwete aliiba kura kupitia NEC na Maaskofu wa Kanisa katoliki na KKKT pamoja na Mufti Sheikh Simba kuingilia kati kumwambia Dr.Slaa akubali matokeo kuepusha kuvunjika amani(Maana siku ile anaituhumu TISS ilikuwa ndio mwanzo wa mbilike,sema busara yake na watu hao niliowataja) japo aliibiwa ni dhahiri nchi haina Rais?Maana na wao walimtukana Dr.Slaa hivyo kwa mujibu wa Case Law(Precedents) uamuzi wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufaa una kuwa ni SHERIA,hivyo Kikwete sio Rais??
 
we haujisomi mtakalia majungu na mipasho tu sisi jimbo tutalichukua muwalete na kina lusinde wenu CDM tutazdi kung'ara tu.
:rockon:
 
sauti ya watu ni sauti ya mungu, you may chain the tongues of men but you will never touch their mind. nasubiri hukumu tuisome tuone nguvu ya ushahidi lakini tuijuanvyo nchi hii jaji ni mteule wa raisi ambaye ni mwenyekiti wa chama kinachoona donge kwa lema unategemea nini?. chadema kimeanza na mungu na kitamalizia na mungu. jambo muhimu ni kukata rufaa haraka ili lema aendelee kuwa mbunge alafu chadema watafute hela wakati wanasubiri maamuzi ya mahakama ya rufaaa ambayo yatakuwa hayo hayo wataingia kwenye uchaguzi na uwezo mzuri maana gharama zilioshatimika kwa arumeru ni nyingi.

ila lisilo la kusahau mataji wa watu ni zaidi ya pesa, kwa hili hata mimi nitajitolea kuwa wakala wa kusimamia kura zisiibwe.
 
Mzee wa richmond..,mh.fredrick lowassa sasa atahakikisha anamwaga pesa ccm (chama cha matutsi) kushinikiza mtoto wake fredrick lowassa apitishwe kugombea ubunge arusha mjini..! Baada ya mkwe wake sioi sumari kushindwa ubunge arumeru mashariki..! Nape mnauye upooooooo! Huu ni mwendelezo wa ufalme wa lowassa kutaka kupata madaraka
 
ule muda wa kupoteza pesa za wananchi kwa uchaguzi umefika hilo jambo walishaliplan tangu siku nyingi thats why walikubali kushindwa kirahisi wakijua wataleta mambo yao hawajari pesa zetu siasa za africa zimejaa uchafu ila hata iweje CCM ni ngumu kushinda huku Arusha.
 
Hapajanuka.....ila panatarajiwa kunuka, thou mbunge wetu ametuomba tusikinukishe................
 
Chadema na helicopter yenu ndio mshapoteza jimbo hivyo sasa CCM ndio watashika hatamu hapo mjini ,mtake msitake ubunge wa Arusha mjini utakwenda kwa CCM,
 
Chini ya utawala wa ccm hii hakujawahi kuwa na haki kwa wanyonge na haitakaa itokee haki ikatolewa kwa wanyonge. Ni jukumu letu sasa kuhakikisha 'at any cost' ikibidi uhai wetu, tunauondoa utawala huu dhalimu kwa mustakabali mwema na ustawi wa nchi yetu na watz kwa ujumla.

Watz wenzangu wapenda nchi hii tupambane kuikomboa nchi yetu kutoka mikononi mwa watu wasiopenda kutenda haki, mafisadi, wezi na wengine wa kariba hii kwa njia yoyote iliyokaribu yetu. Tutumie mitandao ya kijamii, 'word of mouth' print media, tv na njia zinginezo na tusichague 'battle ground' kwani adui yetu anapambana nasi mahali na wakati wote, na kubwa zaidi tuwe wazalendo wakati wote wa mapambano hayo na tujitolee kwa nafsi na mali.
 
matumizi mabaya ya madaraka, fedha na ofisi ni kitu cha kawaida sana kwa serikali ya ccm, chaguzi ndogondogo ni moja ya matumizi mabaya ya fedha za umma, uamuzi wa kumvua lema ubunge ni shinikizo la kisiasa kutoka upande wa pili. Lakini ccccccccmmmm wajue kwamba wamechokwa na hawana future katika nchi ya tz
 
Lama ameongea Live redioni na kusema maamuzi ya mahakama ni shinikizo la Ikulu, na anasema aliambiwa toka jana na Kamanda wa Polisi kuwa awe tayari kwa lolote litakalotokea upande wake na pia awadhibiti wafuasi wake!
 
tusburi kuona majigambo ya hao mashahidi wa magamba mtaani laana pombe na ukimwi lazima ziwamalize
 
napenda kuwapa pole mh lema na makamanda wote hapo a town lakini kwa kuwa sisi tuna mungu tujipange upya kuweza kulirudisha jimbo maadamu hawakukupiga stop kugombea mungu yu pamoja nasi tutashinda tu.

kasema tusimpe pole..tumwambie jipe moyo!
 
Hamjanyimwa kumchukulia hatua Lusinde...alikosea, kama mnataka na nyie mshitakini!!

sisi huwa tunashitaki kwa wananchi. ccm mnajifanyia homicide. hamna huruma na watanzania. pesa ya kuendesha uchaguzi ingetumika kwa mambo mengine ya kimaendeleo kwa watu.
 
AND I QUOTE,

"Baada ya mahakama ya Arusha kumvua ubunge aliyekuwa mbunge wa Arusha mh Lema, pia mahakama imemwambia sheria inamruhusu kugombea tena bila kipingamizi na ametakiwa kulipa gharama zote za kesi iliyoendeshwa, na LEMA kakubali hukumu na kufurahi kuwa mahakama imemruhusu kugombea na kasema atalipa hizo gharama za kesi"

END OF QUOTE
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom