Gavana Balali Ajiuzulu!

1. Kwa sasa apigane tu na maradhi aliyokuwa nayo- tuzidi kumwombea apate nafuu ili aihudumie familia yake.

2. Hata mke wa Dr. Idris Rashid alipofariki kwa ugonjwa wa kukonda sana 1999 watu walisema ni ngoma- ila hadi leo Dr. Rashid yupo TANESCO na bado tu anadunda!


Na Magic Johnson anadunda tu since 1992. Na Mzee Charles Nyirabu alidunda tu for 8 more years since his so-called mistress of Moshi died. So did Dr. Khalid wa Makondeko. The list goes on and on........

Mzalendohalisi, I just hope that you are smart enough NOT to believe, in more than one way, what you have just implied there.

Ndiyo maana watu wanapukutika sana, kwa kuwa tunapimia macho.
 
Na Magic Johnson anadunda tu since 1992. Na Mzee Charles Nyirabu alidunda tu for 8 more years since his so-called mistress of Moshi died. So did Dr. Khalid wa Makondeko. The list goes on and on........

Mzalendohalisi, I just hope that you are smart enough NOT to believe, in more than one way, what you have just implied there.

Ndiyo maana watu wanapukutika sana, kwa kuwa tunapimia macho.

Well stated.
 
Mhh.. alijisemea mzee ruksa hili gonjwa limetushika pabaya!!!

well ngoma si tatizo watu wanadunda hata zaidi ya 20 yrs!, hapa swala ni huyo babu asije kuwa mgeni wa malaika kabla ya kutwambia hasa ilikuwaje? kama hakushiriki, la, naye kama alichota hayo majumba yake ya majuu yapigwe bei turudishiwe kilicho chetu bila kusahau hao binamu zake kina green nini sijui??
 
think nyie watu mnakwenda beyond,hata kama aliiba sio kuanza kudiscuss na kufurahia jamaa ni mgonjwa na kufanya afya yake ni issue hapa na kuanza kutaja majina ya watu humu eti wana ngoma nafikiri thats beyond foolishness & better quit that nonsense...wengine wenu humu mnaopiga hayo matarumbeta ni wagonjwa tuu ila ustaarabu hamna hata kidogo.
 
Well said Koba,
issue siyo ugonjwa jama, I keep on saying swala ni our money money money?? where are they?? and how to get them back period!
 
Gavana Daudi Balali ajiuzulu

*Amwandikia Kikwete barua akiwa Marekani


Na Mwandishi Wetu

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Daudi Balali, amejiuzulu.

Habari za Gavana Balali kujiuzulu, zilipatikana Dar es Salaam jana kutokana na barua aliyomwandikia Rais Jakaya Kikwete akiwa Boston, Marekani, ambako amelazwa akitibiwa.

Nakala ya barua hiyo ambayo Majira iliipata jana, inaonesha kuandikwa juzi na kusainiwa na Bw. Balali mwenyewe, ikieleza kuwa kutokana na afya yake, hawezi kuendelea kutimiza wajibu wake kikamilifu.

"Mheshimiwa, kama unavyoelewa, nimelazwa hospitalini kwa zaidi ya miezi mitatu sasa hapa Boston, Marekani, kutokana na upasuaji mkubwa niliofanyiwa.

"Kwa matatizo yaliyojitokeza ya hali yangu ya kiafya, sioni kama kuna dalili za kuonesha ni lini nitakuwa nimepona kabisa na hata kuendelea na wajibu wangu kikazi.

"Kwa mazingira hayo, naona inafaa niachie nafasi hii na hivyo naandika barua ya kujiuzulu kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania," barua hiyo ya ukurasa mmoja ilisema.

Ili kufahamu kama barua hiyo imefika Ikulu na ni nini majibu yake, Majira iliwasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu, ambaye alisema hakuna mawasiliano yoyote rasmi yaliyokwishafanywa kati ya Gavana na Rais.

"Mpaka sasa ninapozungumza nawe, hakuna mawasiliano yoyote rasmi kati ya pande mbili hizi husika, lakini kama yatakuwapo yatashughulikiwa kwa taratibu na kanuni za kawaida zilizopo na vyombo husika," alisema Bw. Rweyemamu.

Hatua hii ya Bw. Balali imekuja huku uchunguzi wa ubadhirifu ndani ya BoT ukiwa tayari umekamilika na ripoti amekabidhiwa Rais kwa hatua zaidi.

Uchunguzi huo uliagizwa na Serikali kufanyika ili kubaini kama kulikuwa na ubadhirifu ndani ya BoT hasa ukishusisha ujenzi wa majengo mawili 'twin towers' ya Benki hiyo.

Serikali ilifanya uchunguzi huo kupitia Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambapo Kampuni binafsi ya Uingereza ya Ernst & Young ilifanya ukaguzi huo na kuwasilisha ripoti yake kwa Rais.

Uchunguzi huo ulitokana na shinikizo kutoka kambi ya Upinzani ambayo kupitia Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa, ilitangaza ilichokiita orodha ya mafisadi, huku Gavana Balali akiwa mmoja wa waliotajwa kuhusiana na ubadhirifu ndani ya BoT.

Kutokana na shinikizo zaidi kutoka Upinzani kutaka Rais Kikwete atoe kilichomo katia ripoti hiyo, juzi CCM kupitia kwa Katibu wake Mwenezi, Bw. John Chiligati, aliwataka wanasiasa kuvuta subira ili baada ya mapitio ya ripoti hiyo, Rais atautangazia umma.

Juzi akizungumza na waandishi wa habari, Rais Kikwete aliulizwa kuhusu aliko Bw. Balali kutokana na hisia kuwa pengine amekimbia kashfa ya BoT, alisema yuko Marekani anaumwa na yuko kwenye matibabu.

Source: Majira
 
All I can say is that Rweyemamu is lying. When Kikwete was in Washington D.C. he telephoned Daudi Balali in Boston. I am not aware of what they talked about (I was not snooping) but to categorically say there has not been any communication between Mwungana and the governor is to mislead the public or an outright lie. I should expect more from a Director of Communication in Ikulu
 
mwache akimbie nchi,lakini hata kula kwa raha hizo senti

Kama katuibia lazima sheria imfuate kokote kule aliko. Mali zake zote ndani na nje ya nchi zichukuliwe na serikali Majumba yauzwe na pesa itakayopatikana iingizwe hazina. Pesa zilizokuwemo kwenye bank accounts zote zirudishwe hazina na Marekani waombwe huyu jamaa arudishwe Tanzania ili afunguliwe mashtaka. Meghji alikuwa anatetea hakuna kasoro zozote katika accounts za BOT, kama zipo basi na yeye awajibike aachie ngazi haraka sana.
 
Wana JF
So far Balali amesema amejiuzulu kutokana na sababu za kiafya, and in my opinion he is smart enough kuchagua kujiuzulu akiwa Marekani na kwa kisingizio hicho. Lakini kwa wenye akili timamu mnajua kabisa sababu iliyomfanya ajiuzulu, na hasa iliyomfanya akimbilie Marekani kwenda kujiuzulu. Ina my opinion amefanya la maana, kwa sababu angefanya hivyo nyumbani au angeamua kupelekwa muhimbili huenda tungesikia amekufa kwa shinikizo la damu.
Hapa tunataka kuchezewa mchezo mmoja wa ajabu sana, hiyo ripoti ambayo mpaka leo imekaliwa, soon tuaambia inam-implicate Balali peke yake na vidagaa kadhaa. Let us wait and see.
Few weeks ago Comrade Kingunge alisema hakuna ufisadi serikalini, Mwanri akafuata, na wengine wakaendelea kusema same same, i hope waandishi wa habari hapa Bongo watakuwa na akili ya kuwahoji tena watu haohao baada ya ripoti kuwekwa hadharani, ili waseme kama walikuwa wanatuzuga au walikuwa hawajui walichokuwa wanakisema.
 
Dr. Balali hakuwa mwizi, yeye alifacilitate utoaji pesa hizi kunusuru Serikali (CCM) kutumia makampuni hewa (Meremeta, TanGold, Mwananchi Green) kujipatia pesa.

Sisi tunafanya makosa kwa kuwa na fukuto kama moshi wa kifuu. Hawa kina RO, EL, JK na mafisadi wataendelea kupeta, kwa kuwa Watanzania, hamna uwezo wa kufanya kweli na kuleta mageuzi.

Chaguzi za Mitaa na Serikali za Mikoa mtapewa Biriani na Kofia, wote mtageuka minara ya chumvi kama mke wa Lutu na kuwapigia kura CCM iendelee!

Chadema, wakimbilia kutoa habari hovyo hovyo kama gazeti la Udaku alasiri, ndio maana kila kitu wanachosema na kuleta hadharani havipewi maanani.

Jamani tuachieni sisi hiyo kazi ya kuchafua watu majina, nyie jengeni nyumba ya kuiangusha CCM 2010.

As of Balali (By the way Balali ni Mlutheri kwa kuzaliw na si Muislamu kama wengi wenu mnavyofikiri), we should wish him a speedy recovery and perhaps one day he will tell us what happened.

Yanayomkuta Balali, yanafanana na ya Golman Rutihinda, ingawa sijui ni Ufisadi gani ulifanyika na kumtoa kafara Rutihinda!

Tanzania ni nchi hatari, ni heri Balali aendelee kukaa Unyamwezini ale pensheni yake ya Benki ya Dunia!
 
Kama katuibia lazima sheria imfuate kokote kule aliko. Mali zake zote ndani na nje ya nchi zichukuliwe na serikali Majumba yauzwe na pesa itakayopatikana iingizwe hazina. Pesa zilizokuwemo kwenye bank accounts zote zirudishwe hazina na Marekani waombwe huyu jamaa arudishwe Tanzania ili afunguliwe mashtaka. Meghji alikuwa anatetea hakuna kasoro zozote katika accounts za BOT, kama zipo basi na yeye awajibike aachie ngazi haraka sana.


Bubu sio Meghji peke yake, kuna wengi sana walitetea kuwa wapinzania ni waongo. Kingunge ndio aliitisha kabisa mkutano na waandishi wa habari na kusema kelele za waoinzania ni distraction tu, hazina ukweli wowote.... the list goes on and on. Aliyesema ukweli ni Jaka Mwambi peke yake. Kama kweli tukiwa na akili ripoti za Richmond, BOT,...zikitoka lazima hao watu waulizwe tena. Unless wajitetee kuwa wao wanatumiwa tu.
Kuna wakati haya mambo yanakasirisha sana
 
Kuna jamaa mmoja mbongo hapa mjini anafanyakazi part time kwa Rev. Stith, nitaonana nae jumamosi......hopeful anajua whereabouts za Balali hasa kama ni kweli yupo Boston.

Kaka(jina kapuni) samahani, lakini ukifika Boston ni PM. Jiandae kuna baridi kali na snow mingi sana, kwahiyo boots na makoti mazito muhimu........otherwise safari njema.
 
Ballali bows out Cites major health reasons

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam


THE long-beleaguered governor of the Bank of Tanzania (BoT), Dr Daudi Ballali, has resigned.

Government sources confirmed to THISDAY yesterday that Ballali quietly tendered his resignation letter to President Jakaya Kikwete on Wednesday this week, citing serious health reasons.

''The governor cites complications in his medical condition following major surgery as the main reason for his resignation,'' a source said, adding: ''It is expected that the president will accept his resignation without too much ado''.

According to other government sources, Ballali is understood to have met with Mr Kikwete during the president's latest trip to the United States hardly a week ago.

The erstwhile central bank supremo, whose resignation after seven years at the helm comes on the back of a raft of corruption allegations against him, has reportedly been undergoing treatment at a hospital in Boston, US for the past three months-plus.

He is reported to have left the country for the States before the start of a special audit on the BoT, ordered in the wake of suspicions of serious improprieties in the external payment arrears account.

For the better part of this year, Ballali had been battling against allegations of personal involvement in the apparently massive funds misuse at the BoT.

He has also faced increasingly-loaded questions over issues like the ever-ballooning costs of the BoT Twin Towers construction project; excessive legal fees paid out by BoT amounting to billions of shillings; and hefty but dubious payments to the now-defunct Meremeta Gold Mine Company Limited, Tangold, Mwananchi Gold Company and the Alex Stewart Asseyers audit firm.

But at a news conference in Dar es Salaam back in July, he declared that the allegations against him were ''malicious lies and fabrications'', while steadfastly refusing to step down as governor.

There are reports that the Controller and Auditor-General, Ludovick Utuoh, will soon be submitting to the government the much-awaited BoT external payment arrears account audit report.

The government has been under growing pressure from its various development partners to act on the widespread allegations of corruption at the BoT and elsewhere. Some partners have also publicly threatened the government with delays in disbursement of aid if decisive action was not taken in this regard.

There was no immediate comment from State House or the Ministry of Finance on Ballali's reported resignation.
 
•
Gavana Daudi Balali ajiuzulu

sogeza Habari Zinazoshabihiana
• Balali: Kushuka thamani ya shilingi hakutaathiri uchumi 27.10.2006 [Soma]
• Balali apasua bomu 13.07.2007 [Soma]
• Obasanjo akubaliana na mawazo ya Gavana Balali 15.07.2007 [Soma]

*Amwandikia Kikwete barua akiwa Marekani

Na Mwandishi Wetu

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Daudi Balali, amejiuzulu.

Habari za Gavana Balali kujiuzulu, zilipatikana Dar es Salaam jana kutokana na barua aliyomwandikia Rais Jakaya Kikwete akiwa Boston, Marekani, ambako amelazwa akitibiwa.

Nakala ya barua hiyo ambayo Majira iliipata jana, inaonesha kuandikwa juzi na kusainiwa na Bw. Balali mwenyewe, ikieleza kuwa kutokana na afya yake, hawezi kuendelea kutimiza wajibu wake kikamilifu.

"Mheshimiwa, kama unavyoelewa, nimelazwa hospitalini kwa zaidi ya miezi mitatu sasa hapa Boston, Marekani, kutokana na upasuaji mkubwa niliofanyiwa.

"Kwa matatizo yaliyojitokeza ya hali yangu ya kiafya, sioni kama kuna dalili za kuonesha ni lini nitakuwa nimepona kabisa na hata kuendelea na wajibu wangu kikazi.

"Kwa mazingira hayo, naona inafaa niachie nafasi hii na hivyo naandika barua ya kujiuzulu kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania," barua hiyo ya ukurasa mmoja ilisema.

Ili kufahamu kama barua hiyo imefika Ikulu na ni nini majibu yake, Majira iliwasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu, ambaye alisema hakuna mawasiliano yoyote rasmi yaliyokwishafanywa kati ya Gavana na Rais.

"Mpaka sasa ninapozungumza nawe, hakuna mawasiliano yoyote rasmi kati ya pande mbili hizi husika, lakini kama yatakuwapo yatashughulikiwa kwa taratibu na kanuni za kawaida zilizopo na vyombo husika," alisema Bw. Rweyemamu.

Hatua hii ya Bw. Balali imekuja huku uchunguzi wa ubadhirifu ndani ya BoT ukiwa tayari umekamilika na ripoti amekabidhiwa Rais kwa hatua zaidi.

Uchunguzi huo uliagizwa na Serikali kufanyika ili kubaini kama kulikuwa na ubadhirifu ndani ya BoT hasa ukishusisha ujenzi wa majengo mawili 'twin towers' ya Benki hiyo.

Serikali ilifanya uchunguzi huo kupitia Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambapo Kampuni binafsi ya Uingereza ya Ernst & Young ilifanya ukaguzi huo na kuwasilisha ripoti yake kwa Rais.

Uchunguzi huo ulitokana na shinikizo kutoka kambi ya Upinzani ambayo kupitia Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa, ilitangaza ilichokiita orodha ya mafisadi, huku Gavana Balali akiwa mmoja wa waliotajwa kuhusiana na ubadhirifu ndani ya BoT.

Kutokana na shinikizo zaidi kutoka Upinzani kutaka Rais Kikwete atoe kilichomo katia ripoti hiyo, juzi CCM kupitia kwa Katibu wake Mwenezi, Bw. John Chiligati, aliwataka wanasiasa kuvuta subira ili baada ya mapitio ya ripoti hiyo, Rais atautangazia umma.

Juzi akizungumza na waandishi wa habari, Rais Kikwete aliulizwa kuhusu aliko Bw. Balali kutokana na hisia kuwa pengine amekimbia kashfa ya BoT, alisema yuko Marekani anaumwa na yuko kwenye matibabu.
 
this seems to be like Wednesday news.. we have to change this.. haiwezekani habari ya Jumatano tunasoma Ijumaa! are we in a kind of time warp in sector 17?
 
Back
Top Bottom