Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 617
- Thread starter
- #81
Re: KLHN Breaking News - Gavana Balali Ajiuzulu!
--------------------------------------------------------------------------------
Nyani Ngabu soma hapa.. Lakini nadhani sidhani kama huo mjadala unaouleta una maana yoyote katika hii mada. Na hii headline ndio iliyopasua jipu, japo inawezekana wote, Halisi na Hasara walikua wakijua kwa hakika kabisa kuhusu Kujiuzulu (Kujiuzuliwa) kwa Ballali.
--------------------------------------------------------------------------------
Quote: Nyani Ngabu
Ndiyo, sitaki hadi unionyeshe pale KLHN News walikuwa wa kwanza kui-break...
Kwenye tovuti kuna 'Eid Njema sijui Eid Muabarak'....hapa poster wa kwanza alikuwa Hasara au Halisi (sorry I tend to mix up the 2)...so where does KLHN fit into this?
naweza kukufanyia hiyo homework but then it won't be fair. Wewe angalia sehemu zote na uone ni nani aliyesema "Balali Ajiuzulu" kwanza. Halafu njoo nisahihishe.
Nyani Ngabu soma hapa.. Lakini nadhani sidhani kama huo mjadala unaouleta una maana yoyote katika hii mada. Na hii headline ndio iliyopasua jipu, japo inawezekana wote, Halisi na Hasara walikua wakijua kwa hakika kabisa kuhusu Kujiuzulu (Kujiuzuliwa) kwa Ballali.
Today, 07:13 PM
Mzee Mwanakijiji
JF Senior Expert Member Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 6,632
Rep Power: 36
Thanks: 818
Thanked 1,383 Times in 681 Posts
Credits: 144,121
KLHN Breaking News - Gavana Balali Ajiuzulu!
--------------------------------------------------------------------------------
Habari za kuthibitishwa zinasema kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Bw. Daudi Balali amejiuzulu wadhifa wake huo kutokana na sababu za kiafya. Gav. Balali alikuwa ameenda Marekani kwenye jimbo la Massachusetts jiji la Boston ambako alikuwa ameenda kufanya upasuaji. Gav. Balali katika barua yake kwa Rais amesema kuwa kutokana na "sababu za kiafya" hatoweza kuendelea na wadhifa huo. Ikumbukwe kuwa Gav. Balali aliandamwa na tuhuma nyingi katika chombo hicho cha Benki Kuu kwa muda mrefu sasa na watu wengi wakiwemo viongozi wa upinzani wamekuwa wakimtaka Rais amwajibishe.
Hata hivyo wachunguzi wa mambo ya kisiasa na wale waliokuwa wanafuatilia suala hilo la tuhuma za ufisadi wanatambua kuwa katika sakata hilo Bw. Balali hakuwa peke yake na kuna dalili za vyombo na watu wengine mashuhuri kuhusika katika ufisadi huo na hivyo yeye Balali kuwa ni mtolewa kafara wa kwanza.
Kufuatia habari za kujiuzulu kwake ambazo KLH News ilianza kuzisikia tangu jana, kuna uwezekano mkubwa kabisa wa Gavana huyo kutoweza kurudi nyumbani kabisa kutokana na sababu "mbalimbali" ambazo hazitaweza kuzuilika.
M. M.
__________________
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8267&page=3