Gavana Balali Ajiuzulu!

Gavana Balali Ajiuzulu!

this seems to be like Wednesday news.. we have to change this.. haiwezekani habari ya Jumatano tunasoma Ijumaa! are we in a kind of time warp in sector 17?

Kibaya zaidi news kama hiyo ilitakiwa iwe imetolewa na Ikulu, lakini tunapata news hiyo kutoka upande wa pili wa shilingi. Kwa maneno mengine iko based kwenye barua ya Ballali.

Nadhani report ya ukaguzi wa mahesabu ya BoT ina utata na ndiyo maana Ikulu imekuwa nzito kutoa taarifa. Hapo kuna mtego, je, wakimkubalia atakaa kimya au atakuja kupayuka? What if wananchi wakitaka achukuliwe hatua, ni njia gani itatumika kumlinda ili asije akamwaga upupu kwa wengine waliolamba bingo la BoT. Hapo lazima watu wa kitengo wafanye kazi ya ziada ili kuhakikisha kwamba hiyo resignation haitakuja kuwalipukia na hasa pindi jamaa atakapokuja kubanwa ataje waliolamba bingo.
 
KUJIUZULU TU HAKUTOSHI, HUYU BALALI NADHANI AMELIINGIZA TAIFA KWENYE HASARA KUBWA YA WIZI NA UBADHIRIFU WA FEDHA ZETU AKISHIRIKIANA AU KUWAUNGA MKONO MAFISADI KATIKA KUIPORA HAZINA YETU PALE BoT.

ICHUNGUZI UKIMALIZIKA ACHUKULIWE HATUA ZA KISHERIA NA MALI/FEDHA WALIZOIBA WAZIRUDISHE!
 
Hapo nimechoka. Kwa hiyo JK alishazungumza naye wakati akiwa NY, which means he knew what Ballali wa up to or that is what they discussed. Hivi huko USA nani alimpeleka kutibiwa?? Maana kwa wadifa wake nafikiri BOT walitakiwa wampeleke. Sasa kama alijipeleka mwenyewe then everything was planed well ahead!!
 
Well the Bigman has gone now.. the question is who gonna be our new Gavana? Kimei, Rashid (again?) Blandina Nyoni, Dr Dau, Juma Reli....
 
Well the Bigman has gone now.. the question is who gonna be our new Gavana? Kimei, Rashid (again?) Blandina Nyoni, Dr Dau, Juma Reli....

Si Dr. Dau na Juma Reli waliwekwa pale kumsaidia kama siyo walikuwa wansubilia jamaa atemwe (ajiteme mwenyewe) then wapewe mlo wao. Unajua TZ BOT ni lazima kila rais aweke mtu wake ndiyo anfurahi. AMH alimweka Idrisa, BWM akamweka Ballali sasa kikwete atamweka wake. Mimi naona pale mahali hata uwe mchapakazi vipi, rais akibadlika tu lazima na wewe uondoke. Idrisa aliondoka kwa uchungu BOT mpaka tukafikiri hatakujarudia tena kazi za kuteuliwa serikalini au mashirika ya umma. Kwa ujumla BOT ni sehemu ya ulaji wa vigogo wa Bongo, period!!
 
Duuh! hizi habari ni za kweli? naona mnatoa habari na link haziwekwi
 
Nawakumbusha maneno aliyosema DR.Slaa wakati ule ilipotolewa taarifa kuwa Balali ameenda kutibiwa marekani , alisema namnukuu/ kuna taarifa kuwa huyu amepelekwa huko ili asirudi tena nchini / na hayo maneno yalikuwa yana ukweli mkubwa ndani yake na hapa huu ni ushuhuda tuu unaendelea kutokea hapa wandugu.

Jumuiya ya kimataifa imeendelea kuwabana hawa jamaa kuhusu ripoti ya BOT na hata juzi Mbowe kwenye ufunguzi wa mkutano wa baraza kuu la chama chake aliweza kulisema hilo na la kushangaza CCM chini ya Chiligat wakasema rais asishurutishwe kutoa majibu hadharani kwani muda ukifika ataiweka ,na hapao hapo waziri wa fedha akasema kuwa CAG yupo nje ya nchi na akirudi ataweza kuikabidhi kwake...

Naendelea kufuatilia na kuna taarifa kuwa kuna timu ya watu wa hazina walikuwa Ngurdoto kwa ajili ya kuifanyia kazi ripoti hiyo kwa zaidi ya mwezi mmoja, sasa .
 
Nawakumbusha maneno aliyosema DR.Slaa wakati ule ilipotolewa taarifa kuwa Balali ameenda kutibiwa marekani , alisema namnukuu/ kuna taarifa kuwa huyu amepelekwa huko ili asirudi tena nchini / na hayo maneno yalikuwa yana ukweli mkubwa ndani yake na hapa huu ni ushuhuda tuu unaendelea kutokea hapa wandugu.

Jumuiya ya kimataifa imeendelea kuwabana hawa jamaa kuhusu ripoti ya BOT na hata juzi Mbowe kwenye ufunguzi wa mkutano wa baraza kuu la chama chake aliweza kulisema hilo na la kushangaza CCM chini ya Chiligat wakasema rais asishurutishwe kutoa majibu hadharani kwani muda ukifika ataiweka ,na hapao hapo waziri wa fedha akasema kuwa CAG yupo nje ya nchi na akirudi ataweza kuikabidhi kwake...

Naendelea kufuatilia na kuna taarifa kuwa kuna timu ya watu wa hazina walikuwa Ngurdoto kwa ajili ya kuifanyia kazi ripoti hiyo kwa zaidi ya mwezi mmoja, sasa .

Hivi huko Gurdoto kuna nini??? Maana kila kukicha Ngurdoto au ndiyo serikali imeikodisha hiyo lodge kufanyia kazi zake???
 
Hivi huko Gurdoto kuna nini??? Maana kila kukicha Ngurdoto au ndiyo serikali imeikodisha hiyo lodge kufanyia kazi zake???

Serikali ina hisa Ngurdoto ... mali kwa mali! Kwanini wapeleke faida kwa washenzi wengine wakati kitega uchumi chao kinadoda? Vikao vyote vya serikali huwa vinafanyika off-season ili ku-maximize mapato. Usishangae ukisikia serikali inalipia chumba kwa shilingi 200,000 na akienda mtu binafsi analipa shilingi 100,000 ndo mambo ya Bongo hayo!!!!
 
Naendelea kufuatilia na kuna taarifa kuwa kuna timu ya watu wa hazina walikuwa Ngurdoto kwa ajili ya kuifanyia kazi ripoti hiyo kwa zaidi ya mwezi mmoja, sasa.

Wanaifanyia kazi gani? Ama wanatafuta justification za querries zilizo kwenye hiyo report ya Mathawee?

Audited Reports zote huwa zinatakiwa ziwe na seal/sahihi ya Auditor. Sasa wao wakii-doctor hiyo report, sahihi/seal ya Mathawee na Ernst wataipata wapi? Labda kama wakija na style ya PCCB ambapo Dr. Hoseah alionyesha ile report ya Richmonduli kwa nje tu bila hata kuonyesha contents kwa waandishi wa habari. Kwa hiyo ili kuwa na uhakika na report hiyo lazima tupate authenticity ya hiyo report kwa kuangalia seal/sahihi za ma-auditor vinginevyo itakuwa batili.
 
Dr. Balali hakuwa mwizi, yeye alifacilitate utoaji pesa hizi kunusuru Serikali (CCM) kutumia makampuni hewa (Meremeta, TanGold, Mwananchi Green) kujipatia pesa.

Sasa tofauti yake ni nini? Kuwa mwizi....na kufacilitate utoaji pesa kupitia makampuni hewa
 
MODs mnaweza kuiunganisha hii na mada yake baada ya muda or at your own discretion. M. M.

balalikujiuzulu.jpg
 
But mbona haina Title?

Inaelekea yuko mahtuti hata jinsi ilivyokuwa costructed inatisha,

Au amelazimishwa kujiuzulu ndio maana kaiandika kihuni
 
yaweke humu kwanini unayasitiri rafiki yangu , naomba kubali kuwa mtu wa watu tumwagie kila kitu halafu hao wanaotaka kujua umbali ama ukaribu wako waache kuchangia maana shida yake ni kujua visivyo muhimu kwake.
 
Asante Mwanakijiji kwa hii barua!

This is JF, kila kitu kinapatikana kikiwa bado moto kabisaaa!
Wenye vikorosho wajinyonge but this baby will be here to win.

Kuhusu Balali, Nimesema mengi ya kutosha!

BTW. Hii barua si inaweza kupunguzwa ukubwa. Mkjj jaribu kuadjust size kidogo
 
Mama Lao,

Apende asipende he had no choice but to give out money to bail out serikali (CCM)! hata kama angekataa, the next guy was going to face the same dillema and had to either accept what the Government wants or surrender!

Nyinyi mwafikiri ni pesa zinazotoka kirahisi bila ruhusa ya Raisi na Waziri wa Fedha? Nope! Ukirudia mada yangu kuhusu Meremeta utaelewa ni nini kilichotokea. Kibaya zaidi ni kuwa Uchunguzi huu utaleta vurugu mechi ambayo hatutataka kuina kamwe.

When did you see Jeshi being investigated? who has balls to investigate CCM and its arms?

Mwacheni Kondoo wa Kafara atulie huko unyamwezini! The only way for the truth to come out is for CCM loosing the control of parliament in 2010!

Hiyo ripoti itakaliwa Ikulu na Rais atasema kwa Taifa hakuna ushahidi wa Wizi na Sifukuzi Mawaziri!

But collectivelly, we can make the thruth even partial to come out 2011 if we vote more seats to opposition in the parliament!
 
Re: KLHN/JF Exclusive: Barua ya Balali Kujiuzulu

--------------------------------------------------------------------------------

But mbona haina Title?

Inaelekea yuko mahtuti hata jinsi ilivyokuwa costructed inatisha,

Au amelazimishwa kujiuzulu ndio maana kaiandika kihuni

Bowbow, kwanza naona kama "UNAGUSWA" sana na hii mada, toka juzi. ila kwa taarifa ni kwamba:

Nimewahi kuona barua nyingi za Ballali, kama ile waliyoandikiana na Warioba kuhusu fedha za Mwananchi Gold, haikuwa na heading na mbaya zaidi iliandikwa kirafiki mno, ikirejea mazungumzo ya mdomo, kwa hiyo si ajabu, japo sentesi yako ya mwisho inahitaji kufanyiwa kazi zaidi
 
Wataalam wa barua hushauri kuwa: Ukiondoka pahala pa kazi katika hali ya mfarakano, basi usiandike mengi kwenye barua yako ya kuacha kazi.

Katika hiyo barua juu, hilo jambo linajidhihirisha kimapana..

SteveD.
 
Back
Top Bottom