Gavana Balali Ajiuzulu!

Any update from JK kuhusiana na kujiuzulu kwa Gavana au ripoti ya uchunguzi wa BOT?
 
Wakuu wa kaya na wanakaya ya JF

Cha kushangaza ukisoma ile thread ya ugonjwa wa balali kuna watu wancomplain kuhusu serikali kutotoa taarifa za ugonjwa wa Balali and his wareabout. Mtu/watu huyo huyo au hao hao anasema anayoreport ya ukaguzi BoT lakini hataki kuitoa wazi

Je nyie wote sio mafisadi kama wao(serikali)? Kama tutasema muda muafaka bado, kwa nini tusiamini na serikali inasema muda muafaka bado wa kutoa maradhi ya Balali(hadi kifo kimkute).

Hakuna sababu ya kutambiana tunayo wakati hakuna aliyonayo ili tuweke juhudi za kuipata.

Nawakilisha
 
Mimi binafsi sina tatizo na serikali kufanya ugonjwa au hali ya Gavana siri. Hata hiyo ya kutosema alipo au hospitali aliyolazwa. Ni haki yao na mhusika yaani Gavana mwenyewe. Kinachonistua ni pale balozi anaposema hajui alipo au HALI ya mgonjwa. Angesema kuwa kuwa mahali alipo mgonjwa na hali yake vitaendelea kuwa siri mpaka pale watakapoamua kutueleza nisingeona tatizo. Wengi tunajua kuwa kuna wakati madaktari wanakataza mgonjwa kutembelewa ili aweze kupumzika na hasa ukiangalia tamaduni zetu za kiafrika. Huku kukana kujua aliko na hapohapo kusema kuwa mnamhudumia ni kucomplicate mambo bila sababu.
 
Sidhani kama kuna mtu anayo ripoti hiyo ya BoT na kama yupo basi labda ameiminya kwa makusudi. Vinginevyo, kitakachotolewa kwa Rais ndiyo hicho hicho... Rais anarudi ofisini kwa siku chache wiki ijayo..
 
hii ndiyo tanzania na michezo ya kitoto kwa ishu muhimu.
kwa nini balali afichwe?
kwa nini ripoti iwe siri kiasi hicho?
kwa nini habari kuhusu kujiuzulu kwake iwe siri?
kwa nini ajiuzulu akiwa nje?
je watanzania tuna amana na nchi yetu kweli?? au ndo tumewaachia wachache waisasambue wapendavyo? tena kwa jina la dhamana ya....
 
Halisi, umeniwahi tu ndugu yangu, kwani na mimi nilikuwa nataka niweke mambo haya mchana baada ya watu kula Eid kidogo. Kwa vile umelileta hapa na mimi nikuunge mkono. Kama vile mchezo wa Chess.. you move, I move! hadi tuhakikishe watawala wanakuwa kwenye checkmate! Anyway, wana JF tumuombee Balali apone na arudi nyumbani. Hivi karibuni afisa wa ngazi za juu toka Usalama alikuwa huku kijijini na alishangazwa sana kumuona Balali bado mzima na anadunda!

Kwenye sakata la BoT Balali anaweza kutolewa kafara kama ya Isaka! Endapo Balali atanyamaza milele kama alivyonyamaza binti "YULE" basi jaribio la kuziba upande wapili wa hoja litafanikiwa.

Ni wazi kuwa kati ya watu wote waliohusika na uchotaji wa fedha benki kuu Gav. Balali yuko kwenye nafasi ya pekee kuweza kujibu mashambulizi yoyote ambayo yameandaliwa dhidi yake.

Jaribio lolote lile la kumlazimisha ajiuzulu au kumtangaza kajiuzulu au kwa namna yoyote kumfanya asirudi nyumbani mzima (kule nyuma alipoondoka tu niliandika mahali fulani kuwa msishangae akirudi kwenye box) ni jaribio ambalo lazima lipingwe, likataliwe n.k. Endapo Balali ataamua kujiuzulu au kuachia ngazi ni lazima awe katika uhuru wote wa kusema anachojua.

Ni kwa sababu hiyo basi ndugu zangu wa JF, tumuombee apone na awe huru kuzungumza. Naomba niingie kwenye rekodi na kusikika kusema kuwa BALALI AACHWE AZUNGUMZE NA ASINYAMAZE/ASINYAMAZISHWE MILELE!

M. M.
Swali ni alikufa au hakufa?
 
Halisi, umeniwahi tu ndugu yangu, kwani na mimi nilikuwa nataka niweke mambo haya mchana baada ya watu kula Eid kidogo. Kwa vile umelileta hapa na mimi nikuunge mkono. Kama vile mchezo wa Chess.. you move, I move! hadi tuhakikishe watawala wanakuwa kwenye checkmate! Anyway, wana JF tumuombee Balali apone na arudi nyumbani. Hivi karibuni afisa wa ngazi za juu toka Usalama alikuwa huku kijijini na alishangazwa sana kumuona Balali bado mzima na anadunda!

Kwenye sakata la BoT Balali anaweza kutolewa kafara kama ya Isaka! Endapo Balali atanyamaza milele kama alivyonyamaza binti "YULE" basi jaribio la kuziba upande wapili wa hoja litafanikiwa.

Ni wazi kuwa kati ya watu wote waliohusika na uchotaji wa fedha benki kuu Gav. Balali yuko kwenye nafasi ya pekee kuweza kujibu mashambulizi yoyote ambayo yameandaliwa dhidi yake.

Jaribio lolote lile la kumlazimisha ajiuzulu au kumtangaza kajiuzulu au kwa namna yoyote kumfanya asirudi nyumbani mzima (kule nyuma alipoondoka tu niliandika mahali fulani kuwa msishangae akirudi kwenye box) ni jaribio ambalo lazima lipingwe, likataliwe n.k. Endapo Balali ataamua kujiuzulu au kuachia ngazi ni lazima awe katika uhuru wote wa kusema anachojua.

Ni kwa sababu hiyo basi ndugu zangu wa JF, tumuombee apone na awe huru kuzungumza. Naomba niingie kwenye rekodi na kusikika kusema kuwa BALALI AACHWE AZUNGUMZE NA ASINYAMAZE/ASINYAMAZISHWE MILELE!

M. M.
Mzee mzee ....muda unakimbia
 
Dogo siku hizi kimya sana au unatafuna tu mihela
Huwezi kuficha siri ya wizi! Any plot that is against national interest does not qualify to be a national secret. Hao usalama waulizwe, kwa nini mkataba wa Buzwagi, Richmond nk nayo ilikuwa siri lakini tulipoitoa hawajatukamata? Kwani nyaraka za BOT alizoanza kuanika Dr Slaa nyingine si siri, mbona usalama wa taifa hawamkamati hususani kwa kuwa na ripoti yao ya usalama wa taifa waliyompelekea Lowassa ambayo imeandikwa SIRI kwa herufi kubwa? Siri inaweza kuwa kati ya wezi na wezi, lakini hakuwezi kuwa na siri kati ya wezi na wenye mali! Binafsi sijaipata hiyo ripoti, ila nimepata shauku zaidi ya kuitafuta.

Nami nawatakia wote Noeli na Mwaka mpya wenye upendo, furaha, jitihada na mafanikio.

JJ
 
Back
Top Bottom