Fukwe (Beach) za Tanzania na hatma yake

Fukwe (Beach) za Tanzania na hatma yake

Kila kitu tunauza, ilipojengwa Sheraton (sasa Movenpick) zamani palikuwa ni viwanja vya Golf, lilikuwa eneo zuri. Sasa malumbano yakaanza kuwa Hotel ikajengwe nje ya mji, lile eneo liachwe kwa michezo, nakumbuka mwanahabari mmoja wa wakati huo aliuliza ktk makala yake, nani mswahili toka Keko Akida, Msasani Mandazi Road nk anayeonekana pale akicheza Golf, wote ni waasia na wazungu, alinishangaza japo kulikuwa na ukweli. Sasa tutauza beach zote, na nyingi zimeshauzwa manake mahoteli makubwa kando ya hizi beach yanamiliki beach zao.
 
Wakulu;

Katika mapumziko ya Mwishoni mwa Mwaka 2008 nilipata wasaa wa kutembelea Beach Zetu maeneo ya Kisiju. Lakini pia huko nyuma niliwahi kutembelea Beach za Kigamboni na Bagamoyo na zote kwa urefu wa kilometa za kutosha. Pia niliwahi kutembelea beach za Mtwara.

Findings:

Kwa shuhuda za wenyeji wa maeneo hayo ni kuwa sehemu kubwa sana ya beach hizi imeuzwa kwa Wageni toka nje ya nchi ingawa uendelezaji bado haujaanza.

- Sitaki kuamini kama hizi habari ni za kweli . . .

- Sitaki kuamini kuwa Serikali haijui lolote na wala haina mipango makini ya kuendeleza beach zetu wala uhifadhi . . .

- Sitaki Kuamini kuwa Watanzania ni mbumbumbu kiasi hiki na tumelala usingizi wa Pono wakati chetu kinachukuliwa maana hata bei wanazouziwa ni za kutupa . . .

- Sitaki Kuamini . . . Sitaki kuamini . . . Sitaki kuamnini . . . . Hakuna watu wa kulipigia kelele hili wala wa kutuokoa . . .

Somebody tell me kama naota tu ama nini? Tusemezane!


Du! Mods, mbona unazichanganya mapema hivi kabla wadau hawajaona kipya ni kipi?

Haya wakulu kama mnaona imekaa sawa . . .
 
Nadhani sheria ni kwamba ukinunua kiwanja kando ya bahari au beach, ile beach yenyewe ni public property na wewe kiwanja chacko kiwe 80 meters au feet from the beach itself. Vilevile lazima kuwepo na public access to the beach from the roads zinazopakana na beach property hizo.

Sasa tatizo ni kwamba public beaches nyingi hazina toilets facilities(pale Oysterbay tunakula mihogo ya kukaanga lakini umewahi kujiuliza wale jamaa wanajisaidia wapi, na kama wanaosha mikonoi yao kabla ya kuvunjavunja muhogo wauweke ile siki na pilipili unga?) Ukienda kigamboni utaona kwamba ukiingia kupitia hoteli za kule basi ndio unaweza kwenda beach na kuja kutumia facilities za hoteli ulioingia kwa kulipia(buku tatu pale South Beach, Kipepeo etc) Watu wengi sana wanaingia through the public access na ruksa kutembea up and down the whole beach ilimradi usikae katika eneo la hoteli hizo na tena mgambo wao saa zingine wanazuia hata kukaa beach iliyo mbele ya hoteli hizi, jambo ambalo ni kosa.

Hoteli nyingi kule kigamboni licha ya kuingilia kwa kulipia pia unatumia coupon hizo kununulia vinywaji ingawa kwa bei ya kitalii - chupa moja ya soda imetengenezwa pale Mikocheni shilingi 1000! Bei yake ya kawaida ni 250 mpaka 400 - go figure!
 
DrWHO




Naona wewe sasa umelowea huku, mambo ya UK unataka yafanyike pale Bongo, hao wanafunzi wakuifanya hii kesi wako kwenye level ipi? Vile vile kumbuka hii sio mara ya kwanza kwa Coco beach kutaka kuchukuliwa kama nakumbuka vizuri enzi ya mzee ruksa kulikuwa na kitu kama hiki lakini kilizimwa. Kwa hiyo jamaa safari hii wamejiandaa na unavyojua sasa hivi ni watu wawili tu muungwana na rafiki yake ukiwaweka hao mfukoni mambo yamekwisha.

Mkuu, masuala ya pro bono si kama Tanzania hayapo.Na si lazima wanafunzi tu wafanye hiyo shughuli.Kuna taasisi nyingi za kijamii,( pamoja na para legals) sinaweza kuanzisha vuguvugu la kufanya dola ione kuna tatizo na kuchukua hatua muafaka.Aidha kuna taasisi za msaada wa kisheria ambazo huweza kufungua kesi ( public interest litigation) na nyingi zimefanikiwa mfano mzuri ni LHRC ambayo ilifanikiwa kufungua kesi na kuitaka mahakama kuu kuifutilia mbali sheria iliyokuwa inaruhusu takrima na kuitangaza takrima kama rushwa na siyo ukarimu wa kiafrika kama ambavyo spika wa zamani Pius Msekwa aliwahi kuitafsiri.Aidha mtakumbuka kazi nzuri iliyofanywa na mwanaharakati Tundu Lissu na taasisi ya LEAT katika suala la Bulyankhulu.Mifano iko mingi.Ziko pia legal aid centers nyingine kama UDSM Faculty of Law etc. Tatizo ni kuwa taasisi hizi zina mambo mengi na pengine hili suala la Coco beach kwa sasa sio kipaumbele kwao .Pengine,wananchi wangekuwa na muamko mkubwa wakaanza kulizungumzia na kuzifanya taasisi husika zichukue hatua ingesaidia.
 
Mod, naomba usiichanganye na Thread nyingine kwanza. Kuna issues nzito hapa . . . .

--------------

Wakulu;

Katika mapumziko ya Mwishoni mwa Mwaka 2008 nilipata wasaa wa kutembelea Beach Zetu maeneo ya Kisiju. Lakini pia huko nyuma niliwahi kutembelea Beach za Kigamboni na Bagamoyo na zote kwa urefu wa kilometa za kutosha. Pia niliwahi kutembelea beach za Mtwara.

Findings:

Kwa shuhuda za wenyeji wa maeneo hayo ni kuwa sehemu kubwa sana ya beach hizi imeuzwa kwa Wageni toka nje ya nchi ingawa uendelezaji bado haujaanza.

- Sitaki kuamini kama hizi habari ni za kweli . . .

- Sitaki kuamini kuwa Serikali haijui lolote na wala haina mipango makini ya kuendeleza beach zetu wala uhifadhi . . .

- Sitaki Kuamini kuwa Watanzania ni mbumbumbu kiasi hiki na tumelala usingizi wa Pono wakati chetu kinachukuliwa maana hata bei wanazouziwa ni za kutupa . . .

- Sitaki Kuamini . . . Sitaki kuamini . . . Sitaki kuamnini . . . . Hakuna watu wa kulipigia kelele hili wala wa kutuokoa . . .

Somebody tell me kama naota tu ama nini? Tusemezane!
 
Mod, naomba usiichanganye na Thread nyingine kwanza. Kuna issues nzito hapa . . . .

--------------

Wakulu;

Katika mapumziko ya Mwishoni mwa Mwaka 2008 nilipata wasaa wa kutembelea Beach Zetu maeneo ya Kisiju. Lakini pia huko nyuma niliwahi kutembelea Beach za Kigamboni na Bagamoyo na zote kwa urefu wa kilometa za kutosha. Pia niliwahi kutembelea beach za Mtwara.

Findings:

Kwa shuhuda za wenyeji wa maeneo hayo ni kuwa sehemu kubwa sana ya beach hizi imeuzwa kwa Wageni toka nje ya nchi ingawa uendelezaji bado haujaanza.

- Sitaki kuamini kama hizi habari ni za kweli . . .

- Sitaki kuamini kuwa Serikali haijui lolote na wala haina mipango makini ya kuendeleza beach zetu wala uhifadhi . . .

- Sitaki Kuamini kuwa Watanzania ni mbumbumbu kiasi hiki na tumelala usingizi wa Pono wakati chetu kinachukuliwa maana hata bei wanazouziwa ni za kutupa . . .

- Sitaki Kuamini . . . Sitaki kuamini . . . Sitaki kuamnini . . . . Hakuna watu wa kulipigia kelele hili wala wa kutuokoa . . .

Somebody tell me kama naota tu ama nini? Tusemezane!

Hiyo isikupe wasiwasi sana. Nchi bado hiko mikononi mwetu. Na tukiamka tutapindua. Wache wajenge.
 
haya, juzi wakati wa sherehe za uapndaji miti (sic) Kikwete anazilaumu tena manispaa kwa kushindwa kuendeleza beaches. Kinondoni walipojaribu kufanya hivyo kupitia kwa mwekezaji, Pinda aliwakataza. sasa wafanye nini?

Binafsi namuunga mkono sana Mh. Pinda ktk hatua hiyo... Na pia ni muhimu kwetu sisi kufahamu Kikwete alikuwa na maana gani alipozilaumu manispaa kwa kutoendeleza Beach zetu..
Tunapozungumzia kuendeleza beach haina maana ziuzwe kwa wageni au zijengwe Hotel kwa ajili ya Watalii. Inatakiwa ziendelezwe kwani navyokumbuka Coco beach na fukwe za O'bay Hospital maeneo ya Ocean road yamechakaa kiasi kwamba hata wananchi wenyewe wanakosa sehemu za kwenda punga Upepo..

Kwa hiyo sio swala la uwekezaji kwa watalii tu ndilo liwe jibu la kuendeleza beach zetu na makosa makubwa yamekuwa yakitumika kwa viongozi wetu kufikiria kwamba ni watalii peke yao wanaohitaji anasa za mapumziko..Sina kumbukumbu ya hata Bustani nzuri Dar ambayo wananchi wanaweza kwenda wakapumzika zaidi ya kuona vichaka..
 
Mimi nasema kwamba kulingana na mipango miji kuna sehemu zinazotakiwa kuwa kama 'public parks' ambako wananchi wa nyanja zote wanaweza kwenda kujivinjari alimradi tu hawavunji sheria za nchi. Mfano mzuri ni kama mnazi mmoja ingawa eneo lile badala ya kuwa public park limefingwa siku zote. Coco Beach wangeweza kuweka bustani nzuri za kupumzika na kuweka ulinzi wa kutosha maeneo hayo kwani wananchi wanalipa kodi na kazi ya kodi si tu katika kuendesha serkali bali pia kuakikisha usalama wa wananchi.

Coco beach ni eneo pekee lililobaki hapa dar es salaam ambako mlalahoi anaweza kwenda bila wasiwasi wowote.

Ubinafsi na tamaduni ya wanasiasa wetu kuwa na mawazo mgando ya kuendeleza matumbo yao na familia zao. Tumefikia mahali tunatakiwa kubadilika.

Mfumo wa umiliki wa ardhi na uvamizi wa maeneo yote bora na 'hawa wawekezaji' tutakuja kujikuta tumekuwa Kama Zimbabwe na Masettlers wa Kizungu na moto wake ukiwaka kuuzima huwa ni kazi kweli kweli.

Serikali kwa ujumla inachukulia watanzania kama mandondocha lakini wakumbuke kwamba cheo ni dhamana na waenga walisema yanamwisho haya!
 
Natumaini walioko Dar watueleze kama fukwe za bahari hasa Ocean Road kama zimeanza kutumika kupiga picha (za arusi). Creativity is mother of everything..natumaini madiwani wetu busara zitawaingia kichwani kuhusu yaliyonenwa na Mh. Rais.

Kikwete awapasha madiwani Dar
Veronica Mheta
Daily News; Thursday,January 29, 2009 @21:15

Rais Jakaya Kikwete amewataka madiwani wa Jiji la Dar es Salaam kubuni mbinu zitakazowawezesha kupata mapato badala ya kuzuia wananchi kutembelea au kupiga picha maeneo ya fukwe za bahari.

Aidha, amewataka madiwani kuacha tabia ya kuruhusu maeneo ya wazi yaliyotengwa kwa ajili ya michezo, wananchi kupumzika ambayo hivi sasa yamejengwa makazi ya watu au ghorofa za biashara.

Rais Kikwete aliyasema hayo juzi usiku Dar es Salaam katika hafla ya kumpongeza kwa utendaji wake wa kazi kwa kipindi cha miaka mitatu iliyoandaliwa na madiwani wa Jiji la Dar es Salaam. Alisema ni muhimu madiwani kubuni mbinu zitakazowasaidia kupata fedha badala ya kuwazuia wananchi kwenda maeneo ya fukwe kupiga picha za harusi au matukio mengine.

Alizitaka manispaa za Jiji kutoa tangazo kwa wananchi wanaotaka kutumia fukwe za bahari ili walipe fedha kidogo zitakazosaidia Jiji kupata fedha na si kuwazuia. “Jamani ni aibu kuwazuia wananchi kupiga picha kwenye fukwe, toeni tangazo ili wanaotaka kutumia fukwe kwa matukio maalumu wapate vibali na si kuwazuia. Pia maeneo yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya michezo au mapumziko yawe wazi…zoeni takataka jiji liwe safi kwani nchi za nje wananunua takataka na kuzalisha vitu mbalimbali,” alisema Rais Kikwete na kuongeza: “Tatizo lenu madiwani si wabunifu wa kupata mapato, kusanyeni taka na mtangaze zabuni ili watu mbalimbali waje kuzinunua kwa kufanya hivyo mtakusanya vyanzo vya mapato.”

Aliwasihi madiwani kutoruhusu ujenzi wa ghorofa kwenye baadhi ya mitaa, na badala yake anayetaka kujenga ghorofa apewe eneo linalostahili kujengwa ghorofa na si kwenye mitaa ambayo wananchi wamejenga nyumba za kawaida, akisema ujenzi huo wa ghorofa kwenye mitaa unachangia mazingira kuwa machafu kwa sababu hakuna mfumo wa kupitisha maji taka.

Pia aliwataka madiwani kuhakikisha malori ya mizigo yanaondoka eneo la Jangwani ili eneo hilo liwe wazi na vijana wapate sehemu za kucheza michezo mbalimbali, kwani enzi za zamani eneo hilo lilikuwa likitumika kwa michezo zaidi. Naye Naibu wa Jiji la Dar es Salaam, Ahmed Mwilima alisema wamezipokea changamoto hizo na kuahidi kuzifanyia kazi ili Jiji lipate mapato mengi.

Aliwataka madiwani wenzake kuacha tabia za kuogopa kujadili na kutoa uamuzi sahihi juu ya mambo mbalimbali. Aliwasisitiza kutokubali kupitisha ujenzi wa maeneo yaliyo wazi badala yake madiwani hao wasisitize maeneo yaliyo wazi kuachwa ili wananchi wapate sehemu za kupumzika au watoto kucheza; huku wakihakikisha Jiji linakuwa safi.
HabariLeo: Gwiji la habari Tanzania | Kikwete awapasha madiwani Dar
 
Maneno yake na vitendo mbalimbali ,anawalisha watu maneno matamu anatafuna kama panya ,ukiamka asubuhi vidole vyote vya miguu amenyofoanyofoa.
 
kupiga picha kwenye ardhi ya Mungu na public area ni bure.. ulipie ili kiwe nini?
 
Duuuh hii kali.....

Naheshimu mawazo yako Mh Rais.........naomba hilo wazo iwe tu changamoto(Mfano) kwa hao madiwani kutafuta vyanzo vya pesa............kutoza pesa watu kufurahia fukwe ni DHAMBI.............na watu waruhusiwe kuzitumia fukwe hizo under guidance...........

.......waambie hao madiwani wawashirikishe wadau kuzisafisha hizo fukwe.....sensitize wananchi kuhusu usafi wa fukwe na umuhimu wake kwa Utalii..........hao madiwani wakijipanga vizuri......makampuni kibao yatakuwa tayari kufadili juhudi hizo....trust me....
 
hizo fukwe walizopiga marufuku ni public kweli au tuliassume kuwa ni public?


Sheria ya ardhi hiko wazi kuhusu public place zikiwemo fukwe.

Kuhusu gharama za usafishaji, madiwani ni kuwa creative. unaweza kutengeneza indrect tax mechanism mfano mzuri ni kama watu wa New York na safari za feri kwenda StatenIsland ni bure lakini mapato yanapatikana indrectly kupitia tiketi za subway and express toll fee.

It takes a creativy to improve jiji letu and we can make Dar na ikagh'ara ila hii itategemeana na political will iliyopo.
 
Kuna bandiko kuhusu uwezo wa madiwani na kazi zao hapa JF katika ukumbi na wabari na hoja...

Aidha kwa Zanzibar fukwe nyingi sasa zimebadilishwa matumizi yake na kuwa kero kubwa kwa wananchi. Zanzibar ambayo ni maarufu kwa mambo mengi ya michezo ilijikuta ikikosa mashindano ya Ngalawa baada ya fukwe iliyokuwa ikitumika kwa shughuli kupewa Ubalozi wa Oman. Angalia mwenyewe hapa
 
Nadhani wanaolengwa ni maharusi wanaopenda kupiga picha beach! Hasa pale Aga Khan hospital. Tatizo maji ya eneo lile yamejaa kinyesi na maharusi wanapenda kuingia humo na kubebana!
 
Nadhani wanaolengwa ni maharusi wanaopenda kupiga picha beach! Hasa pale Aga Khan hospital. Tatizo maji ya eneo lile yamejaa kinyesi na maharusi wanapenda kuingia humo na kubebana!

Sasa kama wanafanya hivyo kwa hiari yao wengine tatizo lao nini? Kama wanaharusi hao wanapenda harufu ya kinyesi, pouwa tu, kama wanapenda mandhari ya maji yalojaa kinyesi, hiyo mimi na Cupcake haituhusu.

Mimi na Cupcake wangu (tukimaliza kufunga pingu za maisha) tutaenda South Beach, Miami na hakuna mizengwe wala nini huko.
 
Sasa kama wanafanya hivyo kwa hiari yao wengine tatizo lao nini? Kama wanaharusi hao wanapenda harufu ya kinyesi, pouwa tu, kama wanapenda mandhari ya maji yalojaa kinyesi, hiyo mimi na Cupcake haituhusu.

Mimi na Cupcake wangu (tukimaliza kufunga pingu za maisha) tutaenda South Beach, Miami na hakuna mizengwe wala nini huko.

Tatizo ni kuwa wanaweza kupata magonjwa yanayotokana na kuchezea kinyesi. Lakini tatizo kubwa linalowagusa wengi ni kuwa wana-clog barabara zote. Jumamosi jioni ni balaa kupitia njia hizo. Huu ni usumbufu kwa watumiaji wengine.
 
Tatizo ni kuwa wanaweza kupata magonjwa yanayotokana na kuchezea kinyesi. Lakini tatizo kubwa linalowagusa wengi ni kuwa wana-clog barabara zote. Jumamosi jioni ni balaa kupitia njia hizo. Huu ni usumbufu kwa watumiaji wengine.

Heheheheheeee...watu wazima kuchezea kinyesi....mweee...sina zaidi la kusema
 
Back
Top Bottom