Kama COCO BEACH (ambayo ilikuwa kimbilio la walalahoi kujidai na kupumzika week end na siku za sikukuu) kweli imeuzwa basi sina la kusema ila nawaombea maisha mafupi sana hapa duniani na marefu huko motoni makuwadi wote wa soko huria.
haya mambo saa nyingine inapendeza kutoyajua, that way utaishi kwa amani kabisa. Kila rasilimali tumeibiwa sasa hata kupunga upepo wa Mungu napo tunanyimwa! mh, labda ndo sikio la kufa..inaweza kuwa ndo kifo cha CCM kilichotabiriwa...yetu macho
Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa na laana kubwa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.
Akihojiwa na Radio One jana asubuhi, Kapteni Chiligati amesema sheria inaruhusu kukodishwa kwa ufukwe kwa muda usiozidi miaka mitano.
Hata hivyo, akasema sheria hiyo inapiga marufuku uuzwaji wa ufukwe kwenda mtu yeyote.
``Haya ni maeneo ambayo yapo chini ya Serikali za mitaa... lakini sheria inaruhusu kukodishwa kwa miaka isiyozidi mitano kwa ajili ya kuendeleza na kutunza maeneo hayo,`` akasema Kapten Chiligati.
Akasema maeneo hayo ni mali ya umma ambayo yametengwa kwa ajili ya starehe na burudani na kwamba ni mita 60 kutoka majini kwenda nchi kavu.
Kuhusu sakata hilo, Kapteni Chiligati akasema bado taarifa kuhusiana na jambo hilo bado hazijamfikia.
Eneo linalodaiwa kukodishwa lina jumla ya hekta 21.6 na linaanzia maeneo ya Toure Drive na kuishia Bwalo la Maofisa wa Polisi.
Hali hiyo imefanya baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Kinondoni kudai kuwa wamerubuniwa na kutia saini baadhi ya mikataba ambayo imeandaliwa na kupitishwa na watendaji waandamizi na matokeo yake ni kuitia hasara manispaa yao na pia kubariki ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi .
Kutokana na suala hilo, watendaji wa manispaa hiyo wamegawanyika huku baadhi wakiwa matatani kutokana na kutetea uuzwaji wake na huku wengine wakiupinga.
Hata hivyo, uongozi wa manispaa hiyo umekaririwa ukidai kuwa ufukwe wa Coco umekodishwa na si kuuzwa
Kapten Chiligati asema kuikodisha `Coco Beach` kwa miaka 37 ni kosa
2008-05-24 15:34:10
Na Sharon Sauwa, Mikocheni
Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa na laana kubwa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.
Akihojiwa na Radio One jana asubuhi, Kapteni Chiligati amesema sheria inaruhusu kukodishwa kwa ufukwe kwa muda usiozidi miaka mitano.
Hata hivyo, akasema sheria hiyo inapiga marufuku uuzwaji wa ufukwe kwenda mtu yeyote.
``Haya ni maeneo ambayo yapo chini ya Serikali za mitaa... lakini sheria inaruhusu kukodishwa kwa miaka isiyozidi mitano kwa ajili ya kuendeleza na kutunza maeneo hayo,`` akasema Kapten Chiligati.
Akasema maeneo hayo ni mali ya umma ambayo yametengwa kwa ajili ya starehe na burudani na kwamba ni mita 60 kutoka majini kwenda nchi kavu.
Kuhusu sakata hilo, Kapteni Chiligati akasema bado taarifa kuhusiana na jambo hilo bado hazijamfikia.
Eneo linalodaiwa kukodishwa lina jumla ya hekta 21.6 na linaanzia maeneo ya Toure Drive na kuishia Bwalo la Maofisa wa Polisi.
Hali hiyo imefanya baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Kinondoni kudai kuwa wamerubuniwa na kutia saini baadhi ya mikataba ambayo imeandaliwa na kupitishwa na watendaji waandamizi na matokeo yake ni kuitia hasara manispaa yao na pia kubariki ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi .
Kutokana na suala hilo, watendaji wa manispaa hiyo wamegawanyika huku baadhi wakiwa matatani kutokana na kutetea uuzwaji wake na huku wengine wakiupinga.
Hata hivyo, uongozi wa manispaa hiyo umekaririwa ukidai kuwa ufukwe wa Coco umekodishwa na si kuuzwa
Nina hakika ukimuuliza Chiligati kwa nini ufukwe huo ukodishwe (hata hiyo miaka mitano) badala ya kuendelezwa kama eneo la wazi, atakwambia "$erikali haina pesa za kuendeleza na wanajaribu kuliokoa kufuatia uchafuzi wa biashara ndogondogo"!Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa na laana kubwa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.