Fukwe (Beach) za Tanzania na hatma yake

Kama COCO BEACH (ambayo ilikuwa kimbilio la walalahoi kujidai na kupumzika week end na siku za sikukuu) kweli imeuzwa basi sina la kusema ila nawaombea maisha mafupi sana hapa duniani na marefu huko motoni makuwadi wote wa soko huria.
 
Kama COCO BEACH (ambayo ilikuwa kimbilio la walalahoi kujidai na kupumzika week end na siku za sikukuu) kweli imeuzwa basi sina la kusema ila nawaombea maisha mafupi sana hapa duniani na marefu huko motoni makuwadi wote wa soko huria.

Hawa hata usipowaombea tayari mungu amekwishawawekea pa kufikia kwa mujibu wa matendo yao dhidi ya wananchi wenziwao!
 
HUYO MWARABU AACH KUINVEST HUKO JUMEIRA BEACH AJE KUINVEST BONGO?

sounds fishy kwangu
 
haya mambo saa nyingine inapendeza kutoyajua, that way utaishi kwa amani kabisa. Kila rasilimali tumeibiwa sasa hata kupunga upepo wa Mungu napo tunanyimwa! mh, labda ndo sikio la kufa..inaweza kuwa ndo kifo cha CCM kilichotabiriwa...yetu macho

EA's Last Tribal Bushmen in Stiff Survival Battle in Mbulu Valley

Correspondent: Valentine Marc Nkwame

This Day 4/27/07

The Hadzabe clan of hunter gatherers, who are the last of a rapidly shrinking population of 10,000 tribal bushmen in Tanzania, are battling for their very survival against a foreign investor companythey claim is attempting to grab their traditional land.

It is alleged that the Tanzania United Arab Emirates Safaris Limited company, which has roots in the Middle East, intends to take over the entire 3,975 square kilometers of the Yaeda valley and the stretching Eyasi escarpments in the eastern division of Mbulu District, Manyara Region.

The bushmen claim that as a result of the situation, threats, intimidation, fear and chaos have now become the order of the day in their once calm 'Garden of Eden.'

Reports have it that the Yaeda valley, which since human evolution has been home to East Africa's only remaining tribe of pure bushmen - the Hadzabe - has now become a literal battlefield between the native residents and various Mbulu District officials who appear intent on ensuring that the 'investor' firm moves in.

It is stated that the valley population, numbering more than 10,000, is now living in abject fear in the wake of an ultimatum of sorts issued by the district officials, that they either accept the investor's various demands or be forcefully evicted from the valley for good.

Also residing in the same valley are members of the Datoga and Barbaig tribes.

According to Zephania Athuman of the Mongo wa Mono Village committee in the valley, neither he nor other members of the committee were ever involved in the process leading up to the leasing out of the land to the Arab company.

Speaking to this reporter, Zephania wondered aloud how a 'foreigner' could infiltrate the area to such an extent without the natives being aware.

And an elderly member of the Hadzabe tribe, Mahiya Matulu, speaking through an interpreter, displayed scars of wounds from a beating he claimed to have received at the hands of unspecified people, apparently for speaking out too vocally against the deal.

The said investor company, which has said it plans to introduce commercial and sports hunting activities in the valley, moved into the area last year and has already set up a temporary camp, although it is yet to start its proposed activities.

The Mongo wa Mono Village chairman, Reuben Mathayo, said when contacted for comment that agents representing the company have promised to deliver a number a number of development projects in the area, as part of the investment package.

He, however, refuted claims that the deal agreement has already been signed.

"We cannot sign while all this controversy still exists, and in fact even the investor himself has not yet set foot here. But we belive the natives' negative attitude is being incited by some people who do not want this place to be developed," Mathayo said, without offering any names.

It is understood that the district wildlife officer, Allan Shani, has recently presided over several meetings to address the issue, and officials say all these meetings resulted in unanimous agreement to accept the Arab investor company in the valley..

But contradictory findings by this reporter suggest that many of the Yaeda Chini valley residents whose names appeared in the attendance lists of those meetings, have been dead for many years.

According to Dumanga Ward resident Yohana Gitang, many of the native widows even staged protest marches on learning that the names of their dead husbands had been included in the attendance lists.

They include Ms Amina Zungu Gitandu and Ms Kirstina Paulo, who supported Gitang's claims and accused Shani and his game scouts of trying to bully the natives into accepting the investor.

Shani is further alleged to have been gifted (bribed) a new car by the investor company, but he himself denied this when contacted, saying he acquired his brand new, white-coloured Toyota Mark II saloon vehicle with registration number T172 ABE through his 'own efforts."

Also denying charges of receiving 3m/ bribes over the issue were the Mongo wa Mono Village chairman, Mathayo, and Yaeda Chini Ward councilor Bryson Kisaki.

The state-run Commision for Human Rights and Good Governance is also reported to have joined the band, sending a six-strong delegation led by commissioner Jecha Salim Jecha to try and persuade the indigenous valley residents to accept the Arabian-based Tanzania UAE Safaris Ltd company into the vast valley as a move towards 'speeding up their development.'

But jecha and his team are said to have got more than they bargained for, when their public rally address to a crowd of more than 200 people was interrupted by frenzied and animated mass protests and threats aimed at the visiting delegation.

The delegation, comprising Jecha, two commission investigators, a hired local journalist and the district wildlife officer escaped in a convoy of three vehicles, with some angry youths hurling stones in their direction as they disappeared up the trail.

A spokesperson for the Hadzabe community in the valley, Naftal Kitandu, told this reporter that they now intend to further pursue their case of injustice with the courts in Arusha, with main respondents being the Mbulu District Council and the district wildlife department led by Shani.
 
Penye uonevu hapana amani. Uongozi wa serikali yetu ni mhimu kabisa watambue kuwa wajibu wao ni kuhakikisha kuwa haki inatawala katika kila jambo bila ya kujali ngazi au tabaka la wahusika.

Dalili mbaya zinazidi kujionyesha miongoni mwa wananchi, hasa hizi za kuonewa kwa maksudi kwa visingizio visivyokuwa na maslahi kwao.

Yumkini, ukimuuliza Mhadzabe ambaye uhai wake unaelekea kufikia kikomo, atakwambia kuwa nchi yetu uhuru bado.

Na unapoanza kusikia watu wanasema 'kushika mapanga,' pengine unaweza kuwapuuza kuwa ni wapayukaji; lakini kiongozi mwenye busara atajiuliza mara mbili mbili sababu zinazosababisha mawazo ya namna hii, na kiongozi huyo hawezi kusubiri kutumia mabavu kuzima machafuko.
 
Heshima mbele Wakuu.... Leo nimeona hii kwenye Alasiri nikapata mshituko kwa kweli.... Sikutegemea kuwa rushwa imetutafuna mpaka hatuna hata pa kujisitiri, hebu angalia hawa jamaa wa Manispaa ya Kinondoni wamekodisha ule ufukwe mzimaa kwa mtu/kampuni moja kwa jumla ya miaka 37??!?! Hawa wakuu kweli sasa wamekuwa zaidi ya vilafi manake ukumbuke hawahawa (wilaya hii hii) ndio walitoa kibali cha kujenga yale maghorofa marefu kule Masaki (Toure Drive) kisha yakabomolewa na leo tunaambiwa kesi ipo mahakamani kilichobaki pale ni magofu!! Hivi Tanzania inaenda wapi wajamani!?!!?!

Kapten Chiligati asema kuikodisha `Coco Beach` kwa miaka 37 ni kosa
2008-05-24 15:34:10
Na Sharon Sauwa, Mikocheni


Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.

Akihojiwa na Radio One jana asubuhi, Kapteni Chiligati amesema sheria inaruhusu kukodishwa kwa ufukwe kwa muda usiozidi miaka mitano.

Hata hivyo, akasema sheria hiyo inapiga marufuku uuzwaji wa ufukwe kwenda mtu yeyote.

``Haya ni maeneo ambayo yapo chini ya Serikali za mitaa... lakini sheria inaruhusu kukodishwa kwa miaka isiyozidi mitano kwa ajili ya kuendeleza na kutunza maeneo hayo,`` akasema Kapten Chiligati.

Akasema maeneo hayo ni mali ya umma ambayo yametengwa kwa ajili ya starehe na burudani na kwamba ni mita 60 kutoka majini kwenda nchi kavu.

Kuhusu sakata hilo, Kapteni Chiligati akasema bado taarifa kuhusiana na jambo hilo bado hazijamfikia.

Eneo linalodaiwa kukodishwa lina jumla ya hekta 21.6 na linaanzia maeneo ya Toure Drive na kuishia Bwalo la Maofisa wa Polisi.

Hali hiyo imefanya baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Kinondoni kudai kuwa wamerubuniwa na kutia saini baadhi ya mikataba ambayo imeandaliwa na kupitishwa na watendaji waandamizi na matokeo yake ni kuitia hasara manispaa yao na pia kubariki ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi .

Kutokana na suala hilo, watendaji wa manispaa hiyo wamegawanyika huku baadhi wakiwa matatani kutokana na kutetea uuzwaji wake na huku wengine wakiupinga.

Hata hivyo, uongozi wa manispaa hiyo umekaririwa ukidai kuwa ufukwe wa Coco umekodishwa na si kuuzwa.

SOURCE: Alasiri
24/05/2008 (www.ippmedia.com)

My take:
1. Waziri anasema taarifa hazijamfikia, jamani sasa ameshaona ata act au atangoja taarifa zimfikie?
2. Huyo aliyefanya kosa amechukuliwa hatua gani?
3. Madiwani wanasema wamerubuniwa kutia saini mikataba bomu, ha ha haaaaaa!! Shame on them, ina maana wao wanakutana kutia saini mikataba bila kuisoma?? Hawana common sense ya kujua jema na baya? Au kurubuniwa ni "In Kind?"
4. Watendaji eti wamegawanyika, then what?? Wanaweza wakabaki na mgawanyiko wao lakini sisi tunataka kujua ukweli na uamuzi kuwa reversed!
5. Eti eneo limekodishwa halijauzwa, hawa wakuu wanajua hata ukinunua shamba Kimanzinchana Serikali ikikupa Title deep ni ya muda gani?? 33 years, wao wamempa Mkuu 37 years.... Hawa watendaji wanatakiwa wapigwe bakora kabisa.... kutetea such nonsense ni upuuzi mkubwa sana!!!
 
Kapten Chiligati asema kuikodisha `Coco Beach` kwa miaka 37 ni kosa

2008-05-24 15:34:10
Na Sharon Sauwa, Mikocheni

Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa na laana kubwa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.

Akihojiwa na Radio One jana asubuhi, Kapteni Chiligati amesema sheria inaruhusu kukodishwa kwa ufukwe kwa muda usiozidi miaka mitano.

Hata hivyo, akasema sheria hiyo inapiga marufuku uuzwaji wa ufukwe kwenda mtu yeyote.

``Haya ni maeneo ambayo yapo chini ya Serikali za mitaa... lakini sheria inaruhusu kukodishwa kwa miaka isiyozidi mitano kwa ajili ya kuendeleza na kutunza maeneo hayo,`` akasema Kapten Chiligati.

Akasema maeneo hayo ni mali ya umma ambayo yametengwa kwa ajili ya starehe na burudani na kwamba ni mita 60 kutoka majini kwenda nchi kavu.

Kuhusu sakata hilo, Kapteni Chiligati akasema bado taarifa kuhusiana na jambo hilo bado hazijamfikia.

Eneo linalodaiwa kukodishwa lina jumla ya hekta 21.6 na linaanzia maeneo ya Toure Drive na kuishia Bwalo la Maofisa wa Polisi.

Hali hiyo imefanya baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Kinondoni kudai kuwa wamerubuniwa na kutia saini baadhi ya mikataba ambayo imeandaliwa na kupitishwa na watendaji waandamizi na matokeo yake ni kuitia hasara manispaa yao na pia kubariki ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi .

Kutokana na suala hilo, watendaji wa manispaa hiyo wamegawanyika huku baadhi wakiwa matatani kutokana na kutetea uuzwaji wake na huku wengine wakiupinga.

Hata hivyo, uongozi wa manispaa hiyo umekaririwa ukidai kuwa ufukwe wa Coco umekodishwa na si kuuzwa
 
Mwanahalisi Tafadhali, kichwa chako cha habari kinatisha.
kusema kuwa ni "Laana kwa watanzania". duh ni maneno makali mno na yanatisha ndugu yangu, kwani laana si kitu cha mchezo.

nikirudi katika mada:
nikikumbuka jinsi nilivyokuwa nikiburudika katika ufukwe wa coco beach hususan kila weekend, roho inaniuma iwapo zitachukuliwa hatua zozote za kuwafanya wananchi wasiendelee kuburudika bure katika ufukwe ule. kipindi cha sikukuu kama eid na christmass coco beach ni kimbilio la wananchi kupata burudani ya upepo mwanana na pia kuogelea.
kumkodisha mtu ufukwe wa Coco beach ni dhahiri kumpa mtu tiketi ya kujichukulia pesa za bure kwa wale watakao taka kwenda pale kuburudika. kama ni maji ya bahari ni maji ya asili, upepo ni upepo wa asili, mchanga ni mchanga wa asili, sasa iweje mtu apewe haki ya kuvuna pesa za bure kwa kutumia vitu vya asili?. kama ni kujenga mahoteli au huduma yeyote atakayoingiza juhudi na maarifa basi hivyo ndo vinatakiwa kutozwa pesa lakini si ufukwe na maji yake.

mimi ninasema hivi !.iwapo ukodishwaji wa huo ufukwe utasababisha wananchi wasiutumie ufukwe free of charge, basi huyo aliyekodisha ufukwe na mamlaka iliyoukodisha huo ufukwe wakae sawa muda muafaka ukifika tutakwenda mahakamani kudai ufukwe wetu. haiwezekani kupelekwa pelekwa namna hii, hapa niko niko serious!.
Time will tell
 
Ukodishaji wa Coco Beach ni kipimo cha juu cha UFISADI katika nchi hii... Kwanza mbali ya kukiuka sheria, MAnispaa ilifuta tenda ya ukodishaji wa Coco Beach hadi watakapotangaza baada ya THISDAY kuandika hiyo habari na watu wa USalama wa Taifa kuingilia kati wakisema ni hatari kwa usalama wa taifa kwa kuwa hadi eneo jurani na makazi ya Waziri Mkuu lingehusika, lakini wakati watu wanasubiri tenda mpya itangazwe, Manispaa ya Kinondoni ikaamua kuuza eneo hilo, tena ndani ya eneo kuna mtu mwingine anayeendesha biashara zake kwa mikataba na Manispaa hiyo hiyo lakini wametumia kila aina ya hila na ulaghai hata kutumia Mahakama kutaka kuuza eneo hilo. Inaonekana kuna nguvu kubwa sana katika kuuza eneo hilo.

Hoja ya pili hapa ni kwamba mbona THISDAY wameacha kuandika hiyo story? KULIKONI? nadhani hapo napo tunahitaji kupaangalia kwa makini kwani nako upo uwezekano kuna MKONO WA MTU... tusaidiane MAFISADI HAWALALI
 
Hiii ndio BONGO-LAND, kila mtu anakula katika meza yake na mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake...... Lakini ikifika "HIYO SIKU" patakua padogo
 
Kapten Chiligati asema kuikodisha `Coco Beach` kwa miaka 37 ni kosa

2008-05-24 15:34:10
Na Sharon Sauwa, Mikocheni


Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa na laana kubwa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.

Akihojiwa na Radio One jana asubuhi, Kapteni Chiligati amesema sheria inaruhusu kukodishwa kwa ufukwe kwa muda usiozidi miaka mitano.

Hata hivyo, akasema sheria hiyo inapiga marufuku uuzwaji wa ufukwe kwenda mtu yeyote.

``Haya ni maeneo ambayo yapo chini ya Serikali za mitaa... lakini sheria inaruhusu kukodishwa kwa miaka isiyozidi mitano kwa ajili ya kuendeleza na kutunza maeneo hayo,`` akasema Kapten Chiligati.

Akasema maeneo hayo ni mali ya umma ambayo yametengwa kwa ajili ya starehe na burudani na kwamba ni mita 60 kutoka majini kwenda nchi kavu.

Kuhusu sakata hilo, Kapteni Chiligati akasema bado taarifa kuhusiana na jambo hilo bado hazijamfikia.

Eneo linalodaiwa kukodishwa lina jumla ya hekta 21.6 na linaanzia maeneo ya Toure Drive na kuishia Bwalo la Maofisa wa Polisi.

Hali hiyo imefanya baadhi ya madiwani wa Manispaa ya Kinondoni kudai kuwa wamerubuniwa na kutia saini baadhi ya mikataba ambayo imeandaliwa na kupitishwa na watendaji waandamizi na matokeo yake ni kuitia hasara manispaa yao na pia kubariki ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi .

Kutokana na suala hilo, watendaji wa manispaa hiyo wamegawanyika huku baadhi wakiwa matatani kutokana na kutetea uuzwaji wake na huku wengine wakiupinga.

Hata hivyo, uongozi wa manispaa hiyo umekaririwa ukidai kuwa ufukwe wa Coco umekodishwa na si kuuzwa



Hata kama ni kukodishwa ndiyo miaka 37 ama umekodishwa kwa muda gani si watueleze ?
 
...huwezi jua, labda kakodishwa 'mzalendo' apande maua na kuhifadhi mazingira... kinyume na hapo ni kuanza kuwagawa watanzania kwa matabaka iwapo ndugu zangu wa 'uswazi' watashindwa kwenda kuburudika beach siku za sikukuu na wikiendi!
 
Hizi ndio laana zenyewe....jamani...nakumbuka enzi hizo za kwenda kula upepo hata kama huna kitu.
Unatembea toka kinondoni shamba mpaka coco beach....kweli tanzania ndio bongo land...kumbe watu hizi wana uzoefu wa kuuza sehemu za nchi...ndio maana wakataka na nyamagana iwe hivyo?
Ohh gosh...nilifikiri kitu kingeni...kweli (jamiiforum be part of it ni nguli wa habari)
 
iwapo baba wa familia anafanya laana za kuuza uza vitu vya ndani ya nyumba, usitegemee mtoto kuwa na tahadhari zaidi ya baba yake.

hapa nchi haikai sawa mpaka viongozi watakapojirekebisha......
 
Sasa yeye huyo Chiligati akiwa kama Waziri wa ardhi badala ya kuendelea kulalama atumie wadhifa wake kutengua ukodishaji huo haraka sana.
 
Tehe tehe tehe tehe teheee!! mnashangaaa!!!! mtashangaa sana mwaka huu. Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi mpya hamkujua maana yake.. Kila mtu achukue chake mapema bwana. kwani nani wa kuwauliza?
 
Wacheni wacheni wacheni ,hivi hapo kama angekodishwa mzungu mngepiga makelele,mimi nimefurahi sana kuona aliekodi ni mzalendo ingawa sijafahamu nia na madhumuni haswa ya maradi aliokusudia ,inawezekana mtu akajenga na kuinvest nyumba na kukodisha au akaweka sehemu ya Park na kuweza kujipatia fedha ,hivi ndivyo wananchi wanavyotakiwa wawekeze , mtu anaweza sehemu hiyo akaizingira na kuweka mambo ya kufurahisha jamii at the week end ndugu na jamaa wanajimwaga huko,just akaweka kiingilio labda shilingi mia tano au mia tatu kiasi hata mlala hoi anaweza kwenda kujiburudisha ,hayo ndio mambu yalioko ulaya.
na zaidi kuwa jamaa hakununua isipokuwa amekodi sasa tatizo lipo wapi Karume na Salmini wamekodisha visiwa kwa muda wa miaka 99 kuna nchi unakodi nyumba kwa miaka mia na sio unakodi unanunu nyumba kwa muda wa miaka mia ,yaani mjenzi mmiliki na hata aliekodi watakuwa hawapo tena na hiyo ndio biashala.
hapo kuna watu wamekosa mlo tu hakuna cha Chiligati wala wala Chiligate wanataka wamegewe tu ,na jamaa akimuwahi huyo wa waziri kwa donge nono basi mtaona ila hamtasikia kitu.
 
Wakati Manispaa ya Kinondoni ikiwa inadaiwa kukodisha ufukwe wa Coco almaarufu kama `Coco Beach` kwa mfanyabiashara mmoja Jijini atakayeutumia kwa miaka 37, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kapteni (Mstaafu) John Chiligati, amesema kisheria, ni kosa na laana kubwa kumkodishoa mtu eneo kwa muda unaozidi miaka mitano.
Nina hakika ukimuuliza Chiligati kwa nini ufukwe huo ukodishwe (hata hiyo miaka mitano) badala ya kuendelezwa kama eneo la wazi, atakwambia "$erikali haina pesa za kuendeleza na wanajaribu kuliokoa kufuatia uchafuzi wa biashara ndogondogo"!

DAAAMN! Ni $erikali hiyo hiyo ambayo kila kukicha inang'ang'ania mradi wa ID-card wa bil. 183 (ambazo nina hakika mpaka umalizike tutaambiwa gharama halisi zimefika bil.500)!!

Hawa watu wanatupeleka motoni kabla hatujafa; hili ni jukumu la $erikali yoyote duniani kuendeleza maeneo ya wazi walau kuonyesha matumizi ya kodi zao. Wanakwepa majukumu na ndio maana kila kukicha ni skendo za kifisadi maana pesa hazitumiki kwa maendeleo ya wananchi bali miradi ambayo haina msaada wowote kupunguza makali ya maisha ya mwnanchi.

Watu kama hawa kamwe hawawezi kukubali kuondoka madarakani maana kila kukicha hakuna wanalofanya zaidi ya kufikiria wizi ambao mwishowe unawaweka pabaya wao na familia zao, ambapo dola inabakia kuwa wokovu pekee kwao. Tunapanda mbegu mbaya ambayo hatutaweza kuing'oa kwa vizazi na vizazi; mbegu ya kutowajibika ilhali tukitamani familia binafsi zineemeke.

Sehemu nyingine duniani Halmashauri ndio kitovu cha maendeleo ya familia, na zinajishughulisha moja kwa moja kuhakikisha makali ya maisha kwa wanafamilia yanapungua. Leo, halmashauri zetu ndio za kwanza kuuza raslimali ambazo zingeweza kupunguza makali kwa mwanafamilia. Tunakwenda wapi??
 
Back
Top Bottom