Ex-GF wangu kaolewa jana

Samahani mkuu, nimeeleza tu hisia zangu kwa nilichoona alhamisi 9 Dec 2010
My bradah just mind your business and stop day time dreams, aliye uchi haoni aibu wewe unaechungulia ndio unauna aibu ebooo, imetokaaa ikurudi pancha!
 
kilichobaki msubirie apate kaujauzito halaf azae wewe ukapeleke na kamchango ka nepi za mtoto. halaf uje uanzishe sredi nyengine kuhusu rangi ya mtoto.
 
Naona watu wameninangaaa! Poa washkaji. Lakini namshukuru Preta kanielewa. Badae wakuu.
 
Mi nimesema tuliachana, hayo ya kupigwa chini umeyaleta wewe. Bado nasisitiza kilichotokea jana ni a total mismatch, to the disadvantage of the dear sister. Kwa mtazamo wangu, she deserves better, siyo type ile kabisa. Nahisi kakosa uvumilivu tu.

To the disadvantage of the dear sister? Yaani ghafla kageuka kuwa dada tena?
Jamani watu hamweshi kushangaza.
 
Naona watu wameninangaaa! Poa washkaji. Lakini namshukuru Preta kanielewa. Badae wakuu.

Pole sana Mkuu, Kinachokusumbua ni Ka Wivu fulani kalikokupata Ghafla, kwa kawaida sisi binadamu(hasa sisi wanaume) huwa tunakuwa na wivu wetu wa Kiume kwamba hata kama Mshichana mliachana naye ungetamani kwamba aendelee kuishi maisha ya Utawa ha ha ha kwamba asitokee jamaa mwingine akawa anamega. Na wewe inawezekana ulidhani hivyo ( Sina Uhakika)

Sasa Kilichotokea jana ni kwamba Umethibitisha kwamba jamaa anakwenda Kusaula Mtoto sasa roho ikaanza kukuuma na kuanza kumvika Msela Sura na Tabia ambazo si Nzuri ili kujustify Mawivu yako kwa Sababu unazungumza as If huyo Mshikaji Ndiyo umemuona Jana

Otherwise Pole sana Mkuu hata mimi Ningeumia tu lakini ni kwa Muda
 
Tuliachanaga miaka mingi sana kwa hiyo nilijua sina hisia yoyote naye tena. Alivyonijulisha anaolewa anaomba mchango wa send-off nikamchangia kama kawaida na send-off nimeshiriki sherehe juzi 9 December. Sasa sijui ni kwanini nilipomwona yule mchumba wake alhamisi ile, nikaanza kuhisi kwenye nafsi yangu kwamba yule jamaa hamfai, yaani kwa ninavyomfahamu yule dada ile siyo type yake kabisa! Dada kakosea kuchagua bana, no! Siwezi kueleza hii hali, naamini siyo wivu but no, siyo yule kabisa bana!

Mtu B; Uliona nini kilichokufanya udhani yule jamaa hamfai? Kwani wewe una nini kudhani wewe tu ndo unamfaa? - Wivu. Unadhani walikutana siku hiyo?. Kama ulikuwa hujui; Dem ndo alikuwacha, na jamaa ndo alisababisha. Imekula kwako.
 
Sio demu wako tena ni mke wa mtu!!Unajishtukia wewe kama sio wivu!Kama kweli huyo mshkaji labda sio mzuri kama wewe au hana pesa kama wewe,kinakuuma kwamba iwe vipi achaguliwe yeye!!Unachojishtukia ni kwamba mshkaji ana kitu ambacho wewe huna...pole labda anampa gemu ya ukweli na wewe ulikua unapapasa papasa tu!
 
Habri yako bwana Kimbweka. Tuashumu huyo,kwa avatar yako ndo anaolewa bila ridhaa yako baada ya hapo....

Khabri ni swaafi nacheki tu kilimanjaro stars hapa
Hiyo haitawezekana
Maana hatujaachana mkuu
 
Tuliachanaga miaka mingi sana kwa hiyo nilijua sina hisia yoyote naye tena. Alivyonijulisha anaolewa anaomba mchango wa send-off nikamchangia kama kawaida na send-off nimeshiriki sherehe juzi 9 December. Sasa sijui ni kwanini nilipomwona yule mchumba wake alhamisi ile, nikaanza kuhisi kwenye nafsi yangu kwamba yule jamaa hamfai, yaani kwa ninavyomfahamu yule dada ile siyo type yake kabisa! Dada kakosea kuchagua bana, no! Siwezi kueleza hii hali, naamini siyo wivu but no, siyo yule kabisa bana!

you cant tell about a person after only a day-observation
unless macho yako yana 3 -dimension...
mwache dada wa watu aolewe neye, yeye anamjua kitambo na ameridhia nae..:teeth:
 
Habari ndungu huwa sitembelei anga hizi lakini naona hapa imebidi....... Kama ameolewa hatakuwaje demu wako tena..... jamaa hamfai???? kumbuka..... True love is not finding a perfect man, but loving an imperfect man perfectly...

punguza kujikweza dogo. Eti huwa hutembei anga hizi
 
punguza kujikweza dogo. Eti huwa hutembei anga hizi

Mimi sijikwezi ndugu yangu...wewe ndo unajishusha.. kwani anga hizi zina matatizo gani kaka? mbona ziko poa tu? ni kwamba imetokea huwa sizitembelei sio kwamba ni mbaya mara nyingi huwa nipo kule kwenye siasa... ila kila nitakapohitaji ushauri kwenye hii fani basi takuja..
 
Habari ndungu huwa sitembelei anga hizi lakini naona hapa imebidi....... Kama ameolewa hatakuwaje demu wako tena..... jamaa hamfai???? kumbuka..... True love is not finding a perfect man, but loving an imperfect man perfectly...

Umesema kweli kabisa.
Mimatch ni ile iliogoma kati yako na yeye.
Kama msichana ameshaumwa na nyoka kama wewe usiechagua maneno, dharau kwa watu wengine hadi usiowajua, nashukukuru na kumpongeza huyo dada kwa kukugundua mapema na kumalizana nawe.
Kiukweli hakuna kinachokera kama mwanaume anaetazama wenzake kwa dharau, !!!
Pole kaka,
Kua na wewe ujifunze.

Kwanza kabla sijamaliza urugaruga ndio nini?
Suti haikumpendeza??? Wakati wewe unajua kuvaa hadi watu wanakusifia????

Nakusikitikia kwani nahisi, kwa jicho lako hilo, utapata mke mzuri sana wa kwenda nae pati, ila hapo home patakuwa mchanganyiko wa kila kitu, kila tamaduni iliowahi kuwa fashion,

Tafuta ground zero yako ndo uanzie hapo, kwa sasa nado unaelea katika wingu la ujana/adolesent
 
...... wake alhamisi ile, nikaanza kuhisi kwenye nafsi yangu kwamba yule jamaa hamfai, yaani kwa ninavyomfahamu yule dada ile siyo type yake kabisa! Dada kakosea kuchagua bana, no! Siwezi kueleza hii hali, naamini siyo wivu but no, siyo yule kabisa bana!

Mhmm...hapa kuna tatizo, tena sio dogo!

Logically unachosema huyo jamaa pengine anafanana na wewe....kwa sababu kama wewe hukumfaa huyo dada na makaachana na huyu nae unahisi hamfai (kama ambavyo wewe hukumfaa)....so the two of you are alike (warugaruga!)?

Hebu fafanua vizuri tukuelewe, inaelekea kuna vitu vingi hujavisema kwenye hii post yako.
 
Ebwana we, huyo demu wako ni Mtu wa Mbeya na kaolewa na mhaya nini? maana naanza kuhisi ni nani!. Kwanza sio demu wake ni aliye kuwa demu wako . Unadhani kwnaini huyo hamfai wakati wewe ulimwacha? na pia ungefahamu wanawake wanapenda viitu exciting sasa labda jamaa ndio type yake wewe hukuwa type yake ,usikonde utapata tuu wa kwako .
 
Thread hii inanikumbusha shairi nililosoma nikiwa darasa la tatu mwaka 1983
na shairi lenyewe sijalisahau mpaka leo hii linasomeka hivi :-

Hadithi inayokuja ni ya sungura sikia,
Hadithi uliyongoja leo ninakuletea,
Alitoka siku moja njaa aliposikia,
njaa aliposikia,sungura nakuambia.

Siku ile akaenda porini kutembelea,
Akayaona matunda mtini yameenea,
sungura akayapenda mtini akasogea,
Mtini akasogea,sungura nakuambia.

Sungura karukaruka,
Lakini hakufikia,matunda hakuyashika,
Mikononi hakutia hakika alisumbuka nguvuze zikapungua ,
nguvuze zikapungua,sungura nakuambia.

SIZITAKI MBICHI HIZI,
Sungura akagumia naona nafanyakazi bila faida kujua,
yakamtoka machozi matunda akalilia,
Matunda akalilia sungura nakuambia,

Sio kama hakutaka sasa nakupasulia,
Matunda liyataka ndio kisa akalia,
Tunajua hakufika alichoka kurukia,
alichoka kurukia,sungura nakuambia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom