Yaani wewe ndugu yangu mwanaukonga mwenzangu nimesoma hoja yako nilipoimaliza nikakuhurumia huenda hujui kinachoendelea duniani.
Jana Marekani imetangaza kufunga ofisi zake za balozi zipatazo 21 katika nchi za Afrika Kaskazini pamoja na Middle East kufuatia kitisho cha mashambulizi ya Al Qaeda. Sasa sijui unaizungumzia al qaeda ipi iliyodhoofika lakini hapo hapo inaweza kuwa kitisho kwa nchi kubwa super power kama marekani hadi inaamua kufunga balozi zake.
Kwahiyo ndugu yangu hoja yangu iko palepale kwamba Kikwete angekuwa muungwana sana kama angetoa ushauri ambao yeye mwenyewe ana u-practice. Wananchi wa Mtwara tu ameshindwa kuongea nao na kuwatumia batallion ya JWTZ sasa huo uungwana/huruma kwa majirani zake ameutoa wapi?
Mwita Maranya, two wrongs can not make one right!
Wakati tunakosoa kauli ya JK katika suala hili, lakini pia tusiache kukosoa kauli ya Dr. Slaa iliyopelekea kuwepo kwa thread hii. Hii ni busara itakayopelekea kuwa na chama kinachokosoana na si vinginevyo. Binafsi mimi pia nakuonea huruma mwanaukonga mwenzangu na pia najionea huruma kwa sababu najua
repercussion ya kauli ya Dr. Slaa. Bahati tu haitaonekana sana tu kwa kuwa kiwango cha watanzania kupoteza matuamaini kwa Serikali ni kikubwa sana ndiyo maana watu watapata uvumilivu kidogo, lakini kauli ya Dr. Slaa "inayumba" sana kuweza kuielewa. Tunapozungumzia siasa, ni vema tutofautishe baina ya siasa za ndani na nje. Siku zote siasa ya ndani inajengwa kwa siasa za nje kupitia "Diversionary incentives" na si kinyume chake. Na hii huenda ndicho kinachofanywa na hawa marais wawili. Nimesema hapo juu kuwa ushauri wa Kikwete kimantiki uko sawa, labda kimazingira. Hata hivyo naweza kusema pia hata kimazingira ilikuwa ni sahihi kwa sababu lengo ni kupata "Global attention" na pia haukutolewa kwa Kagame pekee, je ni nini kilichofanya Kagame ndio aonekane kama ndiyo pekee aliyepewa ushauri huu? Na je ulifatilia kikao kilichopita cha Baraza la Usalama la UN mwezi uliopita ambapo Rwanda ni mjumbe wa kudumu kwa sasa kwenye Baraza hilo na kuiona hali aliyokuwa nayo Foreign Minster wake? Nilifuatilia live mwanzo mwisho na yule mama alikuwa kama yu mgonjwa kwenye mkutano ule.
Kuhusu Marekani na balozi zake, nadhani pia huna budi kuzingatia kuwa kilichoifanya Marekani kufunga Balozi zake si Alqaeda ile ya Osama, no. Ni kutokana na
intervention yake katika vita ya Syria na Libya, machafuko yanayoendelea ktk arab countries ambazo zimetoa mwanya wa
minimal movement control kwa kutumia kigezo cha machafuko pamoja na wale mamia ya wafungwa waliotoroka ambao kutokana na mateso waliyoyapata, Marekani inaamini kuwa wale watu watalipiza kisasi kwa kufanya mashambulizi, lakini pia inaamini baada au siku chache kabla ya Mfungo wa Ramadhan, radical muslims wanakuwa na highest morality ya kufanya attack. Lakini si Alqaeda as Alqaeda kwa sababu (narudia tena kiasi fulani imedhoofika baada ya kuwa Marekani amebaini njia zake za mawasiliano kitu ambacho awali hakuwa akijua, kiasi cha kuamini AAlqaeda walikuwa na teknolojia ya juu sana ya mawasiliano). Kwa sasa, marekani inatumia neno ALqaeda kama ni justification na supports kutoka kwa wananchi wake kwa sababu ndio jina ambalo wanalielewa sana. Lakini hoja yangu katika hili nilisema kuwa Alqaeda ni mtandao si kikundi tofauti na kesi ya Rwanda. Ni kutokana na kuwa ni mtandao ndio maana hadi wanafunga hizo Balozi hawana hakika
exactly wapi hizo
attacks zinaweza fanywa. Mwita ndugu yangu, nafuatilia kwa karibu sana siasa za nje hususan Marekani.
Nimalizie maelezo haya marefu kwa mwanaukonga mwenzangu kwamba, Dr. hana budi kuwa
well informed katika anga za kimataifa kwa sababu hiyo ndiyo hali ambayo Tanzania inayo kutokana na strategic environment zinazotokana na resources zilizopo. Hakuna namna yoyote ya Tanzania kuwa "dumb" katika siasa za nje kwa sasa. Nitumie fursa hii kuiomba kurugenzi ya mambo ya nje ya Chadema kuiangalia nafasi ya Tanzania kwa sasa katika International political arena kwa umakini mkubwa kuliko ilivyokuwa one year before kwa sababu inaweza kuisumbua katika kipindi cha uchaguzi. Ni rahisi kwa UK na US kuiachilia mbali Zimbabwe, lakini si rahisi kwa Congo, Tanzania na Nigeria.