ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
Dr.Slaa anaweza kuongea hivyo
kwa sasa. Lakini hata Dr. Slaa angekuwa Rais wa nchi,maisha yake binafsi
na mipaka ya nchi yake ikitishiwa,angeanza kwanza ku deal na
wanaotishia mipaka ndipo angekuja kutatua ya ndani. Ukiwa unagombana na
mkeo/mumeo ndani,ukasikia watu wanataka kuvunja gate wavamie kwako,cha
kwanza utaenda kupambana na wanaivunja gate lako ukisha wasambaratisha
ndio utarudi ndani kupatana na mkeo/mumeo.
Kinadharia ushauri wa Kikwete unaweza kuonekana kama mzuri lakini haukuwa na action plan au road map ya utekelezaji kushauri bila action plan ni sawa na kuropoka hasa unapomshauri mkuu wa nchi nyingine.
Kama Kikwete ataanzisha vita na Kagame binafsi nitakuwa wa mwisho kwenda vitani, kwa sababu naamini Kikwete hakuwa sahihi kuwaambia Rwanda wakutane na waasi alichotakiwa ni ku-mediate mkutano kwa kuwakutanisha mahasimu na sio kuwaambia wakutane, kwanza wakutane wapi na nani awe mlalamikaji na mlalamikiwa.
Huku ndio kunaitwa kupamba maandishi tu, kama kasema hivyo kweli anaji expose tu as vuvuzela. Ina maana Dr.Slaa aliomba kazi kwa watanzania ya kuwaongoza bila ya kujua job description, can we really afford another learn as you go leader in our politics.Dr.Slaa anaweza kuongea hivyo kwa sasa. Lakini hata Dr. Slaa angekuwa Rais wa nchi,maisha yake binafsi na mipaka ya nchi yake ikitishiwa,angeanza kwanza ku deal na wanaotishia mipaka ndipo angekuja kutatua ya ndani. Ukiwa unagombana na mkeo/mumeo ndani,ukasikia watu wanataka kuvunja gate wavamie kwako,cha kwanza utaenda kupambana na wanaivunja gate lako ukisha wasambaratisha ndio utarudi ndani kupatana na mkeo/mumeo.
Aliyoyaongea Dr Slaa ndio yalikuwa kichwani mwangu.Namuunga mkono Dr Slaa kwa hili.Tanzania hatuwezi kuingizwa Vitani kwasababu ya matatizo binafsi ya JK na Kagame.
Jk anatuabisha tu. Rwanda is just too a small country to argue with. Wote tunaoneka wehu kama wao. what is the difference ?
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli ya kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake.
Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo kwa vile wanatambulika kama wauaji.
Alisema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Alimshangaa kuwataka kuzungumza na watu ambao Kagame anawaita wauaji wenye asili ya kundi la jeshi la Nterahamwe, lililokuwa linaangamiza Watutsi.
Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani, hajachukua hatua dhidi wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi, alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda, amempandisha cheo, alisema.
Alisema Rais alitakiwa kuwaambia waje awapatanishe lakini si kuwaambia wazungumze na watu anaowatuhumu kuua Watutsi.
Kumezuka sitofahamu ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda, baada ya Rais Kikwete kutoa ushauri huo wakati wa mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia hivi karibuni.
Ushauri huo ulionekana kumchukiza Rais Kagame, anayedaiwa kuhutubia mikutano kadhaa nchini kwake na kutumia lugha ya matusi, kejeli na dhihaka dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania.
CHANZO: NIPASHE
Dr. Slaa sio kosa lake. Uwezo wake wa kufikiri umekuwa wa kiwango cha Josephine Mushumbusi.
Anasema Kikwete haongei na wapinzani wakati Slaa ameonekana mara kadhaa Ikulu akinywa juice. Sasa sijui walikuwa wanakunywa juice kimyakimya!!!
View attachment 105628