Hapana, kosa kubwa linalofanywa na pro-CCM ni kushindwa kusema hii siyo na hii ndiyo; Wewe kuwa Chadema na Dr. Slaa kuwa Chadema haina maana kwamba chochote atakachosema ni ndiyoooooo, litakuwa kosa la magamba hili. Labda magazeti au habari namna ilivyoletwa imepotoshwa. lakini ukweli ni kwamba ushauri wa JK hauna kosa kimantiki labda kimazingira. Marekani haiwezi kuzungumza na Al-qaeda ni kwa sababu kuu mbili. Kwanza Alqaeda ni mtandao wala si kikundi ambao haupo msituni wala mjini wala popote. 2. Nguvu za Alqaeda zimeshadhoofika sana, kwa hiyo marekani hana sababu ya kuzungumza na watu ambao tayari ni dhaifu. Lakini je? umepata kujiuliza kama Taliban ni nini? Ni Serikali au ni nini? Na kwa nini Marekani pamoja na huko nyuma kuitambua Taliban kama kikundi kinachosapoti ugaidi (na hivyo wao pia magaidi) hivi sasa kuonyesha nia ya kuzungumza nao? Halafu tukubali kwamba, Tanzania haiwezi kumshauri Marekani kwa sababu mgogoro wa Marekani na maadui zake hauiathiri Tanzania Directly kama namna mgogoro wa majirani wa Tanzania (Rwanda, Burundi) unavyoathiri Tanzania kwa kila nyanja. Mwita Maranya najua sote ni waathirika wa yule mama aliyeua Ukonga yetu lakini sitakuwa mtumwa wa kukubali kauli iliyokosa substance kwa kuwa tu ni chama kimoja. Hii ni tabia ya kulindana, tabia ambayo siku zote tunagombana na wana Lumumba humu JF.