Dr. Slaa amkosoa Rais Kikwete kuhusu Rwanda

Dr. Slaa amkosoa Rais Kikwete kuhusu Rwanda

Hayo ni maneno ya mkosaji hivi wewe una nini cha kujivunia ukaji "compare" na "achievements" za Jakaya Mrisho Khalfan Kikwete? labda kashfa za kutembea na vichupa vya sumu. Hilo nalo si dogo.

Mwenzangu na mie hata ujumbe wa nyumba kumi hauna, halafu eti una ubavu wa kumkejeli mtu ambae kafika cheo cha mwisho kabisa Tanzania. Ultimate Power. Amabachi wewe hata ndotoni mwako hakiji. Kitoke wapi?

Ungekuwa kijana mwenye maana na "productive" na majisifu yote uliyokuwa nayo ungekuwa na cha maana cha kufanya zaidi ya wewe kutwa kucha kukaa hapa JF ulumbane na sisi tuliokuwa semi retired na ma house wife.

Vijana wenzako "productive" hata hao wa chadema unawaona humu mara kwa mara? kina Zitto, Mnyika, Lema, Mbowe, Nassari? mie nakuona wewe usiyejijuwa usiyejitambuwa, huko hauko kule hauko, kutwa kucha tunashinda tunakesha wote humu. Unanini weyee? Unanchekesha, haaa!

Unajua kwa nini Mwanaasha Kikwete alifeli Form Four, tena peke yake? Alirithi akili za baba yake!!
 
Dr Slaa ameanza kuzeeka ubongo au ameanza kuvuta aina fulani ya tumbaku. Sikutegemea Slaa akose uzalendo kiasi hiki.

Nalaumu waandishi wa habari pia kwa kukosa uzalendo. Hivi nini kiliwasukuma kuandika matapishi ya Slaa? Habari kama hizi hazikutakiwa zimfikie Kagame.

Anyways Dr Slaa umesomeka vizuri na Kagame. Amekutumia friend request kwenye Facebook yako.

Huyo alishazeeka mpaka nywele kitambo tu.
 
Unajua kwa nini Mwanaasha Kikwete alifeli Form Four, tena peke yake? Alirithi akili za baba yake!!

Kufeli darasani sio kutokuwa na akili. Kumbuka hilo. Darasani mara nyingi kuna kujazwa ujinga. Kumbuka na hili pia.
 
Ili uwe rais inabidi uhutubie kina nani we kaburu?
Ili uwe rais inabidi uwe mtanzania mwenye umri wa miaka 40 na kuendelea ... s'thing like that.

Ukianza kuongelea mambo ya kimataifa kwenye mkutano wa kujadili ajira, ujue akili inaenda harijojo.
 
Aliyepewa shahada kwa kutumiwa na mabeberu?Alipata kashahafa kamoja ka uchumi tena gentleman degree unataka unilinganishe nae?Alikua waziri wa mambo ya nje for 10 good years but hajui kwanini Taifa lake ni maskini.Ni Rais lakini hajui kwanini taifa ni maskini yaani msomi mzima wa uchumi na Dokta aliyetunukiwa?He is not my peer intellectually by any description!

Sihitaji kupewa degree na Kenyatta University in exchange ya ardhi ya mababu zangu kule Mrere katika kitongoji cha Hiti kule Rombo sembuse Kibaki Road huko Bagamoyo?

Vilaza hawa hawana tofauti na chifu Mangungo wa Msovero!

Lol, taratibu ndugu usitokwe na povu.And that is why JK is your president. And that is why Chifu Mangungo wa Msovero was a chief. It is funny that there are still some who measure human intelligence and competence by using digriiiiizzzzzz. Digriiz may show that one is qualified, they do not necessarily show that one is educated. In fact you can be Educated without having qualification or any degree. And not everyone with Qualification is educated.
Go and listen to speeches given by brother, Alhaj Malcom X Ibn Shabbaaaaz; then come and tell us that he was not an educated man. That brother did not even have that gentleman degree which you seem to despise. Yet, he was constantly being invited as a guest lecturer in the most reputable institutions is the world, including Havard and Cambridge Universities.
Robert Nesta Marley (Bob Marley) once said- "I man no have education, me have inspiration. If I was educated I would've been damn fool".

Kwa ufupi, kudhania kwako kwamba digriiz ni kipimo cha weledi.... "umebhuughi meeen!!!!"
 
Nyamafu,
Hapo ndo umeona JK amekaa anajadiliana na Upinzani. Ushabiki umelewesha kiasi cha kutoelewa kila kitu kina mazingira yake! Hayo yalikuwa matembezi ya Hiari ya CCBRT na CCBRT ni chombo cha huduma kwa walemavu. Tunachoxungumzia hapa ni lini JK kakutana kujadili mgogoro na wapinzani wake na hapa ninamaanisha Chadema. Kikao pekee ni cha Kujadili Katiba Mpya, ambako hata yaliyojadiliwa hakuyatekeleza ilivyokubaliwa





Dr. W. Slaa
Hapa tunajadili zaidi uzalendo wa taifa letu dhidi ya yanayosemwa na kutishiwa na Rwanda.

Tukiwa sote ni Watanzania na wazalendo wa nchi hii, ni gharama kiasi gani kumuunga amiri jeshi mkuu katika kulinda mipaka na kutetea Taifa letu Tanzania.

Wewe ni kioo cha nchi hii katika upinzani, yakupasa uweke kando masuala ya ndani ya nchi na utazame zaidi kulilinda taifa lako. Je, ungependa nchi iharibikiwe na kuvamiwa nawe ujaaliwapo kuingia Magogoni uanze yakukute haya? Iwapo hutojitoa sasa kuitetea nchi yako, je unadhani ukiwa unaunguruma kutokea Magogoni kulishawishi taifa likuunge mkono katika moja ya sehemu kama hili lililopo sasa? Nani atakusikia?

Ukiwa ni mpinzani shupavu (kama sijakosea), hebu jaribu walau hata kumuunga mkono basi mpinzani mwenzako Mtikila kwa kulitetea taifa.

Bado naamini unayo nafasi kubwa sana kuonyesha uzalendo wako kwa taifa hili, hasa kipindi hiki. Jaribu kuweka pembeni tofauti na uonyeshe uzalendo wako.

Nahitaji sana uzalendo wako mkuu, nakuheshimu na nathamini michango yako kwa taifa. Tuwe pamoja kwa nchi yetu.

uzalendo pasipo akili ni sawa na matapishi tu!
mgogoro wa rwanda ulikuwa na namna nyingi ya kuutatua ikiwa ni pamoja na arbitration,negotiation,pamoja na judicial settlements.Rwanda na mataifa makubwa duniani wamelidhia kufuata mfumo wa utatuzi wa tatizo hilo kwa njia ya usuluhishi wa kisheria kupitia gacaca na ictr na wameweza kurudisha hali ya utulivu nchini na watu wanaishi kama wanajamii moja(they have really tried to rebuild their shattered social fabric in a period of nine years).
Here comes a guy with unreasonable idea evoking other people's endeavour as useless.
he ought to cogitate before anything else.
 
kama kawaida mzee wa kukurupuka...aka dr. SLAA

what a shame,......halafu upewe urais

Hapa ndipo Zitto anapochoka na CDM kiasi cha kufikiria agombee urais mana huyu babu sasa kachoka. I don't think Zitto would have gone as low as Slaa did. Kama Slaa anashindwa kuimba nyimbo za uzalendo wakati mgumu kwa nchi yake hivi kweli huyu ataweza kuwa rais na kulinda mipaka yetu?

Anasema JK haongei na wapinzani. Anadanaganya watanzania mchana kweupe kwa faida ya Kagame. Si juzi tu Mbowe, Lipumba, Mbatia, na Wenje walikuwa ikulu? Wakati Kagame akipata bahati ya kuona wapinzani wake anawaua.

Kwa mantiki ya aliyoyasema Slaa ni kwamba haikuwa busara hata kwa Obama kutumia ela nyingi za misaada Tz wakati kwake Marekani kuna masikini, homeless na omba omba kibao. Dr Slaa anakaribia kuwa janga.
 
=Dr.W.Slaa;6999183]Nyamafu,
Hapo ndo umeona JK amekaa anajadiliana na Upinzani. Ushabiki umelewesha kiasi cha kutoelewa kila kitu kina mazingira yake! Hayo yalikuwa matembezi ya Hiari ya CCBRT na CCBRT ni chombo cha huduma kwa walemavu. Tunachoxungumzia hapa ni lini JK kakutana kujadili mgogoro na wapinzani wake na hapa ninamaanisha Chadema. Kikao pekee ni cha Kujadili Katiba Mpya, ambako hata yaliyojadiliwa hakuyatekeleza ilivyokubaliwa

Hivi wewe ni nani hata upewe hadhi ya kukutana na Rais kila siku, umepewa fursa ya kuonana na Rais, mmezungumza, mmetowa maoni yenu na yeye ana uamuzi wa mwisho kuyakubali au kuyakataa.

Wewe babu mie nakuuliza, una ujuzi upi wa siasa za Kimataifa hata leo uwe na ubavu wa kumkosoa mtu aliyebobea katika diplomasia za Kimataifa?
 
Hoja ya Dr. Slaa ilikua kwamba Nchi haiwezi kuwa dragged vitani kwa sababu ya kauli ya Kikwete na vile vile akashsuri Kikwete aanze kwanza kukaa na wapinzani wake.

Nyie mnaongelea vita, ni wapi Kikwete kaongelea vita? Kikwete kasema, wake ulikuwa ni ushauri na unaweza ufatwe au usifatwe, maneno mengi ya nini?

babu kakosa pakutokea iliyobaki anadandia daladala hata hajuwi zinaelekea wapi.
 
hii inaonyesha jinsi gani Dr. Slaa alivyo na uwezo mdogo wa kufikiri na kutenda, kwa swala la Kagame ka weka siasa mbele na chuki yake dhidi ya JK, itashangaza akimpenda JK lakini kwa hapa alitakiwa aweke utaifa na uzalendo mbele. JK alitoa ushauri tu na haikuwa amri. Kagame kaziba mianya yote ya kufanya siasa huko Rwanda kwa kisingizio cha mauaji ya kimbali. ni nani asiyejua kuwa kagame ndio aliyetoa amri ya kumtungua habriemana akishirikiana na baadhi ya watusi waliokuwa jeshini hapa tanzania. dhamira ya JK sio kwenda vitani hata siku moja na Rwanda, ni vyema slaa na wote waliolewa pombe yake wakalijua hili. dhamira mbaya ya kagame dhidi ya tanzania inajulikana lakini sasa naona ndio ameanza mwanzo wa siku zake za mwisho. sitashangaa akishindwa kumaliza miaka miwili kama rais wa rwanda, yangu macho.
 
Mtu alikuwa Padri wa Katoliki halafu akavunja amri ya sita ya Mungu na kuzaa akiwa Padri. Kwa maana si mwaminifu kwa kanisa lake na wala jamii yake. Halafu akaja chukua mke wa mtu. Sasa huyu akipewa madaraka si atachukua wake za watu hovyo hovyo? Ndio maana hata kufikiri anashindwa hapa kuna suala la kitaifa yeye analeta upinzani wa kitoto kwa kupinga kila kitu anachofanya Rais wetu.
 
Dr.slaa kama wewe uliweza kumuiba Josephine Akiwa mke wa mtu, wanjanja nao watakuibia uanze kulalamika Kama kagame. Funga domo Lako slaa na acha upuuzi na lugha za kizembe kwa amirijeshi mkuu. Indoa njaa zako na endelea kumbaka mke aw watu.
Amiri jeshi mkuu anaeshondwa hata kuwataja na kuwaadhibu wauza madawa ya kulevya tena walioko ndani ya nchi yake ndio unamuona kiongozi shupavu?!JK anapawa kunyang'anywa madaraka maana kashindwa kuyatumia.Ni aibu kuwa na Raisi anaewaogopa wauza anga ndani ya nchi yake!
 
Dr Slaa kama kweli hii kauli haijachakuchuliwa na mleta uzi. BASI Nasema umekurupuka; hakuna ubaya wa kuwataka wasiopatana kukaa meza moja. Mbona nyie wapinzani mnashindwa kukaameza moja kuunganisha nguvuu?
au ndo kila kitu lazima upingee tuu kwa sababu ya kuuza gazeti lenu la chamaa.
Fikiria matamshi yako mzee watu tunakutegemea utuongoze kama mkuuwa nchi na amiri redguard mkuu.
 
Tena Ajabu Dr Slaa kajibu vema na kuweka sawa,
kinachomfanya yy kuja juu kwa lugha za matusi na hasira utadhani katukanwa au kakashifiwa yeye nini?
Kuna vijana wanajipendekeza ndan ya chadema na kwa viongoz utadhani waungu wao,tena kwa sababu zisizo za msingi na maana,
kichefu chefu sana

Dr.W.Slaa,

..u definetely need to do more research kuhusu mgogoro wa DRC kabla ya kuanza kuchukua upande wa Kagame au Kikwete.

..ningeshauri uwe na timu ya vijana wako wanaofanya kazi ya utafiti na kukupatia taarifa ya mambo mbalimbali.

..zaidi timu hiyo inatakiwa ukishauri kuhusu misimamo na mitizamo ambayo unapaswa kuchukua huku ukizingatia sera rasmi za CDM.

..I think u r doing too much. U have too much on your plate. kwa nafasi kama yako unahitaji timu ya wataalamu kukushauri, kukuelekeza, na kukuongoza, kwani masuala ambayo unashughulika nayo ni mengi.

cc😡Jasusi, Kitila Mkumbo, Nguruvi3

JokaKuu nakubaliana nawe kabisa kuhusu hili. Dr.W.S.Slaa anatakiwa awe katika nafasi ya kuelewa kuwa kuna kuzungumza kama mtu binafsi na kuzungumza kama kiongozi wa chama. Nadhani anahitaji washauri katika hili.

Slaa aelewe kuna vitu vutatu hapa, kauli ya Kagame, ushauri wa JK na ugomvi wa PK na Ntarahamwe.

Alitakiwa aeleze kwa ufasha na wala si suala la kuonyesha hasira zake dhidi ya JK.
Hili ni tatizo la kimataifa na approach yake si sawa na kuwaita CDM kuongea nao Ikulu.

By the way mara ngapi tumeona wakiwa wamezunguka majagi ya jusi na Togwa pale Ikulu, mara ngapi amekutana nao katika mikutano na ufunguzi wa barabara .

Dr aelewe tofauti ya kukutananishwa na kuzungumza. JK anaposema PK azungumze na wapinzani ni kwamba amefungua milango ya ima yeye au mtu mwingine kukutanisha pande hizo kwa kuwasuluhusisha. Kitu cha muhimu ni kupata ridhaa ya pande husika kwanza ndio maana JK alisema wazungumze., si kuchukua jukumu kwasababu yoyote anaweza kuwa msuluhushi.

Standard ya opposition party lazima iwe juu sana na isiache doubt kwa namna yoyote.
Kuna umuhimu wa kuangalia washauri wa mzee hasa katika mambo ya kimataifa.
Kitila Mkumbo Jasusi Ben Saanane

Shukrani sana Nguruvi3 na JokaKuu.Hatutawaangusha katika hili....!

Pia suala la kukutana Ikulu lilikua mara moja tu, je rais alitekeleza makubaliano?Maana chanzo kikubwa cha mifarakano kwa mataifa mengi ni kwa serikali kukataa kutekeleza makubaliaano yao waliyoafikiana na wapinzani.

Mkuu, kutokukubaliana na watu wako, hakukuzuii kutoa ushauri ambao ni substantial kwa watu walio nje na kwako. Haya ni mambo mawili tofauti tusiyachanganye. Tunakubaliana kabisa kwamba domestic politics, JK amefeli lakini still hiyo haiondoi essence ya ushauri alioutoa. Ni vema mambo haya mawili tukiyapa mitizamo tofauti ili tuweze kuyachambua fairly

if jk is a failure domestically how can he successful advise kagame on domestic issues? huu ni wendawazimu

Huu uzi unaonesha umuhimu wa kuangalia siasa za ndani na maslahi mapana ya nchi. Tuchukulie mfano mzuri Marekani, ndani ya mwezi mmoja wamekuja marais 3 Tanzania, na marais hawa wanatoka vyama tofauti. Wanaweza kuja kwa mgongo wa taasisi zao za kusaidia watu lakini hapo hapo kwenye kujenga mazingira mazuri kwa nchi yao kufaidika kwa kuwa karibu na Tanzania.

Linapokuja swala la maslahi ya taifa kama hili la DRC na Rwanda tulitakiwa (kama taifa) kuwa na kauli moja. Dr Slaa hakutakiwa kuongea hayo maneno hadharani. Lakini pia, nilitegemea katika sintofahamu inayoikabili Tanzania kwa kipindi hiki, basi viongozi wa juu toka vyama vikubwa vya siasa nchini wangekutakana na kuwekana sawa kuhusu 'Tanzania'. Kama ni ushauri wangepeana humo ndani lakini nje ya nchi lazima tuwe kitu kimoja.

Kagame amefanya kazi kubwa kuinua nchi yake, lakini Kagame ana upande wa pili ambao ni 'shameful' kwa Afrika. Miaka nenda rudi sisi Waafrika tumekuwa tunalalamika kuwa machafuko yanayotokea barani kwetu yanafanywa na wazungu ili waibe rasilimali zao. DRC imakuwa ni kielelezi cha jinsi gani sisi Waafrika ni wanafiki. Kagame anang'aka, si kwa sababu kaambiwa aongee na wabaya wake, lakini anajua msimamo wa Tanzania kuhusu DRC unamuumbua. Angalia pato la taifa la Rwanda lina nini ndani yake? wana-export madini bila aibu, na sasa anajua Bandari ya Dar itakamata madini yake amekimbilia Kenya.

Na iweje Kagame hakumjibu Kikwete pale pale kwenye kikao badala yake ameenda kupiga kelele nyumbani kwake? Huo ujasiri anaotamba kuwa nao aliusahau wapi siku hiyo ya kikao?

Acha kujichanganya wewe, mwanaume anaanza kutatua matatizo kwenye mji wake ndiyo awe na uwezo wa kutoa ushauri kwa jirani! Haiwezekani wewe kwako kuna ngumi zisizo na mpangilio kila leo halafu ukamshauri jirani yako namna ya kuishi kwa amani na familia yake? You must be crazy!!

You are wrong my dear na inaokana hata siasa za Marekani huzijui! Wamaekani ni wamoja ktk masuala ya kuendeleza taifa lao na sio Tanzania! Tumeshuhudia hapa kwetu masuala yote ya muhimu kwa taifa yanaongelewa kishabiki na ccm! Tumeona hata bungeni yanayotokea! Pia tumeona mara nyingi Rais Kikwete akiwakejeli wapinzani na watnzania mara nyingi! So tusidanganyane hapa, huu msala ni wa JK na ccm yake! MMESHASEMA TUPIGWE TU MAANA MMETUCHOKA sasa ya utaifa yanatoka wapi tena? Au mlikuwa mnatukana mamba kabla hamjavuka mto? Kikwete alishawahi kuwakejeli wafanyakazi na kuwaambia kama ni kura wamnyime ila wakigoma atawatuma polisi wakavunje miguu, umesahau mkuu!!

Ukinitoa mimi, nimequote yaliyosemwa na JF members ambao wana ushawishi mkubwa katika JF na misimamo yao inajulikana namna walivyosema katika suala hili. Bil shaka hawa (The Big Show, Nguruvi3 na FJM) wanajulikana vema misimamo yao na siasa zetu za ndani pamoja na mitizamo yao kwa Serikali iliyopo madarakani, lakini hawajafikia kiwango cha kuwa washabiki kiasi cha kuwa "vipofu" kwa "intervention" ya Dr. Slaa katika suala hili. Mossad II na mbwa wa Manzese, hamtakiwi kuongozwa na ushabiki katika suala hili. Lazima tuelewe, pamoja na yanayotendeka nchini, lakini JK ana nafasi yake katika masuala ya kimataifa ndio maana aliaminiwa kuongoza intervetion ya Madascar, alipewa nafasi ya aina yake wakati wa machafuko ya Kenya, na sasa amepewa jukumu la kuongoza Bridgade ya kulinda amani Hukohuko Congo DRC. Tukubali tu katika hili Dr. Slaa ni bora alitakiwa akae kimya au angeficha hisia zake za siasa za ndani katika kuzungumzia suala hili. Na kitendo cha kutohoji "wrongful doing" ya Dr. Slaa, ndio kutatupeleka kulekule kwa chama kilichopo madarakani ambao wao kila kinachosemwa na kufanywa na viongozi wao wa juu ni sawa tu, sitarajii kuiona Chadema ya namna hii au yenye wanachama wa namna hii. Busara nayoiona kwa sasa ni kupitia kwa michango ya threads za namna hii, mlio karibu na Chadema makao makuu kufanya uchambuzi wa kina wa namna ya kum-feed Dr. Slaa katika masuala ya Kimataifa na kutenganisha (for the moment) masuala ya siasa za ndani na nje linapokuja suala la adui baina ya ndani na nje.
 
Dr Slaa kama kweli hii kauli haijachakuchuliwa na mleta uzi. BASI Nasema umekurupuka; hakuna ubaya wa kuwataka wasiopatana kukaa meza moja. Mbona nyie wapinzani mnashindwa kukaameza moja kuunganisha nguvuu?
au ndo kila kitu lazima upingee tuu kwa sababu ya kuuza gazeti lenu la chamaa.
Fikiria matamshi yako mzee watu tunakutegemea utuongoze kama mkuuwa nchi na amiri redguard mk.
Mleta uzi anahusika vipi hapo?Hilo ni gazeti ambalo limekuwa copied na kuwa pasted hapa JF sasa mleta mada amechakachua nini hapo?Isitoshe umepewa chanzo sasa ni kwanini usifuatilie gazeti hilo hata online linapatikana.

Kama hujui visit www.ippmedia.co.tz
 
Ukinitoa mimi, nimequote yaliyosemwa na JF members ambao wana ushawishi mkubwa katika JF na misimamo yao inajulikana namna walivyosema katika suala hili. Bil shaka hawa (The Big Show, Nguruvi3 na FJM) wanajulikana vema misimamo yao na siasa zetu za ndani pamoja na mitizamo yao kwa Serikali iliyopo madarakani, lakini hawajafikia kiwango cha kuwa washabiki kiasi cha kuwa "vipofu" kwa "intervention" ya Dr. Slaa katika suala hili. Mossad II na mbwa wa Manzese, hamtakiwi kuongozwa na ushabiki katika suala hili. Lazima tuelewe, pamoja na yanayotendeka nchini, lakini JK ana nafasi yake katika masuala ya kimataifa ndio maana aliaminiwa kuongoza intervetion ya Madascar, alipewa nafasi ya aina yake wakati wa machafuko ya Kenya, na sasa amepewa jukumu la kuongoza Bridgade ya kulinda amani Hukohuko Congo DRC. Tukubali tu katika hili Dr. Slaa ni bora alitakiwa akae kimya au angeficha hisia zake za siasa za ndani katika kuzungumzia suala hili.

hao wamesha kula ya mbuzi.
 
Amiri jeshi mkuu anaeshondwa hata kuwataja na kuwaadhibu wauza madawa ya kulevya tena walioko ndani ya nchi yake ndio unamuona kiongozi shupavu?!JK anapawa kunyang'anywa madaraka maana kashindwa kuyatumia.Ni aibu kuwa na Raisi anaewaogopa wauza anga ndani ya nchi yake!

we unaleta mambo ya unga hapa.hili ni tatizo la kitaifa. we wawapi?
 
Back
Top Bottom