Dr.W.Slaa,
Mimi nadhani kwenye hili sakata la malumbano ya kagame dhidi ya Kikwete usilifanye la kwao, kwani nimeona hoja yako inaonyesha wazi kuwa malumbano hayo ni baina ya Kikwete (umeuvua uhusika wake kama kiongozi wa nchi) na Kagame.
Hili suala halipaswi kufanywa ni jambo binafsi la Kikwete, Dr Slaa unapaswa uelewe kuwa kikwete akitoka nje ya mipaka ya Tanzania ana kuwakilisha mpaka wewe huko ughaibuni, hivyo anapotokea mtu yeyote na kumkashfu au kumtangazia uhasama Kikwete basi ujue mpaka wewe umejumuishwa.
Ningependa kuona kwenye hili suala tushikamane kama watanzania na tuwe kitu kimoja, si vyema kuingiza tofauti zetu za kisiasa na kiitikadi kwenye mambo yanayo gusa usalama na ulinzi wetu, hapa ikitokea vita sidhani kama kuna mtu atakumbuka u-CCM au u-CHADEMA, ila utasikia watu tukililia taifa letu Tanzania.
Jambo lingine, Dr Slaa una mdhihaki kikwete kuwa ana jipendekeza kufatilia mambo ya watu wengine ilhali ya kwake yamemshinda, sidhani kama ulikuwa makini wakati ukieleza haya, ila angalau ungejisumbua kidogo kuzijua nafasi za kikwete zaidi na urais tu, ni mwenyekiti wa mambo ya usalama (SADC) kwenye nchi za kusini mwa Afrika, hivyo kushauri Rwanda ni sehemu ya majukumu yake, na hata wewe sidhani kama umezuiliwa kwenda kufanya majadiliano na Kikwete, kama amewahi kufanya hivyo wenda unaweza ukawa na hoja ya msingi.