Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Nimeyasikia maelezo ya Dr. Idrisa kwa taharuki sana ati "nchi ikilala giza asilaumiwe" hapa hatuhitaji ushahidi nikuwa ametishia kulihujumu shirika! kondoleeza rice alisema mathalani saddam hussein alikiri hadharani anasilaha za maangamizi hawakuona haja ya kusubiri ushahidi. Huyu bwana kasema asilaumiwe kwa litakalotokea kwangu mie afutwe kazi mara moja.

Mie bado naimani na Dr. Rashid hivyo nashauri ahamishiwe Bandari awe CEO huko, pia nashauri Ngereja aondolewe nafasi yake apewe Bw. John Pombe Magufuli. Nafasi ya CEO wa tanesco itangazwe tufanye International recruitment naimani tutapata CEO mzuri tu.

Zitto atimuliwe kamati ya mashirika ya umma maramoja, kwa maelezo ya spika sitta amefanya kazi isiyomhusu kwa hiyo hafai kuendelea kuwepo ndani ya kamati husika. Pia kuna tetesi siku za karibuni ameonekana akizurura ofisini kwa mtu tunaesadiki yuko nyuma ya mkenge huu. Niwakati sasa tunapaswa kuachana na siasa za ujanja ujanja.

Nashauri pia serikali ifutilie mbali mkataba wa kihuni wa mama mdogo kule kiwira, tuangalie uwezekano wa serikali kuwekeza huko hatimae tuweze kupata hizo 400MW kutoka kiwira.

Inawezekana Dr. Idrisa amekaa ulaya muda mrefu, alipoambiwa mgao akastuka, yakhe huu mgao kwetu poa tu, isitoshe fridge zetu zimejaa maji ya kuchemsha tu. Lakini Idrisa sio yule ninaemjua huyu mbona ni kama "mswahili fulani" tena kakonda mno.
 
Mh Zitto,

Unayosema yaweza kuwa kweli kabisa, uchangiaji wa mawazo hapa JF ni muhimu kuuelewa.....kuna watu wana data kamili (nahisi wew ni mmoja wapo) na kuna watu wana data nusu na kuna watu wantegemea yanayoandikwa hapa JF ndio watoe mawazo yao.

Ndio maana mwanzoni kabisa Dr W. Slaa aliliona hili na kusema kuna "missing information"....inawezekana hilo ndio limetufikisha hapa tulipo kimjadala

Notwithstanding that, kuna fact kuwa RDC/DOWANS ni matapeli fulani waliofanikiwa kutulaghai mapaka tuliwapa LC ili kuweza ku-procure/ku-supply hiyo mitambo.

Umesema kuwa Mitambo kama hiyo haiko SHOW ROOM i.e mtu unakenda na kununua......fine....Je tulipokumbwa na dharula wakati ule.........RDC waliipata ile mitambo Show room? au na yenyewe iliundwa? je ilichukua muda gani........na Je vipi ukitufafanulia (timelines) dharula tuliyokuwa nayo wakati ule na tuliyo nayo sasa hivi.

Umesema tujadili Power Masterplan....nimejaribu kui-search sijafanikiwa kuipata......naomba utuwekee hapa watu tuizamie ili tuibuke kujua kama ni kwa kiwango gani inatekelezeka na kwa kiwango gani haitekelezeki kama ulivyosema.........maana kusema tu haitekelezeki....really it does not make any sense

tuendelee kujadili

Ogah,
Kama unakumbuka iliwachukua muda kiasi gani RICHMOND kuleta mitambo yao? Walishindwa ku deleiver hiyo mitambo kwa muda ambao waliahidi. Ni rahisi sana kutudanganya Watanzania maana hatujui kutunza kumbukumbu.
I hope nchi ina options zingine za kuondoa tatizo la umeme. Imagine mimi Mtanzania leo hapa London ningekosa umeme wa uhakika hata kwa siku moja?

Mimi naamini katika uhuru wa kiongozi kuamua anachoona kinafaa na kisha kuwajibika kama uamuzi wake utaleta hasara. Hii ya wanasiasa kuingilia watendaji, itatuletea matatizo makubwa sana.

Acheni kumshambulia Zitto kwa hili, kaamua anachoona kinafaa hata kama sio popular kwa watu wengine. Hicho mimi ndio naita uongozi. Wakati mambo yanapokuwa magumu, huhitaji na huna muda wa kufanya kura ya maoni kujua ufuate upepo gani.
 
CCM IMEKUWAJE MIAKA YOTE 45 MMESHINDWA KUFUNGUA KAMPUNI YA KUWAINGIZIA KIPATO...SIO LAZMA KILA MWAKA BEFORE UCHAGUZI TUSIKIE MARA EPA MARA DOWANS MARA ID (hiki ndo kichekesho id card wakati hamna computer airport,hospital, traffic ndo usiseme, immigration etc etc) CCM 2010 MNACHUKUA LAKINI SASA ISSUE ZENU TUNAZIJUA !!!!
 
Tunaomba maelezo ya mwakyembe, vikao vyao na tanesco posho ilikuwa shs ngapi? ameshatudokeza ilikuwa nono!
 
SteveD your analogy is very correct. Sasa Powell anajuta na analalama lakini hii inabaki doa katika career yake nzuri sana!
Mi nadhani mheshimiwa Zitto angechukua time off akasome vizuri maoni yetu na pia atafakari akijua kuna watu katika kamati hii wenye maslahi including huyo Idrisa anayetutishia!
Kwa sisi wachezaji wa draft hiyo tunaita Force King
Lakini msimlaumu sana huyo Zitto Akikua ataajua nch kwa kifupi imeoza
 
...hivi hawa mofos wameshatupotezea almost 200 millions American dollars na hili deal la Richmond/Dowans lakini cha ajabu na kulipa pesa yote hiyo bado hatuna generator wala umeme na bado wanatuletea story za DHARULA zilizotuletea Richmond,bei ya 100MW gas turbine haifiki hata 100m$ na gas ni yetu wenyewe lakini sijui sida ni nini hapa?huu ni ufisadi tuu na wote wanataka 10% zao ndio maana endless spin haziishi...timua wote hawa maana kazi imewashinda na hakuna kusikiliza excuse yeyote maana wameshindwa kuleta umeme!
 
Kampuni ya Tanesco imejitoa rasmi katika mchakato wa kununua mitambo ya Dowans kwa kudai kuwa suala hili limeingiza malumbano makali ya wanasiasa. Katika kujitoa kwake kampuni hiyo imesema kuwa siku nchi ikiingia kizani wasilaumiwe wao kwa sababu watu walishindwa kufanya maamuzi magumu.

Habari ndiyo hiyo, nyamanyama na mafuta mengine baadaye!
Kwa hiyo uamuzi wa kununua mitambo hiyo sasa tuseme ndiyo imeachiwa serikali ya wakina Jakaya na Salva Rweyemamu?
Maana ni kama Tanesco wamefanya kuzila eti watanzania tutajuta kukataa kuinunua mitambo hiyo! Nchi imekwisha wal sinema haijaisha ila imeanza. Ebu subiri mtasikia wenyewe usanii utakaofuata, maana kila wakiwa na deal watakuja na kisngizio cha upungufu wa umeme.
 
I want to state here in explicit terms that, I, Kabwe Zuberi Zitto (MP), Chairman Public Investments Committee of Parliament of Tanzania, stand with TANESCO on their desire to acquire gas fired turbines to improve electricity generation to the country. I stand firm to my decision and ready to be held accountable to that. I do this in good faith. I am genuine and honest. People can say all what they want to say, so long as this decision is mine based on the information i have, technical information. So long as i reached to this decision without any influence whatsover, i stand by it.

Sio kweli kuwa TANESCO hawakuja katika kamati na alternatives. Walikuja na alternatives kadhaa na zote tulizijadili.

Zitto,
If you stand with TANESCO's mngnt, will you be ready to go down with them??

I truly sympathize with you because you have swallowed nonsense from TANESCO without knowing and you are here trying hard to protect their positions as if you know everything about electricity, tendering or even Dr. Idriss. Wake up Zitto, these are not small matters and your supporters will not forgive you for the awkward position you have taken.

  1. The alternatives you were given are not alternatives at all, those are TANESCOs long term plans. Alternatives for the DOWANS’ Gas Powered Generators should have been other Gas Powered Generators. They have to be alternatives to using DOWANS product and not TANESCOs long term plans, unless DOWANS was part of their long term plans. If you compare the onsite DOWANS to TANESCOs long term projects, how can't DOWANS win despite of its past?
  2. For Dr. Idris to compare DOWANS onsite generators to upcountry hydro, wind or coal projects, is no different from giving you a choice between getting a car in two days time or constructing a house from foundation-up also in two days time. Which one is possible?
  3. Have you enquired from manufactures for an emergency supply of similar generators? I did. Just an email and got a good response. There are more than 10 companies making similar generators. How about your committee or yourself go online, phone, fax and do the same instead of damaging your character everyday in the JF?
Try to do your Homework instead of continuing to swallow TANESCOs filthies. Good luck.
 
Ogah,
Kama unakumbuka iliwachukua muda kiasi gani RICHMOND kuleta mitambo yao? Walishindwa ku deleiver hiyo mitambo kwa muda ambao waliahidi. Ni rahisi sana kutudanganya Watanzania maana hatujui kutunza kumbukumbu.

Ndugu yangu yaani na wewe umesahau kwamba hao jamaa hata hela hawakuwa nayo. Baada ya kupewa tender ndipo wakaanza kuhangaika kusaka letter of credit. Iwapo serikali isingewakopesha tungekaa mwaka mzima tukisubiri umeme wa Richmond. Baada ya kupata letter of credit, ndipo wakaenda ku-shop hiyo mitambo, watafute usafiri na ndipo wakaja kuifunga, bado unategemea watumie muda mfupi? Hapo tutakuwa tunafanisha tui la nazi na maziwa.

Tusianze kulinganisha utendaji wa Richmond ambao wali-prove failure tangu siku walipopewa tender na ndiyo maana magazeti na hapa jamvini watu walipiga sana kelele, lakini kwa kuwa serikali huwa haisikilizi waliendelea tu mpaka walipokuja kuaibika kwa kishindo. Kila siku tukawa tunaambiwa mitambo itawasili, hakuna kitu mpaka ikabidi watafute watu wa PR [Salva Rweyemamu] kwa ajili ya kutengeneza image nzuri kwa public kwa kuwa walishagundulika kwamba ni matapeli tu.

Kama ulimsikiliza Ngeleja alivyokuwa anamuomba Mwanakijiji kwamba afagilie ununuzi wa Dowans wala usingesita kuona kwamba hakuna tofauti na jinsi Salva Rweyemamu alivyoajiriwa ili angalau atengeneze image nzuri ya Richmond. Kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza!

Kwanini huwa hatujifunzi kutokana na makosa? Kila siku tunalizwa na bado tunarejea makosa yale yale tu utadhani tumerogwa!

Kwanini Dowans alitumia miezi 6 kununua mitambo, kuileta, kuifunga na kuanza kuzalisha umeme mwezi July same year?
 
[*]Have you enquired from manufactures for an emergency supply of similar generators? I did. Just an email and got a good response. There are more than 10 companies making similar generators. How about your committee or yourself go online, phone, fax and do the same instead of damaging your character everyday in the JF?
[/LIST]
Try to do your Homework instead of continuing to swallow TANESCOs filthies. Good luck.[/SIZE]

......hao hata magari yao hawawezi kuendesha wenyewe mpaka waendeshwe unategemea wataweza kutafuta data kama hizo!
 
Nimeyasikia maelezo ya Dr. Idrisa kwa taharuki sana ati "nchi ikilala giza asilaumiwe"

No no no...Dr. Rashid hawezi kusema "nchi ikilala giza asilaumiwe." Hiyo ni reported speech! Maneno yako wewe!

Huwezi kunukuuu tafsiri yako wewe mwenyewe halafu ukaweka alama za kunukuu kama kwamba ni maneno uliyoyachukua kama yalivyo. Ni upotoshaji. Tuambie, Dr. Rashid amesema nini, ametamka nini hasa yeye mwenyewe kinywani?

Tulishaambiwa mwishoni mwa mwaka jana kwamba waziri Ngereja kasema wameghaili kununua mitambo ya Dowans. Kumbe inavyoonekana tulipewa tafsiri ya mwandishi, ya mtu tu wa ajabu ajabu bila ya sisi kusikia walichosema wao wenyewe waziri na Dr. Rashid. Ndio maana nang'ang'ania kutochukua tafsiri ya mtu.

Tujue, katamka nini Dr. Rashid?
 
Joseph Lugendo
Daily News; Friday,March 06, 2009 @20:00

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) , Dk. Idris Rashidi, ametangaza uamuzi wa kujitoa kwa shirika hilo katika nia ya kununua mitambo ya kufua umeme ya Dowans.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya kutolewa taarifa alizodai kuwa ni za uongo na zilizojaa utashi wa kisiasa zaidi, dhidi ya utaalamu wa Tanesco na kwamba zimechangia kuvunja nguvu ya mamia ya wafanyakazi wa shirika hilo wanaofanya kazi usiku na mchana kuhakikisha nchi inapata umeme wa uhakika.

Akisoma uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari katika makao makuu ya Tanesco, Dar es Salaam leo, Rashidi alisema kuwa taarifa hizo zilinukuliwa na vyombo vya habari katika kipindi cha wiki mbili zilizopita, kutoka kwa wanasiasa, wananchi waandamizi aliowaita kwa Kiingereza kuwa ni 'Senior Citizens' na watu wazito wenye majukumu na dhama kubwa.

Aidha, Rashidi ambaye alikataa kuulizwa maswali na kuwataka waandishi kuvuta subira mpaka muda wa maswali na majibu utakapofika bila kutaja siku wala saa, alionya kuwa sasa wananchi ndiyo watakaofanya uamuzi wa mwisho.

"Ni imani yetu kwamba tumeshajieleza na kujenga hoja za kutosha, na umma wa Watanzania utafanya uamuzi wao wakati nchi itakapokuwa imegubikwa na giza, hospitali hazitoi huduma, viwanda havizalishi na wanafunzi vyuoni wakishindwa kusoma," alisema Rashid.

Kwa mujibu wa Rashidi, Desemba 2008 Tanesco iliwasilisha tathmini ya hali halisi ya uzalishaji wa umeme nchini, iliyoainisha mahitaji na matarajio ya uzalishaji kwa muda wa kati na mrefu. Taarifa hiyo iIionyesha kuwa, kwa wakati huo upungufu wa nishati ya umeme ulikuwa megawati 150, na kwamba ukuaji wa mahitaji ya nishati hiyo ni megawati 75 kila mwaka.

Ilijenga hoja alizoziita kuwa ni za kitaalamu na si za kuangalia upepo wa kisiasa, kwamba kutokana na hali ya upungufu uliokuwapo, na ongezeko la mahitaji kwa kila mwaka, ifikapo Desemba 2009, Tanzania itakuwa ikikabiliwa na upungufu wa megawati 225. Alisema tathmini ya hali ya mvua ambayo ndiyo chanzo cha umeme mkubwa kuliko wote na nafuu zaidi, iliyotokana na utabiri wa hali ya hewa, ilionyesha kuwa mvua za mwaka huu hazitalingana na viwango vya kawaida.

Kwa mujibu wa Rashidi, tayari mvua katika mikoa ya Mbeya na Iringa, ambayo ndiyo vyanzo vikuu vya maji ya Bwawa la Mtera, ni za kiwango cha chini na katika maeneo mengine zimesimama. Hoja hiyo ilifafanua kuwa Tanesco ilikuwa na mpango wa mwaka 2009 wa kukamilisha miradi miwili ya kuzalisha umeme ukiwamo wa Kiwira uliokuwa uzalishe megawati 200 na wa Tegeta megawati 45.

Hata hivyo kwa mujibu wa Dk. Rashidi, mradi wa Kiwira uliathirika kwa alichoita kuwa ni malumbano ambayo yamesababisha wawekezaji wakubwa waliotarajiwa kushiriki, kujitoa. Pia mradi wa Tegeta ambao katika mipango ya Tanesco, ulikuwa uanze kuzalisha umeme mwaka huu, umechelewa na sasa utaanza uzalishaji Oktoba 2009.

Kutokana na hoja hizo, Tanesco ilifanya tathmini ya zabuni ya Dowans ya kuuza mitambo yake iliyotangazwa kwenye vyombo vya habari mwaka jana, na kupeleka mapendekezo wizarani ya kununua mitambo hiyo, kwa kuzingatia kuwa haitoshi kupeleka taarifa ya tatizo la uzalishaji wa nishati na mahitaji, bila mapendekezo ya ufumbuzi wa suala hilo.

Mapendekezo hayo yalizingatia pia unafuu na ubora wa mitambo ya Dowans, na yalitolewa kwa tahadhari kwa nia ya kuepusha Tanesco kuingia kwenye mtego usiokwepeka, wa kukodi mitambo hiyo wakati nchi ikiwa kwenye giza katika siku za usoni. Aidha, huku ikijua kuwa ununuzi wa mitambo hiyo si ufumbuzi kamili wa tatizo hilo, Tanesco iliishauri serikali kukaa na wataalamu wa shirika hilo kujadili mpango wa haraka kuhakikisha kunakuwa na uzalishaji wa megawati zisizopungua 200, katika kipindi cha miezi 24 tangu Desemba 2008.

Mjadala huo ulikuwa ulenge katika kuharakisha baadhi ya miradi iliyochelewa kuanza ya Kiwira, Tegeta na Ruhuji ambao ni wa maji megawati 350 na mwingine wa Mnazi Bay wa gesi megawati 300. Mtendaji huyo wa TANESCO alisema miongoni wa 'Senior Citizens' wanaodaiwa kupotosha umma, walipata nafasi ya kukaa na Tanesco kubadilishana mawazo kuhusu hali ya umeme, na mara zote shirika hilo limekuwa likieleza kuwa litakuwa tayari kupokea maelekezo kutoka Kamati za Bunge na Serikali kwa kuwa ndizo taasisi za usimamizi na za uwakilishi wa wananchi.

Alisema, "Hivi karibuni kiongozi mmoja amenukuliwa akisema jitihada hizi ni za kusafisha mafisadi, ni kukiuka taratibu za nchi". Rashid alifafanua kuwa kiongozi huyo hakuwa sahihi kwa kuwa hakuna wakati wowote ambao Tanesco ilisema kwamba ununuzi wa mitambo hiyo hautazingatia taratibu husika za kisheria.

Alisema mitambo hiyo haiuzwi dukani kama mavazi au trekta na kutoa mfano wa mtambo wa Warstsila ambao ulinunuliwa kwa dharura ambapo taratibu zote kuanzia zabuni mpaka kupatikana kwa nishati, ilichukua miezi 18, wakati kwa sasa Tanzania inatakiwa kupata mitambo ya dharura ili Septemba nchi isikumbwe na giza. Uamuzi wa Tanesco kujitoa katika ununuzi wa mitambo hiyo, unatokana na mjadala ulioibuka baina ya wanasiasa juu ya hatua hiyo. Mjadala huo ulitokana na kitendo cha Kamati mbili za Kudumu za Bunge kukinzana katika ushauri juu ya ununuzi huo.

Kamati ya Nishati na Madini ikiongozwa na William Shelukindo (CCM) ilishauri serikali isiruhusu Tanesco kununua mitambo hiyo wakati Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma chini ya Mwenyekiti wake, Zitto Kabwe (CHADEMA) iliunga mkono ununuzi. Hali hiyo ilisababisha Spika wa Bunge, Samuel Sitta kuingilia kati na kutoa mwongozo ambao kwa upande wake, alikuwa akiitahadharisha serikali juu ya uamuzi huo wa kununua mitambo inayodaiwa kuwa imeshatumika.

Wakati huo huo, Theopista Nsanzugwanko anaripoti kuwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeisisitiza serikali ifuate na kuheshimu Sheria ya Manunuzi ya Umma kwa kutafuta mitambo mipya kutatua tatizo la umeme nchini. Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho, Francis Kiwanga alisema nia ya TANESCO na Serikali ya kununua mitambo hiyo ya kampuni binafsi ya Dowans ambayo ni ya mitumba, ni kinyume na sheria na misingi ya utawala bora.

Alisema jitihada hizo zinakiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004 na kutengeneza msingi wa uvunjaji wa sheria. ÒKuhusu malumbano ya Bunge na Serikali kuwa ibara ya 63(2) ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 inalipa Bunge madaraka kwa niaba ya wananchi kuisimamia na kuishauri serikali katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa KatibaÓ alisema Kiwanga.
 
Ndugu yangu yaani na wewe umesahau kwamba hao jamaa hata hela hawakuwa nayo. Baada ya kupewa tender ndipo wakaanza kuhangaika kusaka letter of credit. Iwapo serikali isingewakopesha tungekaa mwaka mzima tukisubiri umeme wa Richmond. Baada ya kupata letter of credit, ndipo wakaenda ku-shop hiyo mitambo, watafute usafiri na ndipo wakaja kuifunga, bado unategemea watumie muda mfupi? Hapo tutakuwa tunafanisha tui la nazi na maziwa.

Tusianze kulinganisha utendaji wa Richmond ambao wali-prove failure tangu siku walipopewa tender na ndiyo maana magazeti na hapa jamvini watu walipiga sana kelele, lakini kwa kuwa serikali huwa haisikilizi waliendelea tu mpaka walipokuja kuaibika kwa kishindo. Kila siku tukawa tunaambiwa mitambo itawasili, hakuna kitu mpaka ikabidi watafute watu wa PR [Salva Rweyemamu] kwa ajili ya kutengeneza image nzuri kwa public kwa kuwa walishagundulika kwamba ni matapeli tu.

Kama ulimsikiliza Ngeleja alivyokuwa anamuomba Mwanakijiji kwamba afagilie ununuzi wa Dowans wala usingesita kuona kwamba hakuna tofauti na jinsi Salva Rweyemamu alivyoajiriwa ili angalau atengeneze image nzuri ya Richmond. Kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza!

Kwanini huwa hatujifunzi kutokana na makosa? Kila siku tunalizwa na bado tunarejea makosa yale yale tu utadhani tumerogwa!

Kwanini Dowans alitumia miezi 6 kununua mitambo, kuileta, kuifunga na kuanza kuzalisha umeme mwezi July same year?

exactly Keil.......thats what i said.....hawa watu tuliwapa LC i.e Letter of Credit..........mazingira ya jinsi hiyo LC ilivyotolewa ni ya ajabu sana...........na wakatuletea mitambo mwaka huohuo.......leo eti tunaambiwa it will take 20 months kwa pesa zetu wenyewe..........hivi jamani tumelogwa na nani/nini?
 
Joseph Lugendo
Daily News; Friday,March 06, 2009 @20:00
Habari nyingine

"Ni imani yetu kwamba tumeshajieleza na kujenga hoja za kutosha, na umma wa Watanzania utafanya uamuzi wao wakati nchi itakapokuwa imegubikwa na giza, hospitali hazitoi huduma, viwanda havizalishi na wanafunzi vyuoni wakishindwa kusoma," alisema Rashid.

Now we have something to work with.

Hicho, unless kuna mengine hayajaripotiwa, ndicho kilichotoka mdomoni mwa Dr. Rashid. Au?
 
Natumaini Mkurugenzi wa Tanesco atajiwajibisha mwenyewe na kuachia ngazi au la, Rais anatakiwa kumfukuza kazi mara moja.

Zaidi ya hapo, kutokana na statement yake aliyoitoa, inaonyesha wazi kuwa KAZI IMEMSHINDA NA PIA ANATAKIWA KUFUNGULIWA MASHITAKA MARA MOJA KWA KUTAKA KUVURUGA AMANI YA NCHI.

Rais alishaonya kuhusu jambo hilo mwanzoni mwa mwaka huu.
 
exactly Keil.......thats what i said.....hawa watu tuliwapa LC i.e Letter of Credit..........mazingira ya jinsi hiyo LC ilivyotolewa ni ya ajabu sana...........na wakatuletea mitambo mwaka huohuo.......leo eti tunaambiwa it will take 20 months kwa pesa zetu wenyewe..........hivi jamani tumelogwa na nani/nini?

Heheheheheee...back on your BS!
 

well anaweza kuja na solution nyingine ..lakini process ya kuagiza hadi kufunga na kuanza ..itachukua mwaka mmoja na zaidi..je wakati huo tutakuwa tunafanya nini..kwenye plan za kiuchumi lazima kuwa na mikakati ya dharura,muda mfupi ,muda wa kati na muda mrefu[normally miaka 25 mbele]...upo hapo???

PM, nakubaliana nawe kwamba procedures za kuagiza mitambo mipya mpaka iingie nchini na kuanza kazi ni ndefu na zinaweza kuchukua hata miaka miwili. Kiongozi wa shirika nyeti kama TANESCO anatakiwa awatumie wataalamu tulio nao pale ili kuangalia mahitaji yetu ya umeme na kuanza kujiandaa mapema ni jinsi gani TANESCO wataweza kukidhi mahitaji hayo. Kama sikosei matatizo yetu ya umeme yaliyoifanya nchi yote iwe kizani kwa muda mrefu yalitokea mwaka 2006 na sasa tuko katika mwaka 2009. Kulikuwa na miaka mitatu ambayo Idrissa Rashid na wataalamu wa TANESCO wangeweza kabisa kutoa taarifa mapema kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kununua mitambo mipya ili TANESO waweze kukidhi mahitaji yetu ya umeme na siyo kungoja mpaka miezi michache kabla ya kuingia kizani na kutuangushia bomu kwamba ni lazima nchi inunue mitambo michakavu na ya kifisadi ili kuepuka kuingia kizani.

Tena anashauri kwamba taratibu za serikali za manunuzi ambazo haziruhusu ununuzi wa mitambo chakavu zipindwe ili kununua mitambo hiyo. Mitambo hii bei yake ni shilingi 60 billioni haina warranty na hatujui kabla ya Richmond kuinunua ilishatumika kwa miaka mingapi.

Halafu anawashinikiza Watanzania eti nchi ikiingia kizani basi TANESCO isiulamiwe. Kwa jinsi alivyoboronga katika swala hili la mitambo ya Dowans Idrissa Rashid kweli hastahili kupewa nafasi yoyote ya uongozi na wengi tunashangaa kwanini yuko madarakani hadi hii leo pamoja na kuwepo ushahidi unaonyesha na yeye alinufaika na pesa za kifisadi alizowekewa na Mzee wa Vijisenti kwenye bank account yake ya nje.
 
Nauliza tena hii ni dharura ya nishati au ni dharura ya uchache mifukoni mwao?

Umeme ni dharura siku zote Tanzania tangu tupate Uhuru. Naomba nieleweshwe huenda neno dharura limepata maana mpya huko Tanzania.

Tuliileta Richmond kutatua dharura ya kila siku.
Leo tena tunataka kununua mitambo ya Dowans kutatua dharura ile ile.
Tuna viongozi wenye akili ya nyumbu, kazi yao kubwa ni kuongoza huu msafara wetu katikati ya kundi la simba kila msimu ukifika.

Tunataka mitambo mipya itakayo tumia Gas yetu ya Songosongo.

Tumevaa sana chupi za mitumba na kuzipa uhalali,ndiyo maana tunaona ni sawa tu kununua mitambo mtumba yenye baraka na mikono nuksi ya Mafisadi.

Watu wasilete zao kwa kisingizio cha dharura.
 
Kifupi kama mimi ndiye Kikwete basi huyu Idrissa anatakiwa kuwakilisha barua yake ya kujiuzuru mara moja.. maneno yake tu yanatosha kuonyesha hawezi kazi alokabidhiwa..
Hata hivyo labda kwa wale wasiomjua, huyu mkuu tunampa heshima yake lakini... Lol! salaaleh! hafai hata kwa kulumangia..
 
Back
Top Bottom