Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Mtaambiwa kutoa order mpaka mitambo itengenezwe ni miaka 2 kisha kuship hiyo mitambo TZ itatumia zaidi ya mwaka 1 kutokana na ships zipo busy sana.Mtaambiwa kuja mafundi kuifunga kwenye grid ya taifa watachukua mwaka kutokana na economic crisis.Watakwambia ndo maana tunataka mitambo ya DOWANS kwa vile ipo hapa hapa TZ.Ukipiga hesabu hapo tayari uchaguzi mwingine
 
Tunashukuru kwa wao kujitoa,hapakuwa na lolote isipokuwa ufisadi tu.Watu hawa wamekosa huruma kabisa na wananchi wa Tanzania.Lakini siku yao inakuja.Mapambano yanaendelea.


Ndio hilo 'jipu' lililosemakana litapasuliwa jana!? Angalau wamesikiliza maoni yetu ingawa kwa shingo upande.
 
PM,

Sidhani kama kweli serikali haina fedha. Hivi ni serikali gani ambayo huwa iko tayari kupoteza mabilioni ya fedha wakati wa dharura tu?

IPTL ilipokuja ilikuwa ni dharura, kwamba nchi ilikuwa inaingia gizani (hayo ni maneno ya Dr. Shija aki-justify kusaini mkataba sijui wa miaka 25?). Hivi ni dharura gani ya miaka 25? Matokeo yake tumefungwa kwenye mkataba ambao hatuwezi kutoka mpaka sijui 2020? Hela za cappacity charges tunazolipa kila mwezi kama zingekuwa zimeelekezwa kwenye investment moja kubwa kwenye sekta ya nishati wala tusingekuwa na hizi dharura. Mwaka jana, kila mwezi TANESCO walikuwa wanalipa kama $ 10 million kwa hao wakodishaji. Piga hesabu kwa mwaka mzima ni bei gani?

Richmond ilipokuja ilikuwa ni dharura, mwanzo ilikuwa dharura ya mwaka mmoja, baadaye ikawa dharura ya miaka 2. Zikapotea bilioni 172, na capacity charges ya milioni 152 kwa siku. Piga mahesabu ya hela ambazo zingetumika kwa miaka 2, bado unasema serikali haina hela?

Juzi wameambiwa mitambo ya Dowans inauzwa sijui $ 69 milioni, wakakimbia mbio mbio kwenda serikalini kuchukua (siyo kuomba) maana wanajua zitatolewa. Na serikali yenyewe ikaanza kupiga debe kwamba wapewe hata kama ikibidi kupindisha sheria ya manunuzi. Hiyo ni dharura genuine? Kwanini wasipindishe sheria kununua mitambo mipya?

Hata tukinunua mitambo mipya bado tutaendelea kuwadai Dowans hilo deni, na hivyo kununua kwao haimaanishi kwamba tunanunua kwa bei poa, bei iko pale pale ila tutalipa pungufu ya zile tunazowadai.

Una hoja nzuri kwamba kuagiza mitambo mipya inachukua muda mrefu, lakini muda huo uko theoretical. Kama TANESCO wangekuwa wamefanya kazi ya kuangalia option ya kununua mitambo mipya, wangekuwa na bei na pia wangekuwa na time frame na ingekuwa rahisi kuongea na PPRA ili wapindishe sheria ya manunuzi na sidhani kama wananchi wangepiga haya makelele. Tatizo wanasema tu mitambo mipya bei kubwa na serikali haina fedha, ama inachukua muda mrefu wakati wao hawajafanya lolote kujua bei wala time frame ya kupata mitambo mipya.

Kuna watu wamesema mitambo iko ready, kuna wanunuzi wali-order lakini kutokana na ukata wameshindwa kwenda kuichukua. Bado hata kama mtambo unatengenezwa kwa order, haiwezi kuchukua mwaka mzima kuunda mtambo as if wanatengeneza ndege. Tatizo tumezidi kupiga zaidi domo badala ya kutekeleza yale ambayo tunatakiwa kutekeleza na matokeo yake tunaishia kutafuta short cut ambazo zinaishia kuwa mzigo kwa shirika lenyewe pamoja na serikali.
 
nia yao sasa ni kutukomoa ili tuone umuhimu wa hiyo mitambo....we should hold them accountable if they dont take measures to cub the situation by not looking for an alternative.
 
huyu Idrissa alitununulia rada sasa anataka DOWANS
 
Huyu idrissa ama kweli unachefua roho za watu.. sasa maswala ya Ubungo yanakujaje?.. Hii mitambo si mali ya Tanesco wamenunua MIPYA na mali yao hawalipi senti kwa mtu wa kati toka day one..imeagizwa toka kiwandani kwa bei sawa na mitumba hii tunayotaka kuuziwa leo. Huo muda kwani hawakuwa nao toka wajue swala hili lina matatizo!.. 3yrs leo tunaingia wa nne uharaka huo wanauona leo au toka 2003, 04, 05 06..

Ikiwa swala ni muda mbona hasemi kuwa mkataba wa Watsila ulisainiwa August miezi miwili baada ya kuwa confirmed in June 2006..Kulingana na makubaliano yao mkataba ulianza rasmi September na Watsila waliahidi by May 2007 mitambo itakuwa imeanza kazi..

Naomba sana atueleze hizo experience zao zilitokana na vitu ganii!..kweli ni muda wa kusafirisha na kufunga au kulikuwepo na sababu nje ya vitu hivyo! isije kuwa anatumia mfano wa Ubungo kuunda hoja ya Dowans wakati anafahamu fika kuwa sababu sio kusafirisha na kufunga na wala tatizo halikuwa la Watsila kushindwa ku deliver on time..Hata hivyo by September 2007 tayari mitambo ilikwisha fungwa isipokuwa walisubiri kufunguliwa na waziri fulani wa Finland ambaye alikuja mwisho wa mwaka huo..Hiyo miezi 18 anaihesabu vipi?..

Nitapenda sana kama atalielezea Taifa hizo experience za Ubungo ili kesho tusije rudia tena maanake sisi wengine hizo experience tuliyoipata toka Richmond/Dowans hatutaki sio tu irudiwe bali wahusika wake wawajibishwe kwa kupoteza muda wote..
 
IDRISA NAE FACTS ZAKE NI KAMA politics!ina maana tanesco hawakujua kwamba wataface hiyo POWER DEFICIT?............

halafu mbona analazimisha sana?..........tena kwa vitisho vya kukaa gizani?kila kitu kinafanywa kama JANGA(CAKAMITIES).ni kama mtu anaefanya IMMEDIATE MEASURES katika kuyakabili maafa ambayo hakuyatarajia...........kama MAFURIKO,AU SIJUI NINI.

Dah!mzee idrisa UTAWAJIBISHWA TU IN ANY CASE
 
Keil,
Mkuu cha ajabu ni kwamba wakati wanaagiuza ya Watsila ni wakati huo huo walikodisha ya Richmond kwa gharama zaidi wakati hawa wote wanatupa same megawatts kisha basi tuna warrant ya Watsila kwa miaka miwili wanaendesha kazi wenyewe.
Ni kitu gani kiliwafanya kununua baaadhi na mingine kukodisha tukitoa blank chaque kwa Richmond wakati tungeweza kuwa na mitambo ya 200MV toka Watsila.. mbali na yote haya ilikuwaje tukachukua mashirika karibu manne tofauti wakati tunachohitaji ni chanzo cha kufua Umeme tena generators zinazotumia gas sio nguvu tofauti tukasema Watsila hawatengenezi solar power ilibidi wapewe mashirika mengine!!

No guys, hawa jamaa inabidi washughulikiwe yaani kila napojaribu kurudi nyuma hasira ndio zinazidi kunipanda..Ujinga mtupu, au labda mdudu kisha anza kula akili zake maanake siamini hawa watu wanaoishi kwa pills!
 
This is what we call Management by CrisisNo Planning at all
 
Kasheshe:

kama bodi yake mwenyewe imekataa, hiyo ni professionalism gani unayoongelea?

Kitila Mkumbo,

Mzalendo mwenzangu, na wewe pia waamini kwamba mashirika ya umma yana responsible board?

Hiyo board inapatikana vipi? kwa masilahi ya nani?

Mashirika ya umma yamekufa karibia yote ni board ngapi za haya mashirika ziliwahi kuwajibika zenyewe?

Ongeeni reality wakuu acheni siasa.

Agenda ya TANESCO kama TANESCO ni rahisi, ukiwaambia serikali wenye mali yao kwamba wanunue mitambo watachukua forever and yet umeme ukikosekana vidole vyote kwa TANESCO.

Sasa wao wanasema mambo marahisi sana kuna mtambo already uko site and functioning, evaluate the cost and purchase it simple...

Kama munayasoma vizuri... wa kulaumiwa ni SERIKALI sio TANESCO mmliki wa TANESCO
 
IDRISA NAE FACTS ZAKE NI KAMA politics!ina maana tanesco hawakujua kwamba wataface hiyo POWER DEFICIT?............

halafu mbona analazimisha sana?..........tena kwa vitisho vya kukaa gizani?kila kitu kinafanywa kama JANGA(CAKAMITIES).ni kama mtu anaefanya IMMEDIATE MEASURES katika kuyakabili maafa ambayo hakuyatarajia...........kama MAFURIKO,AU SIJUI NINI.

Dah!mzee idrisa UTAWAJIBISHWA TU IN ANY CASE

Ndugu yangu fuatilia mambo kwa makini TANESCO imezungumzia DEFICIT ya umeme muda mrefu sana, kabla hata ya Idrisa...

Acha siasa... IT IS A FACT kwamba umeme tulionao hauna guarantee kwamba hatuwezi kwenda kwenye mgao!!! in short! Mtambo mmoja say wa Kidatu ukiwa una matatizo tutaenda kwenye mgao kwa kuwa hakuna reserve capacity...

Hili huhitaji kulijulia hapa JF. linafahamika kwa watu wote makini
 
But every thing in this world needs planing, ndio maana Jeshi linakuwa na Stock ya silaha , askari , training etc.

Sasa tukirudi kwenye Tanesco iwe ni serikali mkosa au yenyewe tanesco kwa kutotekeleza kile walicho takiwa kutekeleza , kama kutoa pesa in time etc , ndio hapo tunapo taka kumjua mchawi wetu nani? kwamba moja anafanya maksudi ili aweke mazingira ya dharura, then watu watengeneze chao? at the expense ya kuuwa mtaji huo mdogo wa nchi na adha zingine. kwa sababu mradi kama huu si endelevu, ni sawa sawa na dawa ya kutuliza maumivi, wakati tiba ni chloroquine na si panadol.

Tatizo lilipo toke Mwaka 2006, Lowasa kama waziriMkuu aliwahakikishia wananchi kwamba serikali imejipanga na wasihofu (meaning pesa ipo au itatafuywa toka chanzo chochote ku-solve hiyo problem) sasa 3 year in tatizo linajirudia , na fedha kama unavyosema wewe hakuna kugharamia miradi mikuu, bali zipo za umeme wa dharura, je hii inaingia akilini?


nadhani kaka umenielewa ..kwa kuongezea tu ...tunapoteza muda kulaumu tanesco .....tatizo lipo serikalini...wao walikuwa na program nzima ya tanesco....sasa kama hawakutoa pesa kazi zikafanyika na hao wakandarasi..tena kamaa wale wa kinyerezi..kikwete alipotoka kwenye ziara korea mwaka 2006 mwishoni moja ya ahadi aliyorudi nao ni ya kupatikana kwa mwekezaji wa kujenga mradi wa kinyerezi...

Tanesco NI kama mwendeshaji .[dereva]...mamlaka ya mwisho ya kufanya uwekezaji mkubwa ipo kwa mwenye mali [hisa]...serikali...sasa unapotoa lawama kuna lawama za mwenye mali na lawama za muendeshaji.......sasa huwezi kumlaumu dereva kwa gari kunock engine kama alikupa mahitaji na ratiba inayotakiwa kwa ukaguzi ....wewe ukawa unamuambia afanye fanye,,,tu!!
 
Kasheshe,
Mkuu unakosea hapa unaposema wa kulaumu ni serikali wakati aliyetaka kununua mitambo hii ni TANESCO hali fedha zinatoka serikalini ambako wewe unasema huchukua forever..
Ni mtambo gani huo uliochukua forever ambao unaweza kuutolea mfano, na iweje leo Idrissa awe nje wakati ni yeye aliyetoa hoja ya ununuzi wa mitambo ya Dowans (tunayoipinga)..
Mkuu swala lipo pale pale kuwa mwaka 2006, Tanesco walipewa fedha na tumeona mitambo ya Watsila ikinunuliwa halafu hao hao wakachukua contract za kina Richmond..wahusika ni wale wale tu mkuu wangu kwani huyo Idrissa katokea - kavutwa toka wapi!..

Mbali na yote hayo mega watts 100 zinaweza kutosheleza only asilimia 20 ya mji wa Dar kama estimate za mitambo ya Watsila ambayo ni imara na yenye sifa kubwa kuliko hiyo ya Dowans, hivyo hili swala la nchi kuingia kizani linatoka wapi?..
 
Nafikiri swala sio Rais wetu yuko upande upi,

Tazama aliwahi kuulizwa na mwandishi mmoja kule Paris juu ya umasikini wa afrika, akajibu namnukuu " hata mimi sijui kwanini mpaka leo sisi ni masikini" Hili ni jibu la mpumbavu haswa akiwa kiongozi wa nchi Aliye ingia madarakani na kukuta Gari mpya za aina ya benz mpya kwa ajili ya msafara wake zimenunuliwa punde tu kwa mapesa mengi lakini baada ya miaka mitatu ananunua gari nyingine aina ya BMW kwa mapesa mengi tu, bila hata ya kutueleza wananchi zile nyingine zina matatizo gani?????

Kwenye nchi maskini kama hii, inashangaza, tazama kama ukinunua gari mpya inaweza kutumika hata miaka ishirini kama inatunzwa vizuri, Haya kuna mradi wa vitambulisho vya Taifa utakaogharimu bilioni 200, hiki ni kichekesho kwenye nchi ambayo watu hufa kwa malaria na mama wajawazito kwa kujifungua, na albino na vikongwe kwa baadhi ya watu kukosa elimu kwa sababu tu eti hakuna pesa za kutosha kuweka zahanati na shule ili watu waondokane na ujinga, inashangaza priorities zetu ni zipi? Hivyo vitambulisho ni muhimu kuliko elimu na uhai wetu?

Tazama ziara yake ya bandarini ndio iliyo nitia kishefushefu kabisaaaaa, aliwauliza kuhusu idadi ya container ( makasha ) yaliyopo na yaliyokwishatolewa akajibiwa bado wanafanyia kazi eti kwa sababu bado wanatumia manual hawana computer, jibu lili tolewa na waziri mwenye dhamana yeye akacheka tu, huu ni upuuzi kwanini hatimui waziri na watendaji wa bandari kama bandari inanunua vogue ya mamilioni kila baada ya miaka miwili kwa ajilia ya mkurugenzi mkuu kutembelea hivi hawaoni kwamba wakiacha kununua mwaka mmoja tu hiyo pesa inatosha kuweka mtandao wa computer ili kazi ifanyike kwa ufanisi faida ikue mara dufu hapo wataweza kununua hata gari kama analotembelea Obama?

Yapo mengi siwezi kuandika yote yanatia hasira sana,
 
Phillemon Mikael,

Mku hapa tunazungumzia swala la Dowans ambalo Tanesco inahusika toka wakati wa Richmond..Hyaa ya Kinyerezi ni mada nyingine kabisa..Hivi ikiwa wao wameshindwa kuwekeza fedha walizopewa kwa mradi wa dharura wataweza vipi kumudu mradi mkubwa..

Ebu rudia tena kusoma ni fedha ngapi tunapoteza kila siku kutokana na mkataba feki wa Richmond, unataka bado kumlaumu Kikwete, hivi kweli kama Tanesco kwa miaka mitatu iliyopita wangekuwa wakipata faida tungekuwa bado tunahitaji msaada wa serikali?.. hizi bail out zitakwisha lini!..why Tanesco wali contract mashirika kama haya kutuuzia Umeme wakati waliweza kabisa kununua wao kama walivyofanya na mitambo ya Ubungo.. Si wao ndio waliweka sahihi za mikataba yote tumlaumu nani ka sio wao.. They have final say hata ktk swala hili tumeambiwa kuwa Tanesco ndio wenye sauti ya mwisho wakisema wanunue, mitambo itanunuliwa..Sasa kama Idriussa alikuwa na uhakika wa kufanikiwa iweje achomoe!..kiongozi ni lazima ujiamini kwa maamuzi yako sio kuja na kulalama kuilalamikia serikali wakati wewe ndiye umelamba dume..
 
keil miaka ya 90"s aliyeingiza tanzania mkenge wa karne IPTL sio shija ..bali ni aliyekuwa waziri wa nishati na madini wakati huo MEJA [baadaye LT.COL] jakaya mrisho kikwete...!

kwa kifupi ccm wanafanya TANESCO shamba lao ...MIMI nitakuwa wa mwisho kulaumu utawala pale ..pale kuna mapesa so ccm wanawaburuza sana....serikali mara zote wanaponunua mitambo huwa wanaingilia taratibu za ununuzi...mimi nadhani bora hazina ingekuwa inawapa pesa tanesco watekeleze miradi wenyewe badala ya kuwaingilia ...

nina wasi wasi kuwa kikwete na serikali yake wanaweza kuwa chanzo cha kuchelewesha kutekeleza mapendekezo ya tanesco ya mwaka 2006....ili kupata dharura ya leo...

uchaguzi mkuu unakuja na matajiri wengi waliotoa mapesa 2005 wameshaumizwa ....inahitajika njia mbadala kupata pesa za uchaguzi ....bilioni 30 kutoka kwenye hiyo bei ya bilioni 69 zinaweza kuwa pesa za kikwete again 2010[kikwete tena 2010] project!..kama hamuamini kamati kuu itakaa na mtaona itakachowafanyia kina mwakyembe na sitta kwa kuwakosesha pesa za uchaguzi.....si mmeona wameshamtuma serukamba apeleke message!!!

TUPELEKE KAINZI KAMATI KUU LEO PATAKUWA HAPATOSHI!!!

tukitaka kuwapima dowans imani watupe mitambo kwa mkopo usio na riba utakaoanza kulipwa mwaka 2012!

lakini tunahitaji umeme ..haraka tufanyeje???
 
Hivi Watanzania ni wajinga sana (mabwege au mazezeta) kiasi kwamba wababaishaji ndio wanatunukiwa nishani?? Kama mtu ameboronga huko kote kwa nini aendelee kuongoza shirika nyeti linalosimamia uhai wa Taifa kama TANESCO?

Kwa wajuvi wa sheria; ni kitu gani kama raia tunaweza kumfanya mtu huyu? Kwa hali ilivyo inaonekana aliyemteua au ambaye ana mamlaka na kitumbua chake hana shaka naye (he is very happy with his performance)!!

Kazi tunayo, tena siyo ndogo!!🙄

No. Hakuboronga huko kote na ndio maana kapewa Tanesco aiweke sawa, ilikuwa hoi bin taabani, Dr. Rashid ndio aliyoi-save, na madudu yote ya Tanesco kayakuta na ndio anajaribu kuiweka sawa.

BOT hali kadhalika, aliyakuta madudu akaweka sawa na alipoondoka tu, madudu yakaanza upya, matokeo yake nadhani mnayafahamu.

Voda, kaifanyia kuwa kampuni ya mawasiliano yenye nguvu (kwa idadi ya wateja na mapato) kuliko kampuni nyingine yeyote ya simu Tanzania.

Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni!
 
Phillemon Mikael,
Mku hapa tunazungumzia swala la Dowans ambalo Tanesco inahusika toka wakati wa Richmond..Hyaa ya Kinyerezi ni mada nyingine kabisa..Hivi ikiwa wao wameshindwa kuwekeza fedha walizopewa kwa mradi wa dharura wataweza vipi kumudu mradi mkubwa..
Ebu rudia tena kusoma ni fedha ngapi tunapoteza kila siku kutokana na mkataba feki wa Richmond, unataka bado kumlaumu Kikwete, hivi kweli kama Tanesco kwa miaka mitatu iliyopita wangekuwa wakipata faida tungekuwa bado tunahitaji msaada wa serikali?.. hizi bail out zitakwisha lini!..why Tanesco wali contract mashirika kama haya kutuuzia Umeme wakati waliweza kabisa kununua wao kama walivyofanya na mitambo ya Ubungo.. Si wao ndio waliweka sahihi za mikataba yote tumlaumu nani ka sio wao.. They have final say hata ktk swala hili tumeambiwa kuwa Tanesco ndio wenye sauti ya mwisho wakisema wanunue, mitambo itanunuliwa..


mkandara ..

unakosema kama unasema tusimlaumu kikwete na ahadi zake za alinacha...yeye ndiye aliahidi kwa mdomo wake kushughulikia haraka upatikanaji wa umeme wa kinyerezi tena akasema ana wawekezaji toka korea ...huo ulikuwa mwaka 2006....baada ya hali ya umeme kutengemaa ...ishu ya kinyerezi imesahaulika ...tunaikumbuka leo..,kama angeendelea na nguvu ile iile 2006 ule mradi ambao ungetumia gesi asilia ungekuwa tayari.....

Kuhusu pesa tanescoo wanazolipa hawa iptl ,na wenzao ..mjuwe zile zinatoka kwenye makusanyo ya bili...ambapo asilimia 80% wanazitumia kuwalipa makampuni yanayozalisha asilimia 40 tu ya mahitaji......serikali inaingia mikataba na kutoa mitaji lakini wanaawachia mzigo TANESCO kuendelea kulipa capacity charges..hii inafanya tunalipa bili kubwa....hata ule mradi wa richmond wataalmu wa tanesco waliukataa kwa sababu walijuwa mwisho wa siku wao ndio wangekuwa na jukumu la kuwalipa kila mwezi kiwangi kikubwa pamoja na kuwa serikali inalipia manunuzi....
 
Kipa,
Kikwete ana makosa na mapungufu yake lakini sio ktk hili..Ikiwa sisi tumeshindwa hata kutumia vizuri fedha zilizotolewa kwa dharura kweli tunaweza jenga nchi ktk miradi ya muda mrefu..Trust me, matukio yote haya nadhani ni bora ungewatazama viongozi wetu wanaoendesha shughuli hizo kabla ya rais..Kikwete atafukuza wangapi..
Huko CCM karibu asilimia 80 wameoza sasa Kikwete ni ktk fungu la kaa walioko ktk kapu wanasubiri kuchomwa..Binafsi naanza kuamini kabisa kwamba hakuna mtu yeyote anayeweza kuibadilisha CCM na Ufisadi ni ukweli ambao hatutaki kuukubali..
The only way out ni kutochagua CCM wameshindwa kama KANU, ZAPU, UPC na vyama vinginevyo vilivyoletea Uhuru barani..waliobakia wote ni madikteta tu!
 
Back
Top Bottom