MadelawaMadilu: hoja yangu imeniacha hoi hasa ya kukosa uzazi wa mpango! Lakini hii dharura ya umeme ni kama uhaba wa chakula, or what say you?
Unaweza ita dharura ya kila siku
Tunaingiza Mashangingi ya nguvu sana ili tuweze kukatiza nyika za Tanzania kiulaini. Wakati huo huo hatuagizi matrekta, hata Used Tractors tu.
Hivi tukiwa na njaa ni dharura?
Jembe la mkono tunalihusudu sana. Yapata zaidi ya miaka 20 ilopita kulikuwa na noti ya shillingi 100 ikiwa na wanafunzi wawili wakilima kwa jembe la mkono bila kuwa na viatu miguuni. Sijui ni mbumbu gani alisagesti picha kama ile iwekwe katika noti. Wakati huo nilikuwa bado sekondari, pamoja na upeo wangu mdogo nilijua wazi kwamba kuna waheshimiwa wengi huko serikali wenye mawazo finyu kama picha yenyewe ilivyokuwa. Tunajivunia sana umasikini wetu, tumefikia mahali tumeamua kuufanya iwe kama tunu ya kitaifa.
HAta tukienda nchi za watu wengine hatukosi kuutaja umasikini wetu kama kionjo cha mazungumzo.
Nani kati yetu hapa,ambaye atakuwa hai miaka 25 ijayo,hajui kwamba tarehe kama hii mwaka 2010 muda wa saa 2 usiku atahitaji sahani ilo shena msosi?
Kama jembe la mkono linaweza kutupatia shibe ya kiwango hiki kilimo cha Matrekta kitatupa shibe kubwa namna gani?, tukiwa na matrekta 10,000 yanayotifua ardhi ya kule Malinyi na Kondoa kwa yule Mzee Mzembe Mustafa hiyo njaa itajibanza wapi?
Unaweza ita dharura ru kama unapenda.
Wajerumani walifanyia utafiti wa kisayansi juu ya Stigler Gouge enzi hizo za 1800, sisi leo bado tunaona taabu hata kusoma kwa makini kile walichokifanyia utafiti??!!!
Tunapenda mambo laini, mambo ya muda mfupi na sifa za haraka haraka, wakati huo huo tunazaa sana tukitegemea wazungu na waarabu watatusaidia na matatizo yetu, tumelogwa??!
KWa taarifa yako sisi watanzania tuna tatizo la nishati kila siku kwa sababu watanzania zaidi ya 75% hawana nishati ya umeme hata hivi niandikapo maneno haya, japo ni kwlei kwamba wanafaidika kwa namna moja au nyingine na nishati hiyo lakini si moja kwa moja. Taabu ni pale wale wachache waanzapo kukosa nishati hiyo, neno dharura hupewa kipaumbele japo ukweli ni kwamba dharura ya nishati ipo siku zote.
Kma dharura ya umeme ipo leo ilikuepo jana na ilikuwepo siku tulipo pata Uhuru miaka 48 ilopita, vipi leo hii Wabunge na viongozi wa serikali na mashirika yake wanatuambia kuhusu dharura ya nishati??
Hii nidharura ya nishati au nidharura ya nishati mifukoni mwao??!