Zitto ni msomi mwenye upeo mkubwa sana. Uwepo wake katika siasa za Tanzania ( Bungeni ) umeleta mwelekeo mpya wa uendeshaji wa bunge letu na siasa kwa kitaifa kwa ujumla wake.
Kama binadamu ana mapungufu yake, lakini by far mapungufu yana out-weigh mazuri.
Sakata la mikataba ya madini, ufisadi na hata kuanguka kwa serikali nzima (Richmond-gate) kote huko kna mkono wa Zitto.
Jamaa kwa umri wake na hata elimu yake amefanya makubwa sana kwenye siasa zetu kuliko akina Mzindakaya ambao tuna wasikia toka tukiwa wadogo, tunasoma na mpaka tu watu wazima. Wengine kwenye mabenchi yao bungeni kuna vishimo kwa kupiga makofi kuunga mkono miswada mbalimbali ya serikali.
Hakuna ubaya kutoa criticism kwani kwa namna bora kunamjenga na kumsadia mlengwa, lakini wengine mnakuwa critical kwa minajili ya kumkatisha mtu tamaa kwa sababu tu ya msimamo wake fulani ambao kwa namna moja au nyingine mtu haukumfurahisha. Nitoe mifano miwili ya haraka; suala la Zitto kugombea uenyekiti Chadema na yaliyojiri kutokana na hatua hiyo yameacha makovu kwa baadhi ya watu, lakini we need to get over it and move on. Whether it was bad move or good one let by gone be by gone. La pili suala la Dowans, hili limewagawa watu ( hususan washabiki/wenye mapenzi na Zitto ) kwenye mapande mawili. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa katika hili Zitto kaweka msimamo wake tena very firm na if anything jamaa ndio kiongozi pekee alie wa face watanzania na kuwaeleza nini kifanyike kuliko hata hao wenye dhamana waliojifungia ndani na kushindwa kusema kitu. Haikuwa nia yangu kuleta mjadala wa Dowans hapa, lakini ninachotaka kusema Zitto ni zaidi ya Uenyekiti wa Chadema na Dowans, ana potential kubwa sana kwa taifa apewe ushirikiano sio kukatishwa tamaa na kama kuna criticism then basi ziwe constructive one.