Defining, Refining and Understanding Zitto Kabwe

Salim alikuwa Mwafrika wa kwanza kugombea Ukatibu Mkuu wa UN na kukaribia kuupata kama sio msimamo wa Nyerere kuhusu Ujamaa na kazi ya Salim aliyofanya kuuingiza China katika UN badala ya Taiwan ambayo wamarekani waliitaka.

Sahihisho halikuwa kwenye hili ... sidhani kama kuna anayepinga hili.

Narudia Mwafrika, mheshimiwa Mbunge mwenzangu kutoka chama changu, kuwa Salim was the first African South of Sahara to contest the seat to final! He was the first African actually.................. combined south and north.

OMG, OMG, OMFG, OMG,

Hureeee, hureeee, hureeee, hureeee,

Nimeteuliwa ubunge, nimeteuliwa ubunge, nimeteuliwa ubunge.

Huree chama cha Zitto kwa kuniteua mbunge, hureeeeeeeeeee.

-- Angalau sasa unatumia first badala ya only.
 
Zitto, with heshima kwako ni kuwa huyo Omary mara zote yeye amekuwa akiitukana CHADEMA na kukufanya wewe pekee ndio mwenye uwezo huko CHADEMA na hilo linakulewesha wewe na ndio maana humkemei hata siku moja kwani jambo kama hilo ndio linaweza kuwa mwanzo wa kukuweka mbali na chama chako kama bado unaamini hivyo.

Pili, unasema kuwa yeye ni msaidizi maalum wa Salim kwenye nini haswa isije ikawa ni nyumbani kwani najua kuwa Salim ni waziri mkuu mstaafu na hivyo hupewa wasaidizi ambao wanalipwa na kodi zetu sasa yeye anafanya kitengo gani?

Omary amekuwa centred kwa sababu yeye amekuwa kama msemaji wako hapa jamvini na mara zote yeye atakutetea tuu hata kama hauko sahihi , kumbuka wakati wa issue ya Dowans niliandika na kumtaka Omary asikuelekeze huko alikokuwa anaenda na sasa imedhihirika kuwa msimamo wako haukuwa sahihi na hata wewew mwenyewe umetoa tena msimamo mwingine kuwa mitambo iliingia kifisadi hivyo yafaa itaifishwe naye Omary tena akaunga mkono.

Ndio maana nasema kuwa Omary hafai kuwa mshauri wako kwani yeye anasikiliza wewe unamwambia nini ndicho anachokifanya badala ya kukushauri, na kama huyu kweli anamshauri Salim ......sijui lakini kwenye jambo gani.........

Usiwe na hasira Omary akiwekwa hadharani mbona yeye anaweka wengine hadharani? mkuki kwa nguruwe?

Kiranja,

Unakumbuka wakati wa uchaguzi wa CHADEMA? Omar aliipondea sana chadema hapa (wakati akimtetea Zitto - baada ya zile rants za zitto dhidi ya wachaga). Mimi nilimuuliza kama alikuwa anaongea kwa niaba ya Zitto au kwa niaba yake mwenyewe (kama Omar) - sikuwahi kupata jibu la wazi na hakika.

Omar anapenda sana kusema wengine ila inapokuja kwake na Zitto, anakuwa mchungu sana kama pilipili.
 
Sahihisho halikuwa kwenye hili ... sidhani kama kuna anayepinga hili.



OMG, OMG, OMFG, OMG,

Hureeee, hureeee, hureeee, hureeee,

Nimeteuliwa ubunge, nimeteuliwa ubunge, nimeteuliwa ubunge.

Huree chama cha Zitto kwa kuniteua mbunge, hureeeeeeeeeee.

-- Angalau sasa unatumia first badala ya only.

Nililiona hilo.....nikataka nibonyeze kifute...kuireport ile post, for ''almost'' name calling.....!
 
Zitto,

..Salim kuwa Mwafrika wa kwanza kugombea haimaanishi kwamba he was the most qualified.

..kwa maoni yangu wagombea kama Dr.Bernard Chidzero wa Zim alikuwa more qualified than Salim Salim.

..halafu ukizingatia misimamo ya Nyerere ktk medani ya siasa za kimataifa, hivi Salim Salim alikuwa anagombea kwa nia ya kushinda nafasi hiyo, au they just wanted to make a statement?
 
Zitto,

..Salim kuwa Mwafrika wa kwanza kugombea haimaanishi kwamba he was the most qualified.

..kwa maoni yangu wagombea kama Dr.Bernard Chidzero wa Zim alikuwa more qualified than Salim Salim.

..halafu ukizingatia misimamo ya Nyerere ktk medani ya siasa za kimataifa, hivi Salim Salim alikuwa anagombea kwa nia ya kushinda nafasi hiyo, au they just wanted to make a statement?

I think it was more of a statement than anything. Kinda like Al Sharpton running for president of the Unites States.

Ila wengine wanaona eti ni ujiko flani hivi....
 
kiranja;641057]
Tangu huyu Omarillyas amalize chuo pale mlimani na Zitto mwaka 2002 ameishia kukaa karibu na wakina Membe hapo wizara ya mambo ya nje na kutumwa kama messanger wa wizara mara leo yuko naye Sullivan huku akijua kabuisa kuwa mkutano wa Sullivan uko ama ulikuwa kwa ajili ya wafanya biashara na wajasiriamali yeye humo alienda kama nani wengine hatujui.

Mwenzio nilimaliza na kupata among the highest GPA's na hata kuwa na uwezo ulikubalika kukufundisha wewe sasa sijui wewe kama unaweza kutoa ushahidi wowote wa hata kumaliza masomo yako pale UDSM. We subiri tu kule unapokwenda wakudai degree yako unayojidai uliipata pale mlimani wakati haipo.....

Siyo, Sullivan tu na mikutano mingine mingi tu katika mabara matatu ya dunia hii ambayo kwa faida yako na wengine wa aina yako ninaambatanisha sehemu ya CV yangu hapa. Sijui nawe unayo maana ukitengeneza majungu na majigambo hapo CHADEMA sijui kama kuna lingine ulilofanikisha. Ofcourse ukitoa maslahi ya tumbo....



Pili , kila mara anaenda Newyork kwenye ubalozi wa Tanzania kule na amekuwa mzigo kw3a wafanyakazi wa ubalozi na mpaka sasa wizarani kuna malalmiko mengi sana juu ya majungu yake ambayo amekuwa akiyaleta kwa sababu anazozijua yeye binafsi kutokana na yeye kujikuta yupo karibu na Membe pamoja na wakina Jack Gotham enzi zile za Great lake region....
Hayo ya majungu ni rahisi wewe kuamini kwani ndio dira ya maisha yako hivyo sina haja hata ya kukujibu.

Omary kukusaidia wewe nenda katafute kazi ya kufanya ili uwe bize na hilo litaweza kumpunguzia Zitto presha ambazo zinatokana na wewe kukosa kazi ya kufanya na hivyo kila mara unakuwa unampotosha .
Ningekuwa nampotisha angekuwa mbunge mashuhuri Tanzania kwa asilimia 25% ya sample ya watanzania na hata kujulikana kote Africa na pande zingine za dunia.

Unadhani Zitto ni kilaza kama wewe eti atakuwa anapotoshwa na watu kama unavyompotosha bosi wako.

Lingine tafuta chama cha siasa na jiunge nacho kama hao CHADEMA hawakufai wewe nenda kajiunge na kingine utakachoona kuwa kunafaa zaidi.
Unadhani siasa ni chama na bila ya chama hakuna kufanya siasa. Sio kila mtu anatawaliwa na ndoto ya kuwa mheshimiwa kama ulivyo wewe hata kufikia kujikweza kama vile wewe ndiye mfadhili mkuu wa CHADEMA. Wengine what matters ni significance ya tuyafanyayo bila kujali kuwa fulani.

Ondoa kambi ya Salim kwani mpaka sasa JK ndio anaongoza hivyo hata ukiwa na hasira za kunyimwa kazi Foreign usitake kuwahusisha CHADEMA.
This shows how oppurtunistic u are.......Sishangai kwani mpo wengi wa aina yako ambao kwenu kazi ya foreign ndio mwisho wa ndoto zako kimaisha....Think big kaka and you will do this country a great favour....

Nimempa ushauri huyu mdogo wangu kwani naamini sasa yeye ndio anatumiwa kuwavuruga viongozi wa CHADEMA na haswa kwa kumtumia Zitto katika kufanikisha kazi hiyo ambayo anaifanya.
Yaani hiko kitambi na huo uheshimiwa wa kulazimisha tayari umeshakupa jeuri ya kujiona wewe ni mkubwa wangu. Unasahau hata waliokufundisha kuchomekea na kuongea na jamii ukaeleweka.....sasa wameshakuwa wadogo zako..du

Kuhusu Zitto, anapaswa kutulia na kuondoa vinyongo na visasi, anayempinga asimuone kama adui ila awe tayari kukaa naye na kumuuliza sababu za huyo mtu kumpinga na akiona ana sababu za msingi ajifunze ila akiona hazina maana basi ampuuze ila kimoyomoyo na kuondoka zake.
Je ninyi mmeondo vinyongo na visasi. Ingekuwa hivyo mngendelea na sumu zenu mnazoendelea kumwaga bila ya mafanikio pamoja na hao "wapiganaji" wenzenu kina Mwakyembe na Mengi.

Pili, aachane na wapambe ambao ni nuksi na kila anachowaambia wao hawatofautiani naye , hao hawatamfikisha popote pale zaidi ya kumwangamiza kisiasa
Well, si ajabu ukaona hivyo maana kwako wewe urafiki is equal to upambe kama ufanyavyo kwa huyo bosi wako unayemjaza chuki na fitina kila kukicha....
 
Nililiona hilo.....nikataka nibonyeze kifute...kuireport ile post, for ''almost'' name calling.....!

I know,

Tatizo ni mis-information tu na wala sio nia mbaya toka kwa Zitto (ninavyodhani mimi).

Unajua kuna watu labda kwa kusahau kuwa, kwa muda mrefu sana hapa jf, mimi nimekuwa upande wa Zitto, nikimtetea kwa nguvu zote, na mara zote nikiondoa kila aina ya doubts kwenye benefits (ooopppsss) zake bila swali au mashaka yoyote, and all of a sudden, kila kitu kimebadilika; wameanza kuhangaika sana kujua kilichosababisha mimi nimgeuzie kitabu Zitto.

Simwamini tena Zitto kwa chochote anachosema, ninaweka miguu yake kwenye moto (kisiasa) kila nikimwona hapa jamvini, ninauliza kwa kina kila kitu anachoshauri au kusema - only and just because ..... I can?

No way .... Just because Zitto alisaliti imani yangu kwake. Kuanzia issue ya Buzwagi hadi dowans, kuanzia kamati ya madini hadi bajeti ya juzi ya serikali ya Kikwete.

Zitto alisaliti imani yangu kwake kama kiongozi na kwa hili, wapambe wa Zitto (na unfortunately Zitto mwenyewe) wameshindwa kulielewa hili na sasa wameanza kutafuta mtu wa kumlaumu kwa hili.

Alianza waberoya - kwa kusema kuwa ananijua mimi ni mchaga wa wapi, na leo kamalizia Zitto kwa kuniteua mbunge wa chadema. Zitto analishwa kasa hapa (msemo wa vijana wa mlimani) na yeye hajui. Atakosana na kila kiongozi wa chadema kwa kudhani kuwa kinachomtokea hapa JF ni mpango wa viongozi wa chadema kummaliza.

Ningemshauri tu achukue muda kujifikiria. Ashughulikie ushauri anaopewa na watu kama Jokakuu, Mkandara na wengine hapa jamvini. Aangalia kila anachotamka na aendelee kujifunza kujishusha na kufanya kazi na wenzie.

Otherwise, anakoelekea ........ sijui tu.
 
Kiranja,

Unakumbuka wakati wa uchaguzi wa CHADEMA? Omar aliipondea sana chadema hapa (wakati akimtetea Zitto - baada ya zile rants za zitto dhidi ya wachaga). Mimi nilimuuliza kama alikuwa anaongea kwa niaba ya Zitto au kwa niaba yake mwenyewe (kama Omar) - sikuwahi kupata jibu la wazi na hakika.

Omar anapenda sana kusema wengine ila inapokuja kwake na Zitto, anakuwa mchungu sana kama pilipili.

Dada yangu hata kama wewe umaamua kuwa adui wa Zitto, lakini kamwe siwezi kukuvunjia heshima, kama dada yangu (ofcourse mimi mkubwa kako) lakini pia daima natambua mchangu wako huko CHADEMA lakini pia utahi wako wa kuona Tanzania iliyo na demokrasia ya kweli inapatikana.

Hata hivyo, napenda kukupa tu ushauri, hilo kundi la majungu na fitina la kina kiranja linakupeleka kubaya lakini pia ndio adui wa CHADEMA na sio Omar.

Kuhusu kumsemea Zitto, sidhani kama nimewahi kumsemea isipokuwa bila ya kujali athari zake, kama rafiki ambaye urafiki wetu unajengwa sana kimisimamo, mitizamo, principles na hata itikadi ingawa mwenzangu kidogo amekumbwa na UCHADEMA kiasi fulani, nimekuwa mstari wa mbele kusema yafuatayo,

Moja, yale ambayo kutokana na nafasi yake kiuongozi na maslahi ya kichama, Zitto anashindwa kuyasema hapa hivyo wewe na wenzako kwa kutumia vivuli vyenu mmekuwa mstari wa mbele kujaribu kumsemea mambo ya uongo na fitina.

Pili, naamini kuwa ni wajibu wangu kumuelezea Zitto kwa jinsi nimjuavyo mimi ili kubatilisha sumu na majungu yenu mayopenda kuyamwaga hapa wakati mwengine kwa kushirikiana na haohao mnaojigamba kuwa ni adui zenu.

Tatu, naamini kazi na style ya uongozi na siasa anayotumia Zitto inalenga zaidi maslahi ya taifa zaidi ya chama hivyo naamini nina wajibu wa kumsaidia katika kufanikisha mengi ambayo naamini ni kwa faida ya Tanzananjema niiotayo kila siku....

wasalam....
 
I know,

Tatizo ni mis-information tu na wala sio nia mbaya toka kwa Zitto (ninavyodhani mimi).

Unajua kuna watu labda kwa kusahau kuwa, kwa muda mrefu sana hapa jf, mimi nimekuwa upande wa Zitto, nikimtetea kwa nguvu zote, na mara zote nikiondoa kila aina ya doubts kwenye benefits (ooopppsss) zake bila swali au mashaka yoyote, and all of a sudden, kila kitu kimebadilika; wameanza kuhangaika sana kujua kilichosababisha mimi nimgeuzie kitabu Zitto.

Simwamini tena Zitto kwa chochote anachosema, ninaweka miguu yake kwenye moto (kisiasa) kila nikimwona hapa jamvini, ninauliza kwa kina kila kitu anachoshauri au kusema - only and just because ..... I can?

No way .... Just because Zitto alisaliti imani yangu kwake. Kuanzia issue ya Buzwagi hadi dowans, kuanzia kamati ya madini hadi bajeti ya juzi ya serikali ya Kikwete.

Zitto alisaliti imani yangu kwake kama kiongozi na kwa hili, wapambe wa Zitto (na unfortunately Zitto mwenyewe) wameshindwa kulielewa hili na sasa wameanza kutafuta mtu wa kumlaumu kwa hili.


Ningemshauri tu achukue muda kujifikiria. Ashughulikie ushauri anaopewa na watu kama Jokakuu, Mkandara na wengine hapa jamvini. Aangalia kila anachotamka na aendelee kujifunza kujishusha na kufanya kazi na wenzie.

Otherwise, anakoelekea ........ sijui tu.

Du....

Nadhani hapo ndipo utakapong'amua umuhimu wa mimi kutoa maoni yangu juu ya Zitto kama nifanyavvyo. Maana najua nikumacha ajibu yeye tu hamchelewi kumgeuzia na akiacha kujibu basi ni wengi watakuja na mitizamo kama ya jama mmoja katika threaad hii kuwa Zitto alihongwa Bil 3 na DOWANS na amepewa nyumba MASAKI.....na mengine mengi ambayo baadhi na wewe unashiriki kuyatengeneza na kuyasambaza...

Zitto tafadhali nitumie angalao kadola mia kutoka katika hayo mabilioni unayopewa kila kukicha.....pleaseeee na mimi labda nitanunua PRADO latest model...chonde kaka....
 
Mwenzio nilimaliza na kupata among the highest GPA's na hata kuwa na uwezo ulikubalika kukufundisha wewe sasa sijui wewe kama unaweza kutoa ushahidi wowote wa hata kumaliza masomo yako pale UDSM. We subiri tu kule unapokwenda wakudai degree yako unayojidai uliipata pale mlimani wakati haipo.....

Mhh,

mashindano ya elimu vs GPA vs what am I talking about

Siyo, Sullivan tu na mikutano mingine mingi tu katika mabara matatu ya dunia hii ambayo kwa faida yako na wengine wa aina yako ninaambatanisha sehemu ya CV yangu hapa. Sijui nawe unayo maana ukitengeneza majungu na majigambo hapo CHADEMA sijui kama kuna lingine ulilofanikisha. Ofcourse ukitoa maslahi ya tumbo....



Hayo ya majungu ni rahisi wewe kuamini kwani ndio dira ya maisha yako hivyo sina haja hata ya kukujibu.

Sijui msimamo wa Zitto kwenye hili ni upi?!

Ningekuwa nampotisha angekuwa mbunge mashuhuri Tanzania kwa asilimia 25% ya sample ya watanzania na hata kujulikana kote Africa na pande zingine za dunia.

Naona hii 25% inawapa kichwa sana kama ile 95% ya umaarufu wa Kikwete.

Unadhani Zitto ni kilaza kama wewe eti atakuwa anapotoshwa na watu kama unavyompotosha bosi wako.

Unadhani siasa ni chama na bila ya chama hakuna kufanya siasa. Sio kila mtu anatawaliwa na ndoto ya kuwa mheshimiwa kama ulivyo wewe hata kufikia kujikweza kama vile wewe ndiye mfadhili mkuu wa CHADEMA. Wengine what matters ni significance ya tuyafanyayo bila kujali kuwa fulani.

Ongea kuhusu viroja

This shows how oppurtunistic u are.......Sishangai kwani mpo wengi wa aina yako ambao kwenu kazi ya foreign ndio mwisho wa ndoto zako kimaisha....Think big kaka and you will do this country a great favour....

Yaani hiko kitambi na huo uheshimiwa wa kulazimisha tayari umeshakupa jeuri ya kujiona wewe ni mkubwa wangu. Unasahau hata waliokufundisha kuchomekea na kuongea na jamii ukaeleweka.....sasa wameshakuwa wadogo zako..du

Vitambi na kuchomekea ... teh teh teh

Je ninyi mmeondo vinyongo na visasi. Ingekuwa hivyo mngendelea na sumu zenu mnazoendelea kumwaga bila ya mafanikio pamoja na hao "wapiganaji" wenzenu kina Mwakyembe na Mengi.

Well, si ajabu ukaona hivyo maana kwako wewe urafiki is equal to upambe kama ufanyavyo kwa huyo bosi wako unayemjaza chuki na fitina kila kukicha....

Zitto, itabidi ukae pembeni maana inaonekana Omar (anayetumia jina lake halisi) na Kiranja (asiyetumia jina lake halisi) "wanatambuana" kwa vilemba vilivyo.
 
Administrator nashauri baada ya muda mchache uondoe hivi viwavi vyetu kama na hao kina kiranja na mwafrika watakubali ili tusifaidishe wasiohusika...

Natumai by then ujumbe utakuwa umefika kwa wahusika wote...na tukaweza kuendelea na mjadala kama ambavyo REV KISHOKA alitegemea..

Samahani kwa wote niliowakwaza kwa majibu yangu

omarilyas
 
Dada yangu hata kama wewe umaamua kuwa adui wa Zitto, lakini kamwe siwezi kukuvunjia heshima, kama dada yangu (ofcourse mimi mkubwa kako) lakini pia daima natambua mchangu wako huko CHADEMA lakini pia utahi wako wa kuona Tanzania iliyo na demokrasia ya kweli inapatikana.

Dada yangu Omari,

Be my guest, sina tatizo na unachoandika hapa.

Hata hivyo, napenda kukupa tu ushauri, hilo kundi la majungu na fitina la kina kiranja linakupeleka kubaya lakini pia ndio adui wa CHADEMA na sio Omar.

Paranoia at best ..... huyo kiranja na mimi wapi na wapi Omar?

Kuhusu kumsemea Zitto, sidhani kama nimewahi kumsemea isipokuwa bila ya kujali athari zake, kama rafiki ambaye urafiki wetu unajengwa sana kimisimamo, mitizamo, principles na hata itikadi ingawa mwenzangu kidogo amekumbwa na UCHADEMA kiasi fulani, nimekuwa mstari wa mbele kusema yafuatayo,

Moja, yale ambayo kutokana na nafasi yake kiuongozi na maslahi ya kichama, Zitto anashindwa kuyasema hapa hivyo wewe na wenzako kwa kutumia vivuli vyenu mmekuwa mstari wa mbele kujaribu kumsemea mambo ya uongo na fitina.

Pili, naamini kuwa ni wajibu wangu kumuelezea Zitto kwa jinsi nimjuavyo mimi ili kubatilisha sumu na majungu yenu mayopenda kuyamwaga hapa wakati mwengine kwa kushirikiana na haohao mnaojigamba kuwa ni adui zenu.

Je, yale uliyoyasema kuhusu chadema na viongozi wake ilikuwa ni kwa niaba ya Zitto?

Tatu, naamini kazi na style ya uongozi na siasa anayotumia Zitto inalenga zaidi maslahi ya taifa zaidi ya chama hivyo naamini nina wajibu wa kumsaidia katika kufanikisha mengi ambayo naamini ni kwa faida ya Tanzananjema niiotayo kila siku....

wasalam....

Hiyo ni imani yako so mimi sina tatizo nayo. Kwa muda mrefu hata mimi nilidhani kuwa Zitto anatetea masilahi ya taifa. Kwa miaka zaidi ya mitatu nimekuwa upande wa Zitto - soma maandishi yangu ya nyuma hapa JF.

Haya yote yalibadilika pale niliposimama (stop) na kunusa kahawa (smell the coffee) ya mienendo ya Zitto. Hint -- issue ya buzwagi imeishia wapi?
 
Wakuuu zangu forget all the crap huyu ndiye Zitto mwakilishi wetu...

Nikiwa Mjini Mugumu Serengeti katika ziara ya kikazi ya viongozi wote wa CHADEMA katika kujenga chama chetu, ninapata taarifa ya mkutano wa waandishi wa habari ambao Katibu Mwenezi wa CCM ndugu Kapteni John Chiligati amekanusha kwamba nchi imekosa mwelekeo. Alikuwa akijibu hoja ya Mwenyekiti wa CHADEMA ndugu Freeman Mbowe kwamba kwa hali ya sasa ya nchi Rais Jakaya Mrisho Kikwete hapaswi kupewa kipindi cha pili cha utawala. Chiligati anasema nchi imetulia, ni shwari kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Chiligati aling'aka na kuanza kutoa matusi yasiomithilika dhidi ya ndugu Mbowe kana kwamba ndugu Mbowe alimtukana ndugu Kikwete. Mbowe hakumtukana Rais Kikwete. Mbowe alisema Uongozi umemwelemea Kikwete na hivyo asipewe kipindi kingine cha uongozi.

Nilikaa na kutafakari kwa kina sana kwa nini Chiligati amesema maneno ambayo hayaendani na taswira yake kama mtu mpole na mwungana? Mimi ninamwona Chiligati hivyo. Sikumjua kabla sijawa Mbunge, nimemjulia Bungeni tena baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, wakati huo wizara hiyo ilikuwa imebakia na vitengo vya Magereza, Uhamiaji na Zimamoto. Haikuwa Wizara kubwa sana, lakini wizara muhimu kwa usalama wa nchi. Nilimwona ni mtu mwungana, alikuwa akishirikiana kwa karibu sana Waziri wetu kivuli katika Wizara hiyo ndugu Mhonga Ruhwanya. Nilishangazwa sana alipoamua kutoka kwenye hoja na kuamua kumtukana ndugu Mbowe!

CHADEMA imezindua kampeni maalumu ya kuimarisha chama katika maeneo ya vijijini. Operesheni hii tumeiita ‘OPERESHENI SANGARA'. Kwa nini Sangara? Kwa kweli wala hatukufikiria kwa kina sana kuna nini katika jina hilo, tuliamua kutafuta kitu kinachowaunganisha wananchi wa mikoa ya Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mwanza na Mara. Tulitafuta kitu ambacho kinahusiana na maisha ya wananchi ya kila siku. Tukakuta Sangara ni jina murua kwani ni samaki alie katika ziwa Viktoria na ni samaki ambae analiingiza Taifa mapato mengi sana. Takwimu za Hali ya Uchumi wa Taifa zinaonesha kuwa Samaki wa Ziwa Viktoria wanachangia takriban asilimia 8 ya mauzo yetu nje ya nchi. Thamani ya mauzo ya samaki kutoka Ziwa Viktoria ni karibia Tshs. 150 Bilioni kwa mwaka. Hata hivyo sehemu kubwa ya fedha hizi zinabaki kwa wawekezaji wachache na Taifa halipati kiasi kinachostahili cha mapato yake kutokana na utajiri huu. Vilevile wananchi wanalalamika kuwa kitoweo cha samaki kimekuwa ghali sana kufuatia samaki wote kuuzwa nje na wao kubakia na Mapanki. Jina hili lilitosha kuwa sehemu ya kampeni ya uimarishaji wa chama katika Kanda ya Ziwa Viktoria.

Nimepata fursa ya kutembelea majimbo yote ya Mkoa wa Mara isipokuwa Jimbo la Musoma Vijijini. Musoma Vijijini nimewahi kwenda; Butiama katika misa ya Baba wa Taifa kwa mwaliko maalumu wa Mbunge wa Jimbo hilo na Buhemba kwa ziara ya Kamati ya Rais kuhusu Mikataba ya Madini. Ninaamini kabla hatujaenda Mkoa wa Mwanza kuendelea na Operesheni mnamo tarehe 11 Novemba, tutapata fursa ya kupita katika Jimbo la Musoma Vijijini ili kuongea na wananchi na kuimarisha chama chetu cha CHADEMA.

Ziara hii imenifumbua macho ya maisha ya Watanzania. Nilipomsikia Chiligati anasema hali ni shwari, kisha nikaangalia maisha ya wananchi wa Buhare (Musoma Mjini), Bukura (Rorya), Nyanungu (Tarime), Muriba (Tarime), Nansimo (Mwibara), Hunyari (Bunda) na Nyamuswa (Bunda), nikasema kweli viongozi wetu hawapo na wananchi (out of touch). Nikachunguza mara ya mwisho ndugu Chiligati alikwenda kutembelea wananchi wa vijijini lini toka amekuwa Katibu Mwenezi wa CCM, nikapata taarifa kuwa hajawahi hata siku moja. Nikathibitisha kuwa sio tu Chiligati alipaniki ‘panick' bali yeye na wenzake wapo ‘out of touch'! Wanajifungia katika maofisi yao yenye viyoyozi Dar es Salaam na kuitisha ‘press conferences' na kusema nchi ipo shwari.

Hali ya nchi sio nzuri hata kidogo, nitatumia mifano halisi niliyoiona katika vijiji vya mkoa wa Mara na kuihusanisha na takwimu za Serikali kujenga hoja zangu kwamba CCM imeshindwa kuongoza Taifa letu, imebaki inatawala na ndio maana wao wenyewe wanapenda kujiita ‘Chama Tawala'. Kwa maoni yangu, hatupaswi kuruhusu CCM kutimiza nusu karne katika Utawala, kwani mwaka 2011 tunatimiza miaka 50 ya Uhuru wa upande mmoja wa Taifa letu (Tanzania Bara). Wazalendo wote wa Taifa hili wanapaswa kujiandaa na kuizuia CCM kutufikisha nusu karne kwani kwa hali ya sasa CCM ni hatari kwa usalama na ustawi wa Taifa letu. Nitajieleza!

Mwaka 2005, wakati wa Kampeni za Uchaguzi CCM waliahidi katika Ilani yao ya uchaguzi kuwa ifikapo mwaka 2010 watakuwa wamepunguza umasikini wa Watanzania kutoka asilimia 38 ya Watanzania mpaka asilimia 19. Mwaka 2005 kulikuwa kuna Watanzania Masikini takribani milioni 11. Hapa tafsiri ya Masikini ni wale watu wote ambao kipato chao kwa mwezi ni chini ya shs 14,000, yaani chini ya sh 400 kwa siku. Hiki ni kiwango cha chini sana kwani kufuatia kupanda bei kwa bidhaa na hasa chakula, hata mwenye kipato cha shs 30,000 kwa siku bado ni mtu masikini tu.

Mnamo tarehe 3 Oktoba, Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo alitangaza takwimu mpya za hali ya Umasikini nchini. Takwimu hizo zimefuatia utafiti uliofanywa na Ofisi ya Takwimu nchini na utafiti huo unaitwa kwa kimombo ‘Household Budget Survey'. Takwimu hizi mpya zinaonesha kuwa Watanzania walio masikini wa kutupwa sasa wamefikia Milioni 12.7. Hii inaonesha kuwa Serikali ya CCM ya awamu ya nne katika kipindi cha miaka 3 ya utawala wake badala ya kupunguza umasikini miongoni mwa Watanzania, imeongeza masikini zaidi ya Milioni 1. Hii imetokana na ukweli kwamba chama hiki kimekuwa ‘nzee', kimechoka na hakina mawazo mapya. Chama hiki tukikiacha madarakani, tena kikiwa na ukiritimba wa Bunge ambao hivi sasa CCM inao, kitaingiza watu wengi zaidi katika dimbwi la umasikini.

Njia mojawapo ya kuokoa Taifa letu, ni kutoruhusu CCM kuuunda serikali tena ifikapo mwaka 2010. Ikitokea hivyo, basi CCM isiwe na ukiritimba Bungeni kama ilivyo sasa ambapo asilimia 86 ya wabunge wanatoka chama hicho kimoja. Hii ndio mantiki ya Mbowe kusema tusimruhusu JK kuchukua muhula wa pili. Mbowe hakuwa na maana ya Kikwete kama mtu binafsi bali CCM. Kwani ikiwa ni suala la Kikwete kama mtu binafsi, CCM watabadili mtu na hivyo kuendelea kutawala. Tunachosema, CCM ya awamu ya nne haistahili kupewa muhula wa pili kwani wamechoka na hawana mawazo mapya ya kuondoa umasikini wa Watanzania.

CCM ya sasa haina idara ya sera wala utafiti na hivyo, hawaongozi tena sera za serikali wanayoongoza bali wanategemea serikali kutengeneza sera na wao wanazikariri katika ilani zao. Lengo la kupunguza umasikini kutoka asilimia 38 mpaka asilimia 19, lilikuwa lengo la MKUKUTA ambapo CCM kwa kutaka kura tu, waliamua kukariri MKUKUTA na kuuweka katika kitabu cha kijani na kicha kuiita ilani.

Watu wa Gazeti la The Economist waliwahi kuita ilani ya CCM kuwa ni ‘wishlist'. Sasa imedhirika kuwa lengo hili kubwa la kupunguza umasikini, limeshindikana. CCM wataweza nini?
Leo CCM imetengeneza mataifa mawili ndani ya Taifa moja la Tanzania. Hivi sasa kuna Taifa la Masikini na Taifa la Matajiri. Masikini wana shule zao zinazoitwa Sekondari za Kata. Matajiri wana shule zao zinazoitwa ‘Academies au English Medium'. Watoto wa masikini katika Sekondari za Kata wanasoma katika mazingira magumu sana. Shule hazina walimu, madarasa hayana madirisha na hata vitabu hakuna.

Nilipokuwa Wilaya ya Rorya nilitembelea Kata ya Bukura. Pale Bukura nilipata bahati ya kutembelea shule ya Kata na kuzungumza na wanafunzi. Shule hii inayoitwa Shule ya Sekondari ya Bukura ina kidato cha Kwanza na cha pili. Shule ya Sekondari Bukura ina Walimu 4 tu na wanafunzi waliniambia walimu wote ni wa masomo ya sanaa. Hakuna Mwalimu wa Sayansi. Shule ya Sekondari Bukura haina uhakika kama mwakani wataweza kuingiza kidato cha kwanza kwani wao wamejenga madarasa mpaka uwezo wao, lakini msingi wa darasa la kidato cha tatu bado upo chini kabisa. Hawana msaada wa serikali.

Nimejionea madarasa ambayo hayana madirisha wala milango. Kuna watoto wanatembea kilometa nane kufika shule na matokeo yake katika kipindi cha mwaka huu peke yake, watoto wa kike 5 walipata uja uzito.

Wanafunzi wa Bukura, wanaonekana ni wenye akili sana, waliniambia kwa nini vyama vya siasa tunapewa ruzuku badala ya ruzuku hiyo kujenga miundombinu ya shule zao. Niliwaeleza umuhimu wa vyama vya siasa katika uongozi wa nchi. Nikawaambia lazima vyama viendeshwe na bila ruzuku matajiri wachache watamiliki vyama. Wakaniambia mbona tayari vyama vimeshikwa na matajiri? Wakanisuta na kuniambia mbona ninyi wabunge hamshindi bila kutoa takrima? Wakaniambia mbona wameona rushwa katika uchaguzi wa viongozi wa CCM katika ngazi ya Kata na Tawi?

Niliwaangalia watoto wale na kukumbuka takwimu za serikali kuhusu elimu. Kwamba hivi sasa kila mwalimu mmoja anafundisha watoto 65 (Rejea PHDR 2007), kwamba watoto 20 wanachangia kitabu kimoja shuleni, kwamba wakati uandikishaji wa watoto umeongezeka na kuvuka malengo ya MKUKUTA, hakuna ufuatiliaji kujua watoto wanasoma nini shuleni. Kata ya Bukura yenye vijiji vya Nyambori, Bwiri, Thabache na Bubombi wananchi wake wanaweza kusema kweli hali nchini ni shwari wakati watoto wao hawapati elimu wanayostahili kama Raia wa Taifa Huru? Hivi Chiligati alipokuwa anamtukana Mbowe kuwa ni muhuni alikuwa anaelezea kadhia hii ya Elimu?

Lakini Chiligati anajua fika kwamba, fedha zilizoibwa Benki Kuu kwa akaunti ya EPA peke yake zingeweza kujenga madarasa 24,000. Madarasa 24,000 ni sawa na madarasa 2 kila Kijiji maana Tanzania ina vijiji 12,000. Hivyo kama mafisadi wasingefisadi fedha hizi, watoto wa Bukura wasingekuwa wanamlalamikia Mbunge wa Kigoma Kaskazini kuhusiana na vyumba vya madarasa. Kama fedha za EPA zingejenga vyumba za Walimu, zingejenga nyumba 19,000. Lakini CCM iliona ni bora ichukue michango ya watu waliokwapua fedha za EPA ili wanunue fulana na kofia za kampeni kuliko kutunza fedha hizi ziweze kujenga mashule.

Chiligati anasema nchi ipo shwari, itakuwaje shwari wakati Serikali ya CCM imeshindwa kutunza hazina yetu? Kama wameshindwa kuaminika kwa hazina yetu na kupata tamaa kuchota fedha za kampeni zao 2005, tuwaamini kweli waendelee kuangalia hazina yetu mpaka 2015? Tunaposema wasipewe miaka mingine 5 tuna maana kuwa CCM haiaminiki tena kutunza fedha zetu za kodi. Hawana ujasiri wa kutochota kidogo waende kupigia kampeni.

CCM na viongozi wake hawajui kuwa kila saa inayopita kuna mwanamke mmoja wa Tanzania anafariki dunia kwa matatizo ya uzazi (Maternal Mortality). Taarifa ya Hali ya umasikini nchini ya mwaka 2007, inaonesha kuwa katika kila Watanzania wanawake 100,000, wanawake 578 wanapoteza maisha kwa ukosefu wa huduma nzuri za afya kwa kina mama. Hii ni sawa na kupoteza Mtanzania mwanamke 1 kila saa. Miaka 47 baada ya uhuru, tunashindwa kulinda afya ya kina mama zetu! Tunajiita Taifa huru na kwamba Taifa hili halina matatizo. Lazima Chiligati anaota! Haiwezekani hali ya Taifa ikawa nzuri ilhali tunapoteza mwanamke mmoja kila saa kwa matatizo ya uzazi.

CCM kwa uchovu wake imeshindwa kuona ya kwamba kuna chumi mbili nchini na uchumi mmoja unakua na mwingine umedumaa. Uchumi wa mijini (Urban Economy) unakua na kukuzwa na sekta za madini, ujenzi, mawasiliano na utalii. Sekta hizi ndizo sekta zinazokua kwa kasi ikiwemo pia sekta ya fedha kama mabenki na bima. Wenye kushika sekta hizi ni matajiri wenye fedha. Kwao hali ya uchumi ni shwari sana.

Uchumi wa Vijijini (Rurak Economy) umedumaa. Uchumi huu unaendeshwa na sekta ya Kilimo ambacho ukuaji wake umebakia asilimia 4 tu kwa takribani miaka 3. Hivyo watu wa vijijini hali zao zimekuwa mbaya sana kwani wanauza bidhaa zao kwa bei za vijijini na wananunua bidhaa kama mafuta, sukari nk kwa bei za mijini. Hivyo wananchi wa vijijini wanapigwa kweli kweli na maisha. Serikali ya CCM labda inashindwa kuelewa kuwa baada ya Ndugu Benjamin Mkapa kujenga misingi imara ya uchumi mkubwa (macro) , hii ya Ndugu Kikwete ilipaswa kutafsiri uimara wa misingi hii kwa maisha ya wananchi wa kawaida wanaotegemea kilimo.

Nilitaraji hii ndio ilikuwa kazi ya msingi ya serikali ya CCM ya awamu ya nne. Imeshindikana miaka 3 ndani ya utawala. Ndio maana tunasema hawastahili kupewa kipindi kingine. Kwa kweli kama chama upinzani, hatuna lingine la kusema. Nchi imekosa mwelekeo.

Wiki ijayo....... Rushwa, Madini, Uaminifu na uchambuzi zaidi wa umasikini.
 
Hint -- issue ya buzwagi imeishia wapi?

Ulitaka ifike wapi na ifike kwa namna gani? Je ulitaka zitto afanyaje ili aifikishe huko unakokutaka? Je na wewe umefanya nini ili ufikishe huko? Je unadhani kwa ufinyu wa wabunge wa chama chake ama udhaifu wa kimikakati na sasa kiasasi uliopo huko angeliweza kufikisha hapo ullipotaka wewe?
 
Back
Top Bottom