Defining, Refining and Understanding Zitto Kabwe

Defining, Refining and Understanding Zitto Kabwe

Kwamba Zitto ana msimamo dhabiti, hilo halina mjadala. Lakini mara nyingine kauli zake zimekuwa zikileta utata sana kwa wanaomsikiliza kijuu juu. Nadhani kisiasa anakosea kama kweli anataka kuaminika na watu wasioelewa. Ila Kisomi huwa-ga yuko sahihi.

Wahanya, nadhani umefika wakati sasa kwa nchi yetu kuchanganya siasa na elimu kama tunataka maendeleo ya kweli. kwa miaka mingi sana tumekuwa tunaendesha nchi kisiasa tu, na matokeo yake ndo hayo ma-ufisadi, mikataba mibovu, n.k. kwa kweli sasa tunahitaji watu wenye elimu ya kutosha pamoja na mwamko wa kisiasa ili tuweze kusonga mbele. Tuna rasilimali nyingi sana za kutufanya tusonge mbele, what we lack is good institutions.
kwenye makaratasi we really have good institutions, lakini watendaji wake je? ndo hao 100% politicians, hata hawajui wanatakiwa kufanya nini kwenye positions zao
 
Rev. Kishoka, hii topic haina uzito wowote,
tukianza kumjadili Zitto tunaweza kumshusha
kisiasa au bado kuendelea kushusha CHADEMA ambacho
ni chama mbadala hapa nchini.

Zitto kuna mazuri amefanya lakini kuna mabaya amefanya
kama binadamu. Lakini kwa kuwa huyu mtu bado yuko CHADEMA tukianza kuchambuana hapa tutakuwa hatuwatendei
haki CHADEMA na yeye pia.

Cha muhimu badala ya kuleta hii topic ya Mh. Zitto tungeongelea
Serikali/Mafisadi wanatumia wanasiasa kuharibu upinzani, lakini simsemei Mh. Zitto.
 
Mkuu naomba nitofautiane na wewe hapa. Zitto ninaye mfahamu mm tangia tukiwa naye pale UDSM, hicho ulicho kisema hakimhusu au si hulka /tabia yake kabisa. Zitto anamisimamo thabiti sana kwenye mambo anayoyaamini yeye kwamba ni sahihi, huwezi kumyumbisha kwenye suala hili, na huwa hayupo tayari kubadili msimamo wake labda sir. God ashuke duniani! Mfano...Sakata la viongozi wa DARUSO....miaka hiyo -kutokana na kutokubali kwake kusurrender, ilipelekea yeye na baadhi ya wenzio kusimamishwa masomo, pili Sakata la Buzwagi...u all know what happaned, tatu....issue ya HOVYO HOVYO, kila mmoja anajua, Issue ya DOWANS....etc just to mention machache!

Yes, Wilcard hapa tupo pamoja......hii ni mmoja wapo ya kasoro za mheshimiwa..... he needs to do something here!


Mkuu Next Level mimi simfahamu zitto sana ila kwa hii issue ya Dorwans nimeona hana msimamo kabisa maana mara iuzwe baada ya wananchi kuja juu angaangalia nitoke vipi akaja tena na kuitaifisha
 
Kwangu mimi, Zitto ni kijana, msomi na mtaaluma kuliko mwanasiasa. Bado yupo katika nafasi ya kutambaa kama mtoto anavyotambaa!

Je kauli zake zinaeleweka au kuaminika? Majibu ni ndiyo na hapana. Ndiyo kwa maana huongea bila kufikiria Kisiasa na Hapana kwa kuwa majibu na kauli zake huleta mgongano wa hisia au kiitikadi na hivyo kufanya wasifu na taswira ya Zitto isieleweke.

Rev. Kishoka,
  1. Zitto sio msomi ila ameelimika. Mtu akiwa na degree moja hawi msomi kwani huo ndio (mwanzo - undergraduate) wa kuelekea kwenye usomi (graduate school, postgraduate degree n.k.).
  2. Zitto kama hatabadilika, basi anaelekea kuwa nia njema sana kwa taifa, kwenye mengi anayoongelea na kufanya, lakini uelewa wake ni mdogo na halielewi hilo. Tatizo kubwa zaidi ni kuwa amezungukwa na wasioelewa zaidi kuliko yeye kwa hiyo kunakuwa hakuna wa kumkosoa kabla ya kuropoka.
  3. Umaarufu aliopata nafikiri nao umeanza kumharibu (kumwingia kichwani), kwani unamfanya asiombe ushauri na anafikiria kuwa anajua sana na pia ana uwezo mkuwba kumbe haelewi ni kwa kiasi gani haelewi.
Ushauri wangu kwa Zitto;
  1. Aende shule (ulaya au marekani) na asome kwa bidii kuelewa yanayofundishwa na sio kwa ajili tu ya kufaulu. Sijui alivyosoma UDSM, lakini nina wasiwasi hakuwa makini sana.
  2. Pia anapoishi huko (ulay au marekani), atajifunza mengi ambayo hayafundishwi darasani na ni muhimu katika kuirekebisha nchi yetu.
  3. Sio vibaya pia akafanya kazi ya kuajiriwa, biashara au vyote. Humo atajifunza sana uongozi na ubora/ubaya wa maamuzi afanyayo.
  4. Aoe.
 
Zitto ni msomi mwenye upeo mkubwa sana. Uwepo wake katika siasa za Tanzania ( Bungeni ) umeleta mwelekeo mpya wa uendeshaji wa bunge letu na siasa kwa kitaifa kwa ujumla wake.

Kama binadamu ana mapungufu yake, lakini by far mapungufu yana out-weigh mazuri.

Sakata la mikataba ya madini, ufisadi na hata kuanguka kwa serikali nzima (Richmond-gate) kote huko kna mkono wa Zitto.

Jamaa kwa umri wake na hata elimu yake amefanya makubwa sana kwenye siasa zetu kuliko akina Mzindakaya ambao tuna wasikia toka tukiwa wadogo, tunasoma na mpaka tu watu wazima. Wengine kwenye mabenchi yao bungeni kuna vishimo kwa kupiga makofi kuunga mkono miswada mbalimbali ya serikali.

Hakuna ubaya kutoa criticism kwani kwa namna bora kunamjenga na kumsadia mlengwa, lakini wengine mnakuwa critical kwa minajili ya kumkatisha mtu tamaa kwa sababu tu ya msimamo wake fulani ambao kwa namna moja au nyingine mtu haukumfurahisha. Nitoe mifano miwili ya haraka; suala la Zitto kugombea uenyekiti Chadema na yaliyojiri kutokana na hatua hiyo yameacha makovu kwa baadhi ya watu, lakini we need to get over it and move on. Whether it was bad move or good one let by gone be by gone. La pili suala la Dowans, hili limewagawa watu ( hususan washabiki/wenye mapenzi na Zitto ) kwenye mapande mawili. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa katika hili Zitto kaweka msimamo wake tena very firm na if anything jamaa ndio kiongozi pekee alie wa face watanzania na kuwaeleza nini kifanyike kuliko hata hao wenye dhamana waliojifungia ndani na kushindwa kusema kitu. Haikuwa nia yangu kuleta mjadala wa Dowans hapa, lakini ninachotaka kusema Zitto ni zaidi ya Uenyekiti wa Chadema na Dowans, ana potential kubwa sana kwa taifa apewe ushirikiano sio kukatishwa tamaa na kama kuna criticism then basi ziwe constructive one.
 
Maadam yupo Chadema, basi ana kasoro kadhaa, licha ya wewe kujitahidi kumpamba!


Kasoro ya mtu kuwa CHADEMA (Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo) ni ipi hata useme eti Zito anakasoro kwa sababu tu yuko CHADEMA.

Besides Zito ni mmoja kati ya viongozi walioko CHADEMA waliobeba neema ya kesho kwa Tanzania. Binafsi kama kijana huwa nafatilia sana shughuli zake hasa za kisiasa na huwa najifunza mengi ya maana kutoka kwa Zito. Mungu mbariki Zito, Mungu ibariki Tanzania.
 
hata mie bado najaribu kumuelewa labda iko siku nitamwelewa zaidi
all the best bwana zitto
 
We all make mistakes. Ninamuomba Zitto to leave his eyes wide open and build his confidence with humility. Yes, he might be very creative with the highest form of authority in what he wants to achieve. But he also needs people around him of all ages in order to build a balanced base of supporters.
Consultations kwenye mambo anayofanya ni muhimu sana, especially ndani ya chama chake ili isionekane ni Zitto kama Zitto mwanasiasa mbobea. Humility in combination with the talents and the credentials he has will enable him to stay longer in the politics of TZ.Maana tusijisahau kuwa kila anayependa kujikweza, huwa anashushwa na anayedhauriwa ndio anakweza.Ili uwe kiongozi imara ni lazima uwe na followers hata kama una uwezo kiasi gani.
 
Heading ya kiingeleza, habari ya kiswahili, Hacheni hizo!!!!.
 
Maadam yupo Chadema, basi ana kasoro kadhaa, licha ya wewe kujitahidi kumpamba!

Jitahidi kumwelewa ndugu yetu huyu. Hii ndio POLITICAL PSYCH ya Zanzibar. Ni kama huku Tanganyika inapokuja masuala ya dini. Muislamu anamuona anayefuata dini ya kikristo ana kasoro, na Mkristo naye anamuona anayefuata dini ya kiislamu ana kasoro...Laima tukumbuke kuwa haya yote yanajengwa na historia (ya kkweli na ya kupotoshwa) na pia maslahi ya kijamii....

Tunapopata changamoto kama za aina ya siasa anazofanya Zitto ni wazi tutaweza kubadilika kidogokidogo...

omarilyas
 
Zitto ni Mwanafalsafa ambaye ameingia kwenye siasa kwa ajili ya kutetea maslahi ya Watanzania,ndio maana siku zote amekuwa akitetea anachokiamini hata kama atapingwa na Watanzania wote,ninaamini kama ilivyokawaida ya wanafalsafa siku moja baada ya kumaliza kazi aliyotumwa na watanzania atarudi kwenye shughuli zake za kifalsafa.

Naamini ulikuwa na maana Zitto ni mwanaharakati?

Omarilyas
 
Sisi kama jamii, tuna nafasi nzuri sana kujijenga upya kuliko walivykuwa babu, baba na kaka zetu.

Nafasi ya sisi kushiriki katika kujijenga ni pamoja na kubainisha walioko kati yetu ambao tunaweza kukua nao na kuwajenga wakawa viongozi wetu.

Vizazi vilivyopita vilikuwa na mapengo mengi. Nyerere alikuwa peke yake, lakiin Zitto hayuko pekee yake, yupo pamoja nasi na sisi tunashirikiana nae pamoja na tofauti zetu za kiitikadi na kisisasa kwa dhamiri moja ya kulijenga Taifa la Watanzania.

FMES kasema Zitto yupo mbele sana ya watu wake anaowaongoza, Mkandara angesema ni Watu na Mazingira, lakini mimi nasema, sisi tupo pamoja katika upeo na upepo mmoja na Zitto ikiwa tu, tutakubaliana kuwa tuna tofauti kati yetu ambazo ndizo zinazojenga mfumo na jamii iliyo huru na yenye afya.

Mfumo butu na bapa ambao hulazimisha watu wote wakawa na nadharia na matazamo mmoja bila kuwa na tofauti, haufai na hauna afya.

Kuna aliyedai kuwa maada hii haitamjenga Zitto, bali ni ya kumfanyia unyama, mimi nasema hilo si kweli. Kama mtu ana dhamiri mbaya, basi ndiye utayaona maandiko na kauli zake kuwa haziko kujenga bali kubomoa.

Sisi kama Taifa tunahitaji kuwa na vichipukizi vipya vya kisiasa na kiutendaji. Ndio wote hapa tupo kwenye mfumo ambao hatuukubali au haufanani na matakwa yetu, na ndio maana tunaanza kujijenga kwa kuanza kutuafuta mfumo bora utakaotufaa sote.

Zitto ni kiongozi mzuri, ni muwazi na mkweli na hata kama maamuzi na kauli zake zinaweza kuwa si sahihi kisiasa, lakini tunajua ukweli kutokana na kupima kauli zake.

Mfano wa suala la Dowans, ukuliangalia kwa utendaji na ufanisi na kuondoa usiasa na hisia mbaya zilizojijenga za kuwepo kwa Dowans, utabaini kuwa Zitto alikuwa sahihi pale aliposema Tanesco inunue mitambo na ijizalishie umeme kwa kutumia mitambo hiyo. Swali ni je Zitto alishaona mbali shida ya umeme inayokuja ambayo ndio imetukaba koo sasa hivi kiasi tunaingia gharama marudufu kwa kutumia IPTL?

Ukiondoa hasira zetu kwa Richmond na Dowans, sioni kama kuna tatizo lolote kwa TANESCO kununua au kutaifisha hiyo mitambo ambayo ililetwa kutuzalishia umeme na tayari kama nchi tumeshaingia gharama kubwa kwa kukosa umeme na kuingia mkataba.

Sasa kama mitambo ya kutupa umeme iko hapa nchini, imejikalia ikipata vumbi, kwa nini tusiwe weevu na kuifanyia kazi alimradi tutafanya kila linalopswa kwa uwazi na kufuata kanuni?

Kwenye suala la Buzwagi, Zitto alijitoa mhanga na akasimamishwa kazi, lakini ikadhihirika baadaye kuwa alikuwa sahihi. Lakini hatuwezi kumlaumu kuhusiana na mapendekezo ya tume kwa kuwa mwenye kutoa uamuzi ni aliyeunda tume na si mjumbe wa tume.

Labda kaam tukisema kuwa hatukuridhishwa na yeye Zitto kuwa kwenye tume ambayo ilikuwa na watu ambao wana madoa na wameliingiza Taifa letu kwenye mkenge kupitia mikataba mibovu.

Kila mmoja wetu ana safari ndefu ya kukua na kukomaa, hata wengine ambao wako CCM, CUF, TLP, NCCR au watu huru, nao wana nafasi sawa ya kukua na kukomaa na kuijenga nchi yetu.

Kiongozi bora na kazi ya kulijenga Taifa la Watanzania si kazi na stahili ya CCM pekee! Ni yetu sote.
 
mchungaji,
kwanza napongeza ulichofanya na kuunga mkono na wanajamii wengi, kuna wakati lazima tuwape moyo viongozi wetu wachache wanaotufanyia kazi nzuri na wenye misimamo yenye tija ili wajua wapo watu wanawasuport na kupata moyo wa kuendelea kufanya wanayofanya.
Zito pamoja na kuwa na mapungufu yake binafsi lakini anastahiri pia kupewa moyo na kuwa kwake hapa JF kunasaidia sana yeye kujilekebisha pale tunapoona amekosea na kueleza ukweli.
mimi ushauri wangu kwake ni kwamba hawezi kufanikiwa akiwa peke yake hata siku moja....
 
Makaayamawe
Zitto sio msomi ila ameelimika. Mtu akiwa na degree moja hawi msomi kwani huo ndio (mwanzo - undergraduate) wa kuelekea kwenye usomi (graduate school, postgraduate degree n.k.).
Aende shule (ulaya au marekani) na asome kwa bidii kuelewa yanayofundishwa na sio kwa ajili tu ya kufaulu. Sijui alivyosoma UDSM, lakini nina wasiwasi hakuwa makini sana.

Pia anapoishi huko (ulay au marekani), atajifunza mengi ambayo hayafundishwi darasani na ni muhimu katika kuirekebisha nchi yetu. Sio vibaya pia akafanya kazi ya kuajiriwa, biashara au vyote. Humo atajifunza sana uongozi na ubora/ubaya wa maamuzi afanyayo.
USOMI- Je tuna maana ya SCHOLAR ama INTELLECTUAL?
Nimjuavyo Zitto ni mtu anayependa sana kujisomea na hivyo kuongeza ujuvi wa mambo. Hii ni tabia ambayo amekuwa nayo tangia miaka mingi pale Mlimani. Kama kuna zawadi anayojua kununua na kuhakikisha anasoma Zitto awapo nje safarini ni vitabu na majarida. Hata ukipitia vitabu vyake utagundua kuwa kilisomwa kwa umakini mkubwa. Ni kweli hivi karibuni nimeshuhudia muamko mpya wa kujisomea miongoni mwa vijana wa rika lake, lakini bado naamini yeye ni mmoja wanasiasa wachache sana wanaojisomea sana…..

KUFUNDISHWA na sio kwa ajili ya kufaulu- Hapa nametetea kwani hata wakati wa enzi za mlimani kama kuna mapungufu aliyokuwa nayo ni kutotilia maanani mitihani yake. Zitto ni mfano wa wanafunzi wachache wanaoenda mlimani kuelimika na sio kutengeneza digree za kupata ajira BOMBA. Kwa hili namtetea asilimia 100%. Angekuwa ni mwanafunzi wa kufaulu tu basi kamwe asingemuona Chachage mwalimu wa SOCIOLOGY kuwa ni mwalimu wake wakati yeye alikuwa akisoma uchumi, Asingemuona Prof Shivji wa LAW, Prof Haroub wa Development Studies amd Dr Lwaitama wa Philosophy kuwa walimu wake wakubwa.....Alilazimika kuwajua na kuwa karibu nao wote hawa na wengineo wang kutokana na kutambua kilichompelek pale UDSM nacho ni kuelemika kwa mapana na marefu.

Nijuavyo Zitto alianza kusafiri nje ya nchi hata kabla hajamaliza chuo kikuu tofauti na ambavyo ilivyo kwa wengi wa watoto wa wakulima na wafanyakazi wa enzi zile kama yeye. Na aienda huko na hadi sasa ni mtu wa kujichanganya kabisa na maisha ya huko na kujisomea sana siasa za huko. Zitto ni mfuatiliaji sana wa mambo yanayoendelea nje ya nchi na bara letu. Ofcourse mengi ni ya masuala ya kisiasa na kiuchumi. Mambo ya kina TI na Rihana hapo utamuacha sana…



WildCard
Buzwagi hakuna alichofanikisha pale. Mkataba umebaki uleule uloosainiwa London. Raisi alipounda ile tume ya Jaji Bomani na yeye akawemo. Wakawa wanalipwa Shs 350000/= kwa siku. Ripoti yao imefanyiwa kazi kiasi gani sijui.
Ni vizuri ukafuatilia kujua nini kinaendelea katika sekta ya madini nchini. Kama unadhani ilikuwa ni busara kung'ang'ania suala la Buzwagi tu na kuacha nafasi ya kushughulikia sekta ya madini yote kwa mapana yake basi ni wazi huwezi ukamuelewa Zitto.

Ni vizuri pia ukajaribu kuuliza mchango wa Zitto katika kamati hiyo. Na pia kujua katika muswada wa sheria ya madini unaozunguka hivi sasa ni mangapi yalitakiwa yafanyika na kamati yamechukuliwa na mangapi hayajachukuliwa na kwa nini? Kiongozi mzuri ni Yule anayetambua majukumu, nguvu na mipaka yake. Kumbuka wao walitakiwa kuchambua sekta na kupeleka maoni yao kwa RAIS. Sasa kama ungependa na wao wajigeuze wabunge wetu ambao wanashindwa kutofautisha nguvu na majukumu yao katika suala la kushauri ama kushurutisha serikali, then hapo utakuwa unawaonea…..



WildCard
Umimi. Anajiimarisha yeye zaidi kuliko chama chake. Hili halitamfikisha popote zaidi ya kupata UMAARUFU. Awaulize akina Mrema waliotumia staili hii walikofikia.

Bongolander
Lakini alivyoiyumbisha Chadema ameonesha kuwa he is somekind of an opportunist and somekind of self centred politician.

Mtu kama huyu akipewa kiti kikubwa anaweza kuburuzwa na kuyumbishwa, au anaweza kufanya mengi ya ajabu ambayo ni unpredictable.
Mimi naomba ufafanuzi wa hii issue ya Zitto kuyumbisha CHADEMA. Hivi ni Zitto ndiye ameyumbisha CHADEMA ama CHADEMA kama asasi ndio kimeyumba kwa kukosa ukomavu? Hivi kati ya Zitto aliyetumia haki yake na utashi wake kisiasa na kichama kuomba ridhaa ya kuwa kiongozi wao na wale waliotumia ………….kumzuia asitumie haki hiyo ni nani aliyumbisha chama. Kwa wale wanaofuatilia mchezo wa Second Chance (ni wa kijinga lakini hata ujinga una mengi ya kuelimisha) wataweza kujua jinsi ya mwanamama REBECA na Yule mwenziwe aliyekuwa Head Butler jinsi walivyokuwa wakilaumu maswahiba yote yanayowakuta ambayo ukweli ni kuwa yalitokana na ujinga, chuki na tamaa zao wenyewe halafu wakiamini kuwa hayo yote yanatokana na kina Salvador na wengineo hapo. Nadhani hii issue ya kumlaumu Zitto kwa kuyumba kwa CHADEMA inaendana na ule mchezo. Tukubali kujikosoa ili tujisahihishe.

Na opportunist ni yupi? Yule aliyetayari hata kutumia siasa chafu za kuvunja chama kwa ajili ya kulinda nafasi yake ama Yule aliyetayari kulaumiwa na kutoeleweka na wafuasi (political base yake) kwa kujitoa katika kinyang'anyiro ili kulinda maslahi/umoja wa chama hata kama wengi hawakuwa tayari kuliona hilo?

Kuhusu umimi kwa kweli hapa mnamuonea kabisa Zitto. Wenye umimi si mnawaona wamefikia hata hatua ya kuhalalisha uozo wa posho mbili/takrima/itifaki ili mradi walinde nafasi na maslahi yao kisiasa. Kwa yeyote anayemjua vizuri Zitto ni wazi atakubaliana na mimi kuwa ubinafsi sio sehemu yake. Zitto nimjuaye mimi ni yule ambaye huona faraja sana kujitoa kwa kusadia wengine kuliko kitu kingine chochote. Ofcourse kwa utanzania wa aina ya usasa, ni vigumu wengi kuamini kama kuna mtu ambaye anapenda kujitolea kusadia wenziwe kwa kile kidogo alichonacho na sio "kujijenga" yeye binafsi...


Na kuhusu CHADEMA, hivi mna uhakika kuwa Zitto hajitolei huko ama mnabeba porojo za kina Mengi na wenzake magazetini? Hivi mnawauliza hao kina…….kutoka CHADEMA kuwa nini mchango wao uliozidi ule wa Zitto mpaka wawe na audacity ya kusema kuwa Zitto ana umimi? Kama umaarufu hivi Zitto alijipa huo umaarufu? Mnataka awamegee kidogo huo umaarufu wake? Fanyeni naye kazi nanyi mtambulike sio kila siku kuwa mstari wa mbele kuhalalisha majungu na uchafu wa hao kina Mwakyembe na wenzake ambao wangependa kuona kuwa kila mwanasiasa nchini atatumia ABCDs zao kisiasa.

Kama CHADEMA wameshindwa kufaidika na umaarufu wa Zitto, kama waonavyo wao, then hilo ni tatizo la Zitto ama la CHAMA? Ni mangapi Zitto ameyaibua huko anapoyaibua ambao wengi wenu hamna hata guts za kufika, na akaishia kuyahakiki na kuwapa viongozi wenzake CHADEMA wayafanyie kazi bila ya yeye kutaka kuwarecognised? Mengineyo mnayakimbia na kuyageuza geuza kwa manufaa binafsi nay a muda mfupi mkiacha kuyatumia ipasavyo. Sasa bado mdai kuwa ana umimi?

Mtanisamehe nimeamua kuyasema haya kwani nimjuavyo Zitto anaweza akaacha huu uzandiki na muono potofu juu yake uendelezwa bila ya yeye kujitetea kwa kutokana na hulka yake ya kutopenda kuonekana anajikweza........
 
Zitto said:
Mfano wa suala la Dowans, ukuliangalia kwa utendaji na ufanisi na kuondoa usiasa na hisia mbaya zilizojijenga za kuwepo kwa Dowans, utabaini kuwa Zitto alikuwa sahihi pale aliposema Tanesco inunue mitambo na ijizalishie umeme kwa kutumia mitambo hiyo. Swali ni je Zitto alishaona mbali shida ya umeme inayokuja ambayo ndio imetukaba koo sasa hivi kiasi tunaingia gharama marudufu kwa kutumia IPTL?

Rev.Kishoka,

..Zitto hakueleza faida, kama zipo, za kununua mitambo chakavu ya Dowans, badala ya mitambo mipya ambayo wabunge wenzake walikuwa wanapendekeza.

..halafu ukiangalia ile statement ya Zitto ni kwamba alikuwa anajaribu kuwabebesha lawama za mgao wa umeme Mzee Shelukindo, na wenzake, ambao walimpinga Zitto na Dr.Rashid kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans.

..binafsi nadhani kitendo kile cha Zitto kilikuwa ni mchezo mchafu sana ambao nisingependa auendekeze.

..serikali na Tanesco walikuwa na muda wa kutosha kushughulikia tatizo la mgao wa umeme. hata Raisi aliwahi kutamka kwamba mitambo ya Dowans haitanunuliwa. sasa kisichoeleweka ni kwamba Tanesco na serikali walikuwa wakifanya nini muda wote mpaka nchi imekumbwa na mgao?

..kama Zitto angekuwa mwanasiasa makini, na mwenye kutetea maslahi ya wananchi, basi angekuwa wakwanza kuwahoji Tanesco na serikali kuhusu hatua wanazochukua/walizochukua kutuepusha na mgao ukizingatia kwamba mitambo ya Dowans were off the table.

..kitu cha kushangaza ni kwamba Zitto amesubiri mgao uanze halafu anatokezea na kudai " I told you so."

..binafsi nadhani badala ya ZITTO kutumia nafasi yake kutafuta suluhisho la matatizo yanayoikabili Tanesco ameishia kuwa a DISTRACTION kutokana na kauli zake zisizo na kipimo.

NB:

..kuna uwezekano Zitto amezungukwa na wapambe[yes men and women] ambao hawamsaidii ktk kupima uzito wa matamshi anayoyatoa.

..vilevile huku mitaani apunguze kutoa matamshi kama yeye Zitto, badala yake azungumzie msimamo wa chama chake.
 
Jokakuu,
Katika swala la Dowans sikumsikia hata kiongozi mmoja wa Chadema akipinga maelezo ya Zitto isipokuwa nadhani Dr. Slaa yeye alipendekeza ombi la Zitto kamati mbili (ya (Mahesabu na ile ya Nishati) zikutane na kujadili swala zima la Dowans akiwa yeye kisha ridhika na maelezo aliyopewa na Dr. Rashid.
Binafsi naamini kabisa Zitto hakuwa akifahamu mchezo alokuwa akichezewa. Toka kuingizwa kwake kamati ya madini na kisha hiyo ya mahesabu..Ukitazama kwa makini serikali imekuwa ikiwachezea Wabunge kwa kuwazungushia kamati ambazo wanavuta kipato zaidi kutokana na Posho.
Mategemeo ya viongozi wa serikali ni kwamba kina Zitto, Shelukindo na wengine wapambanaji watakaa kimya ama kupunguza kelele badala yake hawa watu wamezidi kuongeza nguvu ya mashambulizi. Ndio maana tumeona ujio wa uchunguzi kuhusu Posho mbili kuwakata makali Wapambanaji..

Mkuu Jokakuu, ni afadhali ya Zitto ambaye kila kazi ya kamati yake huiweka hapa na maamuzi hata kama ni yake binafsi hueleza kile alichofikiria yeye kuwa bora kuliko hao wengine na kamati zao hatufahamu kinachoendelea..Tena nadhani kila Zitto anapokuja hewani hupasua nyoyo za Mafisadi kwa sababu hoja hizo mara nyingi ilitakiwa kuwa siri na yafanyike chinichini..

Trust me, kama sii Zitto kuja hapa na kusema mawazo yake ambayo wengi wetu hatukuyapendelea Dowans ingenunuliwa na msingefahamu kilichotokea..Lakini kuja kwake sisi sote tumejifunza na yeye poia kajifunza na kuelewa nini mtazamo wa wananchi ktk swala la mitambo ya Dowans..
 
Nani perfect dunia hii? Nitajie mtu aliye perfect, kutoka chama au dini yoyote duniani. Tujifunze mawasiliano jamani.

Kwenye kiingereza tutasingizia lugha ya kigeni, sawa.Hata kiswahili nacho?

Mwenzio hajui Kiingereza kwa hiyo hata maana ya "perfect" hajui. Kwa hiyo Kibs ni wa kumchukulia hivyo hivyo tu....
 
Rev. Kishoka, hii topic haina uzito wowote,

Cha muhimu badala ya kuleta hii topic ya Mh. Zitto tungeongelea
Serikali/Mafisadi wanatumia wanasiasa kuharibu upinzani, lakini simsemei Mh. Zitto.

Can the tone of this forum change for once or at least once? Kama ni kupiga vita ufisadi, mbona ndio kila siku and matokeo hakuna?

We need to start changing our thinking. We need to think progressively and also redefining ourselves and our future which is at stake.

Sasa hivi mkiambiwa Mafisadi wamejiandaa kwa kutawala miaka mingine 20, ina maana wameshafikiria ya mbeleni na si yaliyoko leo hii!
 
Mwenzio hajui Kiingereza kwa hiyo hata maana ya "perfect" hajui. Kwa hiyo Kibs ni wa kumchukulia hivyo hivyo tu....
Maana yake ni nini? Naona taratibu unaanza kupindisha bandiko
 
Back
Top Bottom