Kwa hii kauli nimemshangaa sana Sarri, kama kiongozi, kama kocha unakiri vipi tena hadharani kwamba huwezi kumfunga opponent wako? Ni motivation gani unayowapa wachezaji wako, kama si kuwakatisha tamaa kwamba hawawezi kumshinda City hata siku moja?
Tena amesema kabisa mara zote 3 walizokutana Guardiola amemfunga, hivyo hajui ni namna gani atamfunga City. Eti ni namna gani atamfunga City waulizwe wengine lakini si yeye.
Dah, ningekuwa shabiki wa Chelsea ningekuwa disappointed sana. Yaani kocha amekubali kufungwa kabla ya mechi haijachezwa