Mkuu
Unafikiri washabiki wenzako wa Mafia team aka Chelsick watakubali? Hapa tupo kwenye burudani ukifungwa una leak your wounds ukishinda unasheherekea. Ligi bado ndefu hadi mwezi May ndio tutafahamu hatma ya Premier League lakini kuna wenzetu walianza kudai hili kombe kuanzia November last year.
Tatizo kubwa la EPL hivi sasa ni marefa kuto kutoa uamuzi wa haki wanapochezesha mfano wa jana Arsenal Ramsey alifanyiwa fujo na refa hakutoa kadi kwenye penalty box na ni mchezaji yule yule aliyemvunja mguu, kama angeonywa au kutolewa kwa red card tungekuwa tunaganga mengine, na leo Aston Villa Vidic alitakiwa kupewa red card lakini aliendelea kucheza hadi mwisho.
Hili naliona kama tatizo kubwa sana. Nilikuwa nafikiri limekwisha hasa baada ya wakati ule miaka michache iliyopita wakati Tottenham Hotspurs walinyimwa goli ambalo liliwasaidia Manure kuchukua ubingwa - Umafia umeingia sana kwenye soka how to clean it ndio big question hivi sasa, kwa sababu there is a lot of money in this sport.