Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,115
Gari lililokuwa linatumika kufanya matangazo (PA) ya mikutano ya Makamu Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu, lenye namba za usajili T 658 DQL limenusurika kuteketea kwa moto usiku huu Chato mkoani Geita baada ya watu wasiojulikana kutaka kufanya jaribio la kulichoma moto likiwa limepaki na magari mengine eneo la Twiga Lodge.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lillifika eneo la tukio na kuzima moto kabla hayajatokea madhara zaidi.
=====
Taarifa za awali, Gari ya matangazo (PA) M4C T 658 DQL niliyotangulia nayo kwaajili ya matangazo imenusurika kuteketea kwa moto baada ya ccm kufanya jaribio la kuichoma kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu usiku huu saa 1:10 Usiku.
Gari husika baada ya kumaliza mkutano uliofanyika Jimbo la Mbogwe jioni niliondoka nalo kuelekea chato na kuanza matangazo baada ya matangazo lilihifadhiwa TWIGA LODGE ambapo yapo magari ya watu tofauti zaidi ya matano (5) yaliohifadhi pia ila yote yako salama isipokuwa M4C ya chama.
Jeshi la zima moto na uokoaji lilifika eneo la tukio na kuzima moto husika kabla hayajatokea madhara zaidi.
Kinachoendelea sasa ni mimi, DJ Othuman na Dreva Ally kutafutwa hapa chato muda huu kila Lodge wanagonga chumba kwa chumba at wakisema ni zamu yetu kuchomwa moto.
Upuuzi huu unafanywa na Dola + Uvccm.
Yohana Kaunya
KM - Bavicha Taifa ,
Chief of staff Team ya Makamu Mwenyekiti chadema (Mhe. Tundu lissu)
Saa 1:30 Usiku (Chato)
02,Augost 2023.
________
Pia soma: Tundu Lissu: Gari yetu ta matangazo imechomwa moto karibu na Chato. Hatutishiki, Mkutano wa Chato utaendelea
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lillifika eneo la tukio na kuzima moto kabla hayajatokea madhara zaidi.
=====
Taarifa za awali, Gari ya matangazo (PA) M4C T 658 DQL niliyotangulia nayo kwaajili ya matangazo imenusurika kuteketea kwa moto baada ya ccm kufanya jaribio la kuichoma kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu usiku huu saa 1:10 Usiku.
Gari husika baada ya kumaliza mkutano uliofanyika Jimbo la Mbogwe jioni niliondoka nalo kuelekea chato na kuanza matangazo baada ya matangazo lilihifadhiwa TWIGA LODGE ambapo yapo magari ya watu tofauti zaidi ya matano (5) yaliohifadhi pia ila yote yako salama isipokuwa M4C ya chama.
Jeshi la zima moto na uokoaji lilifika eneo la tukio na kuzima moto husika kabla hayajatokea madhara zaidi.
Kinachoendelea sasa ni mimi, DJ Othuman na Dreva Ally kutafutwa hapa chato muda huu kila Lodge wanagonga chumba kwa chumba at wakisema ni zamu yetu kuchomwa moto.
Upuuzi huu unafanywa na Dola + Uvccm.
Yohana Kaunya
KM - Bavicha Taifa ,
Chief of staff Team ya Makamu Mwenyekiti chadema (Mhe. Tundu lissu)
Saa 1:30 Usiku (Chato)
02,Augost 2023.
________
Pia soma: Tundu Lissu: Gari yetu ta matangazo imechomwa moto karibu na Chato. Hatutishiki, Mkutano wa Chato utaendelea