Changamkia Fursa Biashara ya Gesi ya CNG inazidi kupamba moto Vituo vya kujaza Gesi ya CNG vinazidi kujengwa

Changamkia Fursa Biashara ya Gesi ya CNG inazidi kupamba moto Vituo vya kujaza Gesi ya CNG vinazidi kujengwa

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
8,988
Reaction score
11,862
Kufikia mwezi wa 4 2025, vituo 10 vya CNG vilianza kujengwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro.

Kampuni ya PUMA Energy Tanzania Limited ilianza kujenga vituo Tegeta, Ubungo External, Mbezi Beach, na Morogoro.

Energo Tanzania Limited ilianza kujenga kituo Mikocheni.

Victoria Service Station Limited inajenga kituo Kipawa.

Rafiki CNG Station ilianza kujenga kituo Tabata Relini.

Tanzania States Natural Gas Holdings Company Limited ilianza kujenga kituo Goba.

Natenergy ilianza kujenga kituo Kigamboni.

Kiwanda cha Kinglion kilianza kujenga kituo cha kupokelea gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG Receiving Facility) Kibaha.

Vituo vilivyo kamilika mpaka sasa ambavyo vinajaza gesi ni Tembo Energy - Tabata, TPDC - Mlimani, TAQA Dalbit - Sam Nujoma, Rafiki CNG Station - Tabata.

Kampuni zinazo safirisha gesi ni Kampuni ya Tan Health Limited.

Kutokana na ongezeko la ujenzi wa vituo vya CNG, unafuu wa gharama unaopatikana katika matumizi ya gesi asilia kama nishati mbadala ya mafuta katika vyombo vya moto na mwamko mkubwa wa wananchi kutumia CNG, idadi ya watumiaji wa gesi hiyo katika vyombo vya moto inatarajiwa kuendelea kuongezeka kwa kasi.

CNG inaweza kutumika kwenye pikipiki, bajaji na magari.
cng-motorcycles-for-greener-rides-in-india.png


images (27).jpeg


images (31).jpeg
 
Kibongobongo gesi bora ikae kwenyw magari. Huku kwenye pikipiki na hawa boda boda vishandu kutwa kuangusha kihasarahasara si maafa yatakuwa makubwa! Na mlipuko wake ni wa KIBABE! Check youtube videos.
 
Je, unahitaji
Mpango wa Biashara wa Kuanzisha Kituo cha Kujaza Gesi Asilia (CNG)?
Yaani: Business Plan for Establishing a CNG Refueling Station

Biashara ya kuanzisha kituo cha kujaza gesi asilia (CNG) nchini Tanzania ni fursa kubwa na ya kipekee, hasa kutokana na mabadiliko ya dunia kuelekea matumizi ya nishati safi, salama, na nafuu. CNG ni mbadala wa petroli na dizeli unaopunguza gharama za uendeshaji wa magari na kutoa mchango mkubwa katika kulinda mazingira kwa kupunguza utoaji wa gesi chafuzi.

Kwa sasa, serikali na sekta binafsi zinawekeza katika miundombinu ya gesi asilia, jambo linaloweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wanaotaka kuanzisha vituo vya CNG. Mahitaji yanatarajiwa kuongezeka sana miongoni mwa:

(i) Magari binafsi yanayobadilishwa kutumia CNG

(ii) Mabasi ya mijini na masafa marefu

(iii) Malori ya usafirishaji mizigo

(iv) Bajaji (ambazo zinatumika sana kwenye usafiri wa mijini)

(v) Pikipiki (hususan bodaboda) ambazo zitakuwa na mfumo wa kutumia gesi asilia


Kupitia mpango wa biashara ulioandaliwa kitaalamu, utapata:

(i) Utafiti wa Soko: Tathmini ya mahitaji ya CNG kwa magari, bajaji, na pikipiki katika miji na mikoa ya Tanzania.

(ii) Makadirio ya Gharama na Mapato: Bajeti ya uanzishaji, gharama za uendeshaji, na makadirio ya faida kwa miaka kadhaa.

(iv) Mkakati wa Masoko: Njia bora za kuvutia wamiliki wa magari, bajaji, na pikipiki kutumia kituo chako.

(v) Uchambuzi wa Hatari na Mikakati ya Kudhibiti: Njia za kupunguza changamoto za kibiashara na kiufundi.

Kumbuka kuwekeza kwenye kituo cha CNG hakutakuletea tu faida ya kifedha, bali pia kutakufanya kuwa sehemu ya suluhisho la kitaifa katika kukuza matumizi ya nishati safi, kupunguza gharama za usafiri, na kulinda mazingira.

Tutafute kupitia mawasiliano yafuatayo:
📱 Piga Simu / WhatsApp: 0687746471 / +255687746471
📱 WhatsApp: 0612607426 / +255612607426
📧 Barua Pepe: bandg.editors@gmail.com / clean.energies.group@gmail.com

#CNG #GesiAsilia #Biashara #BusinessPlan #PetrolStation #GasStation #Energy #CleanEnergy #LPG #NaturalGas #CNGRefueling #TanzaniaBusiness #MpangoWaBiashara #OilAndGas #SustainableEnergy #Uwekezaji #Investment #Bajaji #Pikipiki
 
Back
Top Bottom