Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,651
- 218,131
Kauli hii ya kishujaa imetolewa na Mwamba Mwenyewe Freeman Mbowe alipokuwa anahitimisha mpango wa Operesheni Haki Mkoani Morogoro.
Mbowe ambaye sasa anaitwa Mtemi Isike, baada ya kusimikwa huko Tabora , amesema kwamba Chama chake sasa kinataka viongozi wake wafanye kazi moja tu ambayo ni kusuka chama kwa kukusanya wanachama wapya na kuhudumia wanachama wake 24/7 , hivyo ni lazima wapewe vitita vizito kila mwezi ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Kwa kadri ya kumbukumbu zangu CHADEMA yaweza kuwa ndio Chama cha kwanza cha kisiasa nchini Tanzania kuwalipa wafanyakazi wake wote hadi wa ngazi ya chini kabisa Mshahara, vyama vingine watendaji wake wengi huishi kwa kutegemea RUSHWA ZA WAGOMBEA WAKATI WA CHAGUZI za ndani au Uchaguzi Mkuu.
Mbowe ambaye sasa anaitwa Mtemi Isike, baada ya kusimikwa huko Tabora , amesema kwamba Chama chake sasa kinataka viongozi wake wafanye kazi moja tu ambayo ni kusuka chama kwa kukusanya wanachama wapya na kuhudumia wanachama wake 24/7 , hivyo ni lazima wapewe vitita vizito kila mwezi ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Kwa kadri ya kumbukumbu zangu CHADEMA yaweza kuwa ndio Chama cha kwanza cha kisiasa nchini Tanzania kuwalipa wafanyakazi wake wote hadi wa ngazi ya chini kabisa Mshahara, vyama vingine watendaji wake wengi huishi kwa kutegemea RUSHWA ZA WAGOMBEA WAKATI WA CHAGUZI za ndani au Uchaguzi Mkuu.