Uchaguzi 2020 CASE STUDY - Jimbo la Hai - Walitumia teknolojia gani kupata matokeo sahihi ya kila kituo ndani ya saa 8?

CCM walikuwa na matokeo yao ya mfukoni hata kabla ya kuanza kupiga kura.

Zoezi la kupiga kura ilikuwa ni kuhalalisha uharamia ndani ya Sanduku la kura.

Lakini itawasaidia nini CCM ambao wapo madarakani zaidi ya miaka 60 na bado umaskini umetamalaki kila kona ya nchii hii.

Chama kikongwe eti kipaumbele chake bado ni kupika matokeo ionekane kinakubalika .

Hapo ndiyo kinazidi kujichimbia kaburi.
 
Nikishaelwa aina ya watu kama nyinyi huwa sipendi kujipotezea muda.
Hukutumwa kusoma wala ku comment, ni ujuha wako ndio uliokuleta kwangu.
short, jiheshimu nikuheshimu, sikumtukana wala kumkejeri yoyote yule. Najua na nina thamini maoni ya wote yenye staha.

Hatuwezi wote kufanana. Kuvumiliana ni sehemu ya maisha. Mimi sio mnafiki wa kusifia ujinga hata kama nina uwezo wa kuhoji. Sio muoga, nina tumia kichwa na uwezo niliopewa kutafakari na kuhoji pale panapo hitajika.
 
Unajua sifa ya uchaguzi halali na wa kweli?

Kinacholalamikiwa ni nchi kuongozwa na watu walioingia madarakani kwa HILA na UDANGANYIFU na WIZI WA KURA kwa kutumia uhalali wa hiki kinachoitwa uchaguzi wakati huu ni ujambazi dhidi ya demokrasia..!!
Sawa mkuu.
sasa toa muongozo nini kifanyike? kuanzisha vurugu? kukaa kimya? kuja kulalamika humu jf? Tunahitaji suluhisho lililo sahihi ili kuondoa hizo dhurma na kutenda haki.

Tuamini story zako tu bila kusikiliza wengine? Lazima tu balance story na sehemu pekee ya kutoa haki ni mahakama. Ndio maana nakushauri na kuwashauri wote wanaoweza kusaidia haki ipatikane hata kama wenye mamlaka wapinge, hao watu waende kwa viongozi wetu walionewa ili waidai.
 
Sawa kabisa. Sasa kwanini msikusanye huo ushahidi wote then mkaenda mahakamani. Ni muhimu kutumia huu uzalendo ulionyesha hapa kwa kusema ukweli utumike huko, uwe shahidi upande wa kina mbowe ili wapate haki yao otherwise utaonekana ni mnafiki au unatumiwa tu.

Na hayo yote yanatokea kwanini nyinyi kama wasimamizi na mawakala mnakubari kama sio kushiriki kwenye dhurma? au hujapata mgao wako?

Watu kama nyinyi ni kutia risasi kabisa, maana mnashiriki kuiangamiza nchi.
Mahakama ipi unazungumzia? Kama ni hizi zilizo chini ya Prof. Juma afadhali wafanye mambo mengine.Upumbavu umetamalaki kote kote: si polisi,tume ya uchaguzi,wakurugenzi,dpp wala mahakamani.Msajili wa vyama ndiyo usiseme.EXTREMELY SHIT HOLE CHARACTERS!
 
Bila kudhibitisha/verify utambulisho wako kuwa ni mfanyakazi wa serikali sehemu ipi, namba ya kitambulisho chako, kituo ulichoshiriki kusimamia uchaguzi, mkuu wa usimamizi wa uchaguzi kituoni hapo, barua ya utambulisho kutoka NEC kuwa wewe ni msimamizi halali wa uchaguji; moja kwa moja tunakuweka kwenye kundi la watu waongo na wenye nia mbaya dhidi ya watanzania. Na kwa kweli Vyombo vya usalama vikikupata vikutendee haki yako kwa wewe kutaka kuhatarisha maisha na mali za watanzania.
Ulitaka aweke hayo yote hapa JF?
 
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho.

Ilikuwa kwa vyovyote vile asitangazwe mshindi either by HOOKS or by CROOKS. Hili lilikuwa apizo la Magufuli na wenzake na walilifanya kwa ushamba na ujinga wa viwango vyote vya ujinga duniani.

Kwa waliopoteza kumbukumbu, jimbo la HAI ndilo lilikuwa jimbo la kwanza kutoa matokeo ya uchaguzi takribani masaa yasiyozidi 8 baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa ile saa 10:00 jioni ya tarehe 28/10/2020.

Kwa teknolojia ya uhesabuji kura ktk vituo vya kupigia kura, kujaza fomu mbalimbali, compilation ya matokeo ngazi ya kata na jimbo ili kumpata mshindi wa udiwani na mbunge na kwa kuzingatia jiografia ya majimbo yetu ya uchaguzi yote Tanzania mtu anaweza kuona ugumu wa kuikamilisha kazi hiyo ktk interval ya masaa takribani 9 au 10 tu katika ngazi ya jimbo.

Bahati njema mimi nilikuwa mmoja wa maafisa wa uchaguzi huu nikiwa mwajiriwa ndani ya serikali, nikipewa jukumu hili pia.

Katika eneo nililosimamia mimi, kituo cha mwisho kuleta matokeo wilayani (jimboni) ili kufanya majumuisho kumpata mshindi wa ubunge ilikuwa ni saa 2asb kesho yake yani 29/10/2020!

Kwa kawaida, baada ya kituo cha kupigia kura kufungwa saa 10:00 jioni, uwezekano wa mtu wa mwisho kupiga kura inaweza kuwa kati ya saa 1 hadi 1.30 kutegemea na kituo na idadi ya wapiga waliokuwepo kabla ya saa 10 jioni. Hii maana yake mtu wa mwisho alipiga kura saa 11:30jioni kabla ya kuanza kuhesabu..

Kuna vituo vingine zoezi la kuhesabu kura, kubishana na mawakala na kutatua migogoro inayojitokeza na kujaza fomu mbalimbali ikiwemo ya taarifa ya kituo lilikwenda hadi saa 4usiku..

Baada ya hapo kwa kawaida msimamizi wa kituo cha kupigia kura hubeba masanduku ya kura na matokeo hadi makao makuu ya kata ili kufanya majumuisho ili kumpata mshindi wa udiwani na kumtangaza..

Baada ya hapo msimamizi wa kituo cha kupigia kura wakiambatana na msimamizi msaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata hubeba masanduku ya kura, matokeo ya kura za ubunge na urais hadi jimboni/wilayani kwenda kufanya majumuisho ya kura za ubunge na Urais..

Likifanyika hili, mshindi wa ubunge hutangazwa na kisha msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hutuma NEC matokeo ya kura za urais za jimbo...

Je, haya yalifanyika pale Hai katika interval ya masaa machache vile? How exactly?..

Na pengine tujaribu kujiuliza HAI, Kilimanjaro jiogarafia ya jimbo hilo ikoje? Walitumia teknolojia gani kiasi ambacho ndani ya masaa 8 tu baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa wakawa wamepata matokeo sahihi ya kila kituo na kuwatangaza wasindi wa udiwani na ubunge?

Mimi nasema, ni uongo. Haiwezekani abadani unless matokeo yawe yalikuwa yakitumwa kutoka vituo vya kupigia kura kwa njia ya mtandao wa computer!

Matokeo ya kawaida ya majimbo - ubunge japo na yenyewe ni wizi mtupu yalianza kutangazwa kesho yake ya tarehe 29/10/2020 kuanzia ingalau saa 6mch..

Ni wazi bila shaka kulikuwa na matokeo mengine "fake" tofauti na matokeo halisi yaliyotumika kutangaza washindi.

Mkuu napata taabu sana kuweka mchango wangu hapa, nimekuwa Jimboni Hai siku sita kabla, nilikuwa na reliable contacts 163 wakikusanya data kwenye vijiji vyote na mimi nilikuwa Mwowe Msikitini baadae nikaenda Lyamungo Sinde.

Mkuu kapigwa na hata wakirudia mara tano. Tatizo ni wananchi walikuwa na hamu ya kubadilisha mtu. Maneno yeyote mengine ni uwongo. ASANTE SANA.
 
Mbowe kadhibitiwa na dogo janja.

Safi sana Sabaya, wewe ni shujaa.
Sabaya, mkuu wa wilaya, mwenyekiti wa ulinzi na usalama wilayani, ana mamlaka ya kuamuru Polisi wafanye atakavyo anaweza kumtia ndani mtu yeyote kwa masaa 48, na mengine mengi. Huyu anakuwaje SHUJAA kwa kumtesa mtu ambaye hana jeshi, hana chochote?

Shujaa ni yule anayepambana na jitu lenye mabavu na kulishinda. Kama dogo Daudi alivyomshinda Goliati.

Kama kwa wizi huu ccm wanakuwa mashujaa, basi hawajitambui na ni wa kudharauliwa kabisa
 
Unaniuliza mimi kwa kutumia "phrase ya " umejuaje kwani...."

Kama ni hivyo, thibitisha wewe sasa kwa kutuambia kuwa HAI waliwahi kutoa matokeo kwa sababu walikuwa na "special and unique" wasimamizi wa vituo..

Lakini ninachoweza kukuambia na kukuhakikishia ni hiki;

Kwamba, mfumo wetu wa uchaguzi kuanzia uteuzi wa wagombea, kampeni, kupiga na kuhesabu kura, kutoa na kutangaza matokeo unafanana kila jimbo na nchi nzima..

Mfumo waliotumia jimbo la Kilosa, Mororogoro au Tandahimba nk ni uleule uliotumika HAI au Arusha mjini..

Na nikuambie jambo jingine moja;

Kwamba, bahati njema mimi nimeshiriki chaguzi karibu zote za vyama vingi; 1995, 2000, 2005, 2010, 2015 na huu wa juzi 2020..

Hakuna jimbo lililowahi kukamilisha mchakato uchaguzi (kupiga kura, kuhesabu kura, kushughulikia migogoro, kukusanya masanduku na kufanya majumuisho katani na jimboni) ndani ya masaa 6 hadi 8 baada ya mtu wa mwisho kwa kila kituo kupiga kura na kisha kumtangaza mshindi...!!

Nimeanza kuona HAI mwaka huu na Arusha na Kawe na Mbeya na Iringa na maeneo mengine..!!

Kuanzia mwaka 1995 hadi 2015, matokeo katika majimbo ya wabunge huanza kutoka kesho yake ingalau kuanzia saa 6mchana na kuendelea na kuna majimbo mengine huenda hadi siku 4 ndipo mshindi anatangazwa...!!

Kumbuka kuwa, mimi sisemi kuwa kuchelewa sana kutangaza matokeo ni vyema. Pia sisemi kuwa, kuwahi sana kutoa matokeo ya kura ni jambo baya..

Hapana. Hoja yangu ni kuwa, at least there is a "standard duration of time"..

Ukiwahi sana "under the standard duration of time", kama msimamizi wa uchaguzi, lazima kutakuwa na maswali utakayopaswa kujibu..

Vivyo hivyo ukichelewa sana kutangaza na wewe kama msimamizi umeshapokea matokeo ya vituo vyote na kufanya compilation, pia utakuwa na maswali ya kujibu..

Kila kitu kikizidi, kina madhara...
Sikubishii maoni yako ila sikubaliani na theory yako ambayo ni conspiratorial tu. Umma wa watanzania tulishaamabiwa hata na viongozi wa upinzania kuwa mwaka huu tume iliandaa uchaguzi vizuri sana na upigaji wa kura ulikuwa smooth sana.

Kwa hiyo ule ucheklleweshaji wa zamani mwaka huu haukuwapo kwa vile tume ilikuwa imeandaa vitu vingi vya kura na vifaa vilikuwapo vya kutosha.. Ni ajabu kuwa baada ya kushindwa wote viongozi wa upinzani wanakuja na sababu tofauti kabisa na assessment yao ya kwanza.
 
Hukutumwa kusoma wala ku comment, ni ujuha wako ndio uliokuleta kwangu.
short, jiheshimu nikuheshimu, sikumtukana wala kumkejeri yoyote yule. Najua na nina thamini maoni ya wote yenye staha. Hatuwezi wote kufanana. Kuvumiliana ni sehemu ya maisha. Mimi sio mnafiki wa kusifia ujinga hata kama nina uwezo wa kuhoji. Sio muoga, nina tumia kichwa na uwezo niliopewa kutafakari na kuhoji pale panapo hitajika.
Hongera mkuu, wewe ni hodari wa matusi. Mimi si fani yangu hii, kwa hio kwa hili nakupa ushindi kama mlivopata ushindi wa kupora haki za watu hongereni mabingwa wa wizi!
 
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho.

Ilikuwa kwa vyovyote vile asitangazwe mshindi either by HOOKS or by CROOKS. Hili lilikuwa apizo la Magufuli na wenzake na walilifanya kwa ushamba na ujinga wa viwango vyote vya ujinga duniani.

Kwa waliopoteza kumbukumbu, jimbo la HAI ndilo lilikuwa jimbo la kwanza kutoa matokeo ya uchaguzi takribani masaa yasiyozidi 8 baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa ile saa 10:00 jioni ya tarehe 28/10/2020.

Kwa teknolojia ya uhesabuji kura ktk vituo vya kupigia kura, kujaza fomu mbalimbali, compilation ya matokeo ngazi ya kata na jimbo ili kumpata mshindi wa udiwani na mbunge na kwa kuzingatia jiografia ya majimbo yetu ya uchaguzi yote Tanzania mtu anaweza kuona ugumu wa kuikamilisha kazi hiyo ktk interval ya masaa takribani 9 au 10 tu katika ngazi ya jimbo.

Bahati njema mimi nilikuwa mmoja wa maafisa wa uchaguzi huu nikiwa mwajiriwa ndani ya serikali, nikipewa jukumu hili pia.

Katika eneo nililosimamia mimi, kituo cha mwisho kuleta matokeo wilayani (jimboni) ili kufanya majumuisho kumpata mshindi wa ubunge ilikuwa ni saa 2asb kesho yake yani 29/10/2020!

Kwa kawaida, baada ya kituo cha kupigia kura kufungwa saa 10:00 jioni, uwezekano wa mtu wa mwisho kupiga kura inaweza kuwa kati ya saa 1 hadi 1.30 kutegemea na kituo na idadi ya wapiga waliokuwepo kabla ya saa 10 jioni. Hii maana yake mtu wa mwisho alipiga kura saa 11:30jioni kabla ya kuanza kuhesabu..

Kuna vituo vingine zoezi la kuhesabu kura, kubishana na mawakala na kutatua migogoro inayojitokeza na kujaza fomu mbalimbali ikiwemo ya taarifa ya kituo lilikwenda hadi saa 4usiku..

Baada ya hapo kwa kawaida msimamizi wa kituo cha kupigia kura hubeba masanduku ya kura na matokeo hadi makao makuu ya kata ili kufanya majumuisho ili kumpata mshindi wa udiwani na kumtangaza..

Baada ya hapo msimamizi wa kituo cha kupigia kura wakiambatana na msimamizi msaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata hubeba masanduku ya kura, matokeo ya kura za ubunge na urais hadi jimboni/wilayani kwenda kufanya majumuisho ya kura za ubunge na Urais..

Likifanyika hili, mshindi wa ubunge hutangazwa na kisha msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hutuma NEC matokeo ya kura za urais za jimbo...

Je, haya yalifanyika pale Hai katika interval ya masaa machache vile? How exactly?..

Na pengine tujaribu kujiuliza HAI, Kilimanjaro jiogarafia ya jimbo hilo ikoje? Walitumia teknolojia gani kiasi ambacho ndani ya masaa 8 tu baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa wakawa wamepata matokeo sahihi ya kila kituo na kuwatangaza wasindi wa udiwani na ubunge?

Mimi nasema, ni uongo. Haiwezekani abadani unless matokeo yawe yalikuwa yakitumwa kutoka vituo vya kupigia kura kwa njia ya mtandao wa computer!

Matokeo ya kawaida ya majimbo - ubunge japo na yenyewe ni wizi mtupu yalianza kutangazwa kesho yake ya tarehe 29/10/2020 kuanzia ingalau saa 6mch..

Ni wazi bila shaka kulikuwa na matokeo mengine "fake" tofauti na matokeo halisi yaliyotumika kutangaza washindi.
Umejitahidi sana kuelezea msimamo wako ambao ni haki yako. Lakini umemwacha msomaji bila majibu, baadhi ya maswali kadhaa ambayo msomaji anaweza kuuliza au wewe unaweza kuyajibu:
1. Je, matokeo yalitangazwa saa ngapi na siku gani? (ie baada ya masaa mangapi tangu kufungwa kwa uchaguzi? Je, ni jimbo pekee ambalo lilitangaza matokeo haraka kuliko jimbo lolote lile lenye uwiano wa idadi ya wapiga kura?

2. Je, utaratibu wa kuhesabu na kutangazwa amepewa nani?
3. Je, kwenye kuhesabu kura nani huwa wanashiriki, i.e. Wakala wa wagombea wanakuwepo wa pande zote mbili? Je, nani wengine wanahusika?

4. Je, nani wana dhamana ya kubeba masanduku ya kura? Je, kuna nani zaidi anayehusika kuona kwamba masanduku hayo hayabadilishwi au kwa namna yoyote ile kuhujumiwa?
5. Je, unao ushahidi usio na shaka kwamba JPM alihusika na hizo njama? Tupe ushahidi wako vinginevyo ni majungu tu.
 
Yani ni uongo na dhuruma za wazi,kuna majimbo gari la mwisho kuwasili Wilayani naambiwa ilifika SAA 5:30 alfajiri
 
Vp kihusu ule uchaguzi wa Serikali za Mitaa?? Mlichukua hatua yeyote au mlishangilia??
Aaah mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu...
Sijaona wala kusikia hatua zozote zilizochukuliwa baada ya kususia uchaguzi wa serikali za mitaa
Me mwenyewe ni miongoni mwa wale tuliopinga Maan niliona kama viongozi wameweka maslai ya chama mbele bila lengo lolote...
Ila kwa uchaguzi huu hatua zingechukuliwa tena za haraka sanaa maan wahusika ndo viongozi wenyewe
 
Halafu mkiona kuna shida mahali mngechukua hatua gani ?
Hatua nyingi Sanaa Mkuu.....
-Kwenda jumuiyaa za kimataifa..
-Maandamano ya Aman.. tena yangefanikiwa maan watu walikuwa na morale kubwa sanaa
-kufungua pingamizi mahakaman n.k
 
Back
Top Bottom