Uchaguzi 2020 CASE STUDY - Jimbo la Hai - Walitumia teknolojia gani kupata matokeo sahihi ya kila kituo ndani ya saa 8?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho.

Ilikuwa kwa vyovyote vile asitangazwe mshindi either by HOOKS or by CROOKS. Hili lilikuwa apizo la Magufuli na wenzake na walilifanya kwa ushamba na ujinga wa viwango vyote vya ujinga duniani.

Kwa waliopoteza kumbukumbu, jimbo la HAI ndilo lilikuwa jimbo la kwanza kutoa matokeo ya uchaguzi takribani masaa yasiyozidi 8 baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa ile saa 10:00 jioni ya tarehe 28/10/2020.

Kwa teknolojia ya uhesabuji kura ktk vituo vya kupigia kura, kujaza fomu mbalimbali, compilation ya matokeo ngazi ya kata na jimbo ili kumpata mshindi wa udiwani na mbunge na kwa kuzingatia jiografia ya majimbo yetu ya uchaguzi yote Tanzania mtu anaweza kuona ugumu wa kuikamilisha kazi hiyo ktk interval ya masaa takribani 9 au 10 tu katika ngazi ya jimbo.

Bahati njema mimi nilikuwa mmoja wa maafisa wa uchaguzi huu nikiwa mwajiriwa ndani ya serikali, nikipewa jukumu hili pia.

Katika eneo nililosimamia mimi, kituo cha mwisho kuleta matokeo wilayani (jimboni) ili kufanya majumuisho kumpata mshindi wa ubunge ilikuwa ni saa 2asb kesho yake yani 29/10/2020!

Kwa kawaida, baada ya kituo cha kupigia kura kufungwa saa 10:00 jioni, uwezekano wa mtu wa mwisho kupiga kura inaweza kuwa kati ya saa 1 hadi 1.30 kutegemea na kituo na idadi ya wapiga waliokuwepo kabla ya saa 10 jioni. Hii maana yake mtu wa mwisho alipiga kura saa 11:30jioni kabla ya kuanza kuhesabu.

Kuna vituo vingine zoezi la kuhesabu kura, kubishana na mawakala na kutatua migogoro inayojitokeza na kujaza fomu mbalimbali ikiwemo ya taarifa ya kituo lilikwenda hadi saa 4usiku.

Baada ya hapo kwa kawaida msimamizi wa kituo cha kupigia kura hubeba masanduku ya kura na matokeo hadi makao makuu ya kata ili kufanya majumuisho ili kumpata mshindi wa udiwani na kumtangaza.

Baada ya hapo msimamizi wa kituo cha kupigia kura wakiambatana na msimamizi msaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata hubeba masanduku ya kura, matokeo ya kura za ubunge na urais hadi jimboni/wilayani kwenda kufanya majumuisho ya kura za ubunge na Urais..

Likifanyika hili, mshindi wa ubunge hutangazwa na kisha msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hutuma NEC matokeo ya kura za urais za jimbo...

Je, haya yalifanyika pale Hai katika interval ya masaa machache vile? How exactly?..

Na pengine tujaribu kujiuliza HAI, Kilimanjaro jiogarafia ya jimbo hilo ikoje? Walitumia teknolojia gani kiasi ambacho ndani ya masaa 8 tu baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa wakawa wamepata matokeo sahihi ya kila kituo na kuwatangaza wasindi wa udiwani na ubunge?

Mimi nasema, ni uongo. Haiwezekani abadani unless matokeo yawe yalikuwa yakitumwa kutoka vituo vya kupigia kura kwa njia ya mtandao wa computer!

Matokeo ya kawaida ya majimbo - ubunge japo na yenyewe ni wizi mtupu yalianza kutangazwa kesho yake ya tarehe 29/10/2020 kuanzia ingalau saa 6mch..

Ni wazi bila shaka kulikuwa na matokeo mengine "fake" tofauti na matokeo halisi yaliyotumika kutangaza washindi.
 
Maisha yaendelee! Hakuna namna ya kufanya.

Nimehamishia nguvu kushabikia timu yangu ya Simba!Siasa za bongo ndio nimefikia tamati!Sio kupiga kura au kushiriki shughuli za siasa za moja kwa moja eneo ninaloishi!Ikiitishwa mikutano ya kisiasa eneo langu mimi naelekea bar kunywa bia!Kadi yangu ya mpiga kura sasa hivi ni majivu!

Simba oyeeeee!
 
Sawa kabisa. Sasa kwanini msikusanye huo ushahidi wote then mkaenda mahakamani. Ni muhimu kutumia huu uzalendo ulionyesha hapa kwa kusema ukweli utumike huko, uwe shahidi upande wa kina mbowe ili wapate haki yao otherwise utaonekana ni mnafiki au unatumiwa tu.

Na hayo yote yanatokea kwanini nyinyi kama wasimamizi na mawakala mnakubari kama sio kushiriki kwenye dhurma? au hujapata mgao wako?

Watu kama nyinyi ni kutia risasi kabisa, maana mnashiriki kuiangamiza nchi.
 
Matokeo ya uchaguzi mkuu mwaka huu yalikua matokeo ya kupikwa, Rais wabunge na madiwani walijiteua wenyewe kwa kile kilichoitwa order kutoka juu(NEC) wasichokijua ni kwamba utawala uliongia madarakani uneturudisha nyuma miaka 20, Serikali ndio inayokwenda kushinda dhidi ya raia na watumishi wake wote.
 
Kwa mfano Mbowe Kashindwa, hivi Unapata faida gani kushindwa kwa mtu huyu. Subiri Utafurahia kushidwa kwa Mbowe na Wapenzani wote Pale baada ya Miaka Miwili...Mitatu.

Kama miaka Mitano Umeinjoy then Jua Mitano Mingine utaenjoy mara dufu.

Kama ulikuwa Kajambanani/Chokola then jua utakuwa hivyo mara dufu.
 
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho...
Acha uzushi, kama hayo yalitokea mbona mgombea wa CHADEMA alijaza fomu ya kukubali matokeo?
 
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho...
unahisi taarifa hii itabadilisha maamuzi na kwamba mbowe wako ashinde ??? Nini faida ya uzi wako wakati huu?? Au unawafariji wenzako mkuu???

AchAna na mambo ya uchaguz yamepit.. chapa kazi tuijenge nchi
 
Jimbo la uchaguzi la HAI liko mkoa wa Kilimanjaro. Ni jimbo ambalo "the most wanted person" na watawala wa CCM, mwenyekiti wa taifa wa chama kikuu cha upinzani Tanzania - CHADEMA ndugu Freeman Aikael Mbowe aligombea ubunge kupitia chama chake hicho...
Ukweli ni kwamba polisi , makarani na mawakala waliosimamia uchaguzi hawakutoka nje ya nchi. Siku moja kabla ya uchaguzi kuna karani mmoja wa jimbo la Moshi mjini alisikika akiongea kwenye simu kuwa wao wameelekezwa kwamba wakati wa kuhesabu kura karani atasoma kura hatazilizo tikiwa kwa wagombea wengine kuwa za CCM, wakala akibisha Karani ambaye ni kada wa CCM (mjumbe wa tawi) ataita polisi kumtoa nje wakala na kura zitahesbiwa na kurekodiwa kwa faida ya mgombea wa CCM.

Kingine ni karatusi nyingi zilizo baki katika vituo zilitikiwa kwa wagombea wa CCM. Japo haya ni vigumu kithibitisha lakini ukweli utaendelea kujulikana siku hadi siku maana wadau wa uchaguzi ni wengi na hakuna siri ya watu zaidi ya wawili Sembuse makarani na mawakala zaidi 80,000
 
Mbowe kengeza kadhibitiwa na dogo janja.
Safi sana sabaya, wewe ni shujaa.
Mboye ajiteue viti maalum
Mbowe wewe ni boya tu

Uchama pembeni, hapa nauliza wewe mtu mzima na akili zako timamu kabisa pengine ni Baba/Mama wa familia unaandika ujinga wa kiwango hiki? Ok ana Makengeza does that one makes u Happy?

Wewe hapo ulipo umejiona kasoro ulizanazo! Acheni mambo ya kukosoa uumbaji wa Mwenyezi Mungu,shindaneni kwa hoja na siyo huu ujinga ulioandika hapa. Kila la heri.
 
Back
Top Bottom