Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Ni mjinga pekee atayeshangilia kuwa na kampuni chache zenye monopoly badala ya kuwa na kampuni nyingi ndogondogo zenye kuajiri watu wengi na kutengeneza ushindani.
Mfano safaricom Ina dominate soko kwa zaidi ya 60% utailinganishaje na Tanzania kwenye kampuni zaidi ya 4 na hakuna ambayo inamiliki soko zaidi ya 40% hivyo ushindani ana ajira nyingi kwa wazawa.
Ukija kwenye viwanda vya UNGA wa sembe, Kenya kuna viwanda vichache sana sana sidhani kama vinafika 100 vya UNGA wa sembe,hivyo hata ajira ni kidogo sana tofauti na Tanzania ambako hakuna kiwanda kikubwa Cha sembe kinachodominate ila vipo zaidi ya 2000 vidogo vidogo vyenye uwezo kuzalisha Tani 20 kwa siku hivyo ajira ni kubwa sana kuliko Kenya yenye viwanda vikubwa vichache, vilevile kwenye mafuta ya kula na bidha nyingine.
Boss safaricom ilishauzwa, its no lomger a kenyan company
 
This a typical stairs in a regular Kenyan house vs. Samia Stadium stairs …. Sijui mtu anaingia stadium au anaingia kwa choo …🤣🤣🤣🤣
View attachment 3602416View attachment 3602417
Endelea kucheka halafu mmalize kujenga Talanta mjipate ham-meet specifications! Maana kuna suala la sections separations kwa kila level with multiple access! Mnatamba kujenga Talanta yet hamna bus stand ya maana Nairobi kumejaa tope!
 
Total sponsorship ya KPL!
Ukichua media rights za Azam media ukajimlisha na sportpesa sponsorship kwa mwaka kwa league yao yote bado hawajafikisha sponsorship ya muuza jezi wa simba , jatty rutty
Screenshot_20260606-174155~2.jpg
Screenshot_20260606-173905~2.jpg
 

Tumeshakubaliana kuwa kwenye mambo yetu ya ndani tunanyukana kwa siasa zetu za ndani. Lakini tukitoka nje ya nchi tunakuwa wamoja.
Rais anapoenda nje ya nchi, yeye ni sura ya Taifa, Unatakiwa ujue tofauti ya Local na International.
Watu wenye akili watahisi kuwa hujui maana ya National Interests in International Society
 

NB: Mipaka ya nchi inapoishia, ushindani wa ndani unapaswa kusimama. Katika diplomasia ya kimataifa, mataifa hayashindani kama vyama vya siasa, bali yanashindani kama dhumuni moja la kitaifa dhidi ya mataifa mengine. Tofauti za ndani hazipaswi kupelekwa nje kwa sababu zinafifisha nguvu ya nchi ya kujadiliana au kujitetea.

Ushindani wa kisiasa, utofauti wa kiitikadi, na mijadala ya ndani ni mambo ya kawaida na ya afya katika demokrasia yoyote. Ndani ya nchi, vyama na makundi yanaruhusiwa kupishana vikali ili kujenga nchi.

Rais anaposafiri nje ya nchi, haendi kama mwenyekiti wa chama fulani cha siasa, bali anaenda kama Mkuu wa Nchi (Head of State).

Anakuwa ndiye nembo, sauti, na uwakilishi wa wananchi wote (ikiwemo wapinzani wake wa ndani).
Kushambulia, Kumdharirisha au kudhoofisha hadhi ya Rais akiwa nje ya nchi kunatafsiriwa kimataifa kama kudhoofisha Taifa lenyewe, jambo linaloweza kupunguza ushawishi wa nchi hiyo kiuchumi, kisiasa au kiusalama.
 
Back
Top Bottom