President of China
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 34,013
- 93,380
Hakuna udini Tanzania, but tunawaonya tu, wale wanaoleta chokochoko za udini. Mimi ni Mkristo, Mke wangu ni muislam. Watoto wangu wanaenda Kanisani na Msikitini. Wao ni WakrislamKuna tofauti ya terrorism na udini. Alshabaab ni millitia ya nchi jirani iliyoattack Kenya kwa sababu ya grievances za kisiasa na nimekueleza hivo. Vita vya Somalia sio vya udini bali ni siasa na wanauana waislamu kwa waislamu. Kando na hilo, Somalia kuna udini sana japo huo udini haujaleta shida ya mauaji popote maanake Somalia 98% ya population ni Waislamu. Mimi nimeishi Somalia na nilipokuwa huko, niliona shida ya kidini ipo. Bahati yao wengi wao ni Waislamu ila ukienda huko uwe Mkristo unapata wameanza kukuonyesha kaubaguzi fulani hivi hadi saa zingine inabidi ujifanye Mwislamu ndio maisha kidogo iwe smooth. Somalia ingekuwa na Wakristo zaidi ya asilimi 10 kungekuwa na shida sana.