Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

#BIASHARA Mmiliki wa kampuni za Mbeya Cement na Camel, Edha Nahdi, amenunua kampuni kubwa zaidi ya saruji nchini Kenya kwa thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 260.

Ununuzi wa kampuni hiyo ya Kenya, Bamburi Cement, inayojulikana kwa uzalishaji wa saruji ya Tembo umefanywa kupitia kampuni ya AMSONS Group ambayo Nahdi ni Mkurugenzi Mtendaji.

Ununuzi huo wa kampuni ya Bamburi ambayo ina viwanda viwili kwenye miji ya Nairobi na Mombasa, utaifanya kampuni ya AMSONS kuwa mojawapo ya wawekezaji muhimu zaidi kwenye sekta ya saruji kwenye eneo la Afrika Mashariki.

Bamburi kwa sasa inazalisha wastani wa tani milioni 3.2 za saruji kwa mwaka na ukijumlisha na uzalishaji wa tani milioni 1.6 ambazo tayari zinazalishwa na AMSONS kupitia Mbeya Cement na Camel, uwezo wa kuzalisha saruji wa kampuni hiyo kwa sasa utafikia kiasi cha tani milioni 4.8 za saruji.

Hatua ya AMSONS kuingia kwenye biashara kwa kiwango hiki ni miongoni mwa hatua mpya kabisa kwenye uhusiano wa kiuwekezaji baina ya nchi za Afrika Mashariki. Kwa kawaida, wawekezaji kutoka Kenya wamekuwa wakiwekeza Tanzania kwa muda mrefu sasa lakini ununuzi huu wa Bamburi unaonyesha namna wawekezaji Watanzania wanavyoanza kuteka kibiashara nchi hiyo jirani.

Kampuni ya AMSONS ilianzishwa mwaka 2006 ikijulikana zaidi kwa biashara ya mafuta kupitia jina la Camel Oil lakini sasa imeingia kwenye biashara mbalimbali ikiwemo ya uzalishaji wa unga wa ngano na usafirishaji.

Vyombo vya habari vya Kenya na hasa kwenye mitandao ya kijamii vimeeleza kwamba jambo kubwa katika uwekezaji wa AMSON kununua kampuni ya Bamburi ni namna ilivyokubali kulipa gharama za ziada ili kufanikisha kukamilika kwa biashara hiyo.

#EastAfricaTV

FB_IMG_1720763966544.jpg
 
Hivi unajua huyo huyo muhindi ndiye anayemilika Port of Dar? Yani unashare yetu yenye tumegundua utapeli tukasimamisha wakati kwenu mmeuza Port, mmeuza BRT, mmeuza National parks na bado mnaendelea kuuza.
Tumebinafsisha hatujauza,ujinga huu umemezeshwa na Wapinzani.

Hifadhi hazijauzwa Wala kubinafsishwa acha upumbavu
 
#BIASHARA Mmiliki wa kampuni za Mbeya Cement na Camel, Edha Nahdi, amenunua kampuni kubwa zaidi ya saruji nchini Kenya kwa thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 260.

Ununuzi wa kampuni hiyo ya Kenya, Bamburi Cement, inayojulikana kwa uzalishaji wa saruji ya Tembo umefanywa kupitia kampuni ya AMSONS Group ambayo Nahdi ni Mkurugenzi Mtendaji.

Ununuzi huo wa kampuni ya Bamburi ambayo ina viwanda viwili kwenye miji ya Nairobi na Mombasa, utaifanya kampuni ya AMSONS kuwa mojawapo ya wawekezaji muhimu zaidi kwenye sekta ya saruji kwenye eneo la Afrika Mashariki.

Bamburi kwa sasa inazalisha wastani wa tani milioni 3.2 za saruji kwa mwaka na ukijumlisha na uzalishaji wa tani milioni 1.6 ambazo tayari zinazalishwa na AMSONS kupitia Mbeya Cement na Camel, uwezo wa kuzalisha saruji wa kampuni hiyo kwa sasa utafikia kiasi cha tani milioni 4.8 za saruji.

Hatua ya AMSONS kuingia kwenye biashara kwa kiwango hiki ni miongoni mwa hatua mpya kabisa kwenye uhusiano wa kiuwekezaji baina ya nchi za Afrika Mashariki. Kwa kawaida, wawekezaji kutoka Kenya wamekuwa wakiwekeza Tanzania kwa muda mrefu sasa lakini ununuzi huu wa Bamburi unaonyesha namna wawekezaji Watanzania wanavyoanza kuteka kibiashara nchi hiyo jirani.

Kampuni ya AMSONS ilianzishwa mwaka 2006 ikijulikana zaidi kwa biashara ya mafuta kupitia jina la Camel Oil lakini sasa imeingia kwenye biashara mbalimbali ikiwemo ya uzalishaji wa unga wa ngano na usafirishaji.

Vyombo vya habari vya Kenya na hasa kwenye mitandao ya kijamii vimeeleza kwamba jambo kubwa katika uwekezaji wa AMSON kununua kampuni ya Bamburi ni namna ilivyokubali kulipa gharama za ziada ili kufanikisha kukamilika kwa biashara hiyo.

#EastAfricaTV

View attachment 3039988
Toka amenunua Mbeya Cement amemwaga pesa na Sasa kiwanda kimeanza kupata faida.

Mwaka uliopita kilitoa Gawio baada ya miaka 10.

Anawekeza pesa ambapo kiwanda Cha Mbeya cement Sasa kinatarajia kuanza Kuzalisha Tani 1.5Mln.
 
Mama amekopa sana haijulikani pesa zinakoenda 🤣🤣🤣

Kigoma 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/C9T8NiaCE9Y/?igsh=MTZneDMybDJxbzkyNQ==

Tunataka kuona zile fedha zakutisha ziliokopwa za lot 3,4 and 6 za SGR 😁😁😁😁😁😁

Ukipata any update let me know😁😁😁

SASA ni over 2yrs update ziko wapi???

Hope umeelewa what I mean, kama haturuhusiwi kukosoa mutuambie ili tuendelee kusifia kuona nchi sukari inafika elf kumi kwa kilo na bado waziri WA kilimo Yuko ofisini 😁😁😁😁😁😁
 
Hivi hamna namna huyo tukamripoti kwa mods wampige pini kuingia kwenye huu uzi?
Anatumia I'd nyingi humu, akipigwa ban hii anatumia ile, jamaa ni troll humu jf, nyuzi zote ndiyo yuko hivyo hivyo na ndiyo maana haupiti mwezi bila kupigwa ban, it seems jamaa bado haja mature hata kama ni mkubwa basi ni kubwa jinga.
 
Toka amenunua Mbeya Cement amemwaga pesa na Sasa kiwanda kimeanza kupata faida.

Mwaka uliopita kilitoa Gawio baada ya miaka 10.

Anawekeza pesa ambapo kiwanda Cha Mbeya cement Sasa kinatarajia kuanza Kuzalisha Tani 1.5Mln.
Je unajua wamiliki WA mbeya cement 65% walikua hao hao wanaomiliki bamburi na ni wahindi??😁😁

Serekali inamiliki 25% hvi Kama sijakosea hapo mbeya cement

Hilo unalijua lakini?????
 
Je unajua wamiliki WA mbeya cement 65% walikua hao hao wanaomiliki bamburi na ni wahindi??😁😁

Serekali inamiliki 25% hvi Kama sijakosea hapo mbeya cement

Hilo unalijua lakini?????
Kwa nini nisilijue? Kwanza Serikali ndio ilikuwa inakwamisha ufanisi wa kiwanda,mama alilipa Madeni waliyokuwa wanadaiwa upande wa Serikali na kuwezesha kukwamua kiwanda.

Sasa kinaleta mabilioni na kutoa csr Kwa Wilaya husika
 
Back
Top Bottom