Hii ni sapphire nilokwambia.Kwa hiyo hizi takwimu za serikali ni uongo ila zako ndio sahihi si ndio? 👇👇View attachment 2978655View attachment 2978656View attachment 2978657
Zipo blue,pink na kijani.
Ya kijani ndio yenye thamani zaidi.
Hizo hapo ni pink sapphire gram moja ni $ 980 kama walivyoeleza hapo.
Ibadili iende kwa shilingi za kiTanzania ni milioni na kitu.
Kitu cha mwisho cha kukueleza.
Serikali inajikita katika dhahabu kwasababu dhahabu ndio madini yanayofaa thamani yake kwa mbadilishano na fedha,na kwa kuwa na higher durability ndio madini yaliyochaguliwa kuwa mbadilishano na fedha na kuwa sehemu ya hazina kwa sababu tatu.
1)Dhahabu ina wepesi kuipata.
2)Dhahabu ina wepesi kuihifadhi na ikabaki kuwa bora.
3)Dhahabu haina process nyingi na iko na characteristics moja kwa kila aina ya dhahabu,ipige moto inakua safi,sio kama gemstone kutunza gharama pia hainaga durability.
Ndio maana gemstone huuzwa sana nje kwasababu ya mapambo.
Leseni ya mchuuzi wa dhahabu ni Tzsh 250,000.
Leseni ya mchuuzi wa gemstone za bei ya juu (Almasi,sapphire,ruby,Tanzanite) ni Tzsh 1,800,000.
Labda wawe wamebadilisha.
Kaulizie watu wa madini kama nimeongopa uje unikosoe.
Picha inayofuata chini ni ruby iliofanyiwa mnada itizame thamani yake.
HIVI UNAWEZA IFANYIA MNADA DHAHABU KIASI HICHO!?
Carat 50 ni sawa na gram 20+ ila thamani yake mabilioni ya Tanzania.
Dhahabu gram 20 ni sawa na milioni 2.6+.