Kweli kabisa hata hii kasi ya maendeleo imetokana na vitu ambavyo hata havikuwa vya wazi. Vitu kama umoja wetu, kuongea kiswahili, kuchanganya wanafunzi wa sekondari kutoka mikoa yote nchini, viliweka misingi ya kuijenga nchi.
Leo hii tuna undugu na amani, ndiyo maana JF iliweza kushamiri, wakina Dimond wanafanikiwa, Milard Ayo akianzisha Channel inapata subscribers, ligi yetu unakuwa kwa kasi, hata CAF wanalijuwa hilo.
Sasa tumekuja na hizi tangibles kama ujenzi wa barabara, reli, masoko, bwawa la umeme, viwanja vya ndege n.k. Yaani miaka 10 ijayo tutakuwa mbali sana.