Hakuna uwazi, unajuwa kilichosainiwa MOU feb 28 2022, kwenye Dubai expo? Unajua kilichosainiwa Oct '22 na serikali. Mbona walikaa kimya hawakutueleza kuhusu DP World mpaka taarifa zilipovuja ndo wanajibaraguza kujidai kutaka kujadiliwa bungeni.
Mkuu, uwazi upi unaoutaka?. Hakuna nchi yoyote Ile duniani ambayo Kila inachokifanya katika utendaji wake wa Kila siku lazima izungumze kwa wananchi. Mkuu kila siku wizara zinaingia mikataba mingi Sana karibia Kila siku mikataba mbalimbali inasainiwa. Kama Kila mkataba lazima serikali isema kwa wananchi wote basi hakuna kazi yoyote itakayofanyika nchini, nchi hii tutakua kazi yetu ni taharuki na mijadala kuanzia asubuhi hadi jioni kuhusu mikataba.
Mkuu, kazi ya serikali chini ya rais aliyechaguliwa na sisi wote, ni kuingia mikataba kwa niaba yetu Ili sisi tuendelee na kazi zingine, yeye na wasaidizi wake hawaendi shamba Wala kufanya kazi zingine, kazi zao wao ni hizo za kuingia mikataba kwa niaba yetu tukiamini kwamba wanafanya hivyo kwa mujibu wa maslahi, taratibu na mamlaka waliyokabidhiwa kikatiba ya nchi yetu.
Bunge ndilo lenye jukumu la kuisimamia serikali endapo itakengeuka jinsi ya kuingia mikataba hiyo, serikali inapaswa kuomba kibali toka bungeni pale inapotaka kuingia mikataba mikubwa Kama huu wa DPW, lakini mikataba mengine mingi, serikali haiwajibiki kulishauri bunge, hiyo ipo chini ya uwezo wao, ni sehemu ya kazi zao.
Kwa mfano SSH alipokwenda ufaransa, aliingia mkataba na kampuni Ili kuja kukarabati uwanja wa ndege Dar "terminal ll", bila hata kushauri bunge, au mikataba ya Air France kuja Dar, au mikataba ya Ujenzi wa Meli na kampuni la Korea.
Huu mkataba wa DPW ni mkataba mkubwa, ndio sababu serikali ilipaswa kuomba bunge liridhie. Kawaida kabla bunge alijaanza vikao vyake, serikali uwapelekea wabunge nakala ya kile ambacho wanataka wabunge wakiridhie, Ili wakijue mapema Ili waweze kuwashirikisha wapiga kura wao Ili wajue na kutoa maoni Yao.
Hizi nakala zikiwafikia wabunge, lazima wazungumze na wananchi wao Ili kuomba ushauri, hapo ndipo taarifa zilipoanza kuenea na kusababishia taharuki, sio kweli kwamba kulikua na usiri hadi wananchi waliposikia na kupiga kelele.
Tatizo ni uelewa mdogo wa wananchi jinsi serikali na bunge vinavyofanya kazi katika kushughulikia mambo haya ya mikataba.
Wewe kwa akili yako unadhani kwamba ni kelele za wananchi ndizo zilizosababisha kwa huu mkataba kupelekwa bungeni, wakati ni kinyume chake. Kitendo Cha mkataba kupelekwa bungeni ndicho kilichosababisha wananchi kujua na kuanza kupiga kelele.