Ndio sababu nimekushamgaa Sana kuwataja viongozi wa Kenya kwamba ni watu wenye kupenda ushirikiano wa biashara.
Katika nchi ambayo haipendi kabisa ushirika wa biashara katika ukanda huu, Kenya inaongoza. Kenya itashirikiana na nchi yoyote ya jirani pale itakapoona kwamba yenyewe itafaidika zaidi kuliko, au Kama hawana jinsi ya kufanya.
Kenya inalazimika kujipendekeza kufanya biashara na Tanzania kwa sababu uchumi wa Kenya unaitegemea Sana Tanzania, bila Tanzania uchumi wao utavurugika wote
1)Mali ghafi zitokanazo na kilimo Kama vile pamba, katani, miti na Alizeti, Kenya inategemea Tanzania by 70%
2)Vyakula vya binadamu na wanyama, matunda na viungo, Kenya hutegemea Tanzania by 40%
3)Gas za kupikia, na muda sio mrefu tunawapelekea Bomba la gesi.
4)Kenya hutegemea kutumia ardhi ya Tanzania kupitisha bidhaa zao kwenda masoko ya nchi za SADC
5)Tanzania is the biggest Business partner in Afrika. Kenya is not the biggest Business partner to Tanzania
Mambo haya yanaifanya Kenya kuigopa Tanzania, ndio sababu wanashindwa kutuchezea Kama wanavyowachezea waganda, lakini kamwe usiwasifie viongozi wa Kenya kwamba wanapenda ushirikiano wa kibiashara.
Mkuu wakenya sio watu wazuri katika kufanya nao biashara. Hivi hujiulizi kwanini Bakhresa akimbilie kuwekeza katika nchi zote zinazotuzunguka, Hadi ameenda kuwekeza South Afrika lakini asiende Kenya wakati Kenya ndio nchi yenye uhitaji mkubwa wa Vyakula?