ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 79,425
- 85,248
Vikwazo na kutoaminiana kupo ila inatakiwa utashi wa Kisiasa kama unavyoona Ruto anafanya ,haya mambo huanzia Kwa Wanasiasa sio tuu wa Kenya Bali na Tanzania.Mkuu, ndio sababu nikakuambia waulize wafanyabiashara wakubwa ambao wanakwenda Kenya kuwekeza, hao ndio wanaowajua wakenya, wewe hujawahi kuwa mfanyabiashara mkubwa ambaye unaweza kuwa tishio kwa wafanyabiashara wa Kenya, wewe uliajiriwa na kufanya kazi na wakenya.
Wewe unachanganya kati ya utendaji kazi wa wakenya na Kenya kuwa ni nchi inayoruhusu biashara huru, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. Wewe ulifanyakazi na wakenya, kwahiyo unawajua vizuri utendaji wao wa kazi ukilinganisha na watanzania, lakini hujawahi kwenda Kenya kuwekeza, huko hukujui vizuri, wanaowajua vizuri wakenya katika uwekezaji ni
1)Serikali ya Uganda
2) Rostam Aziz
3)Aliko Dangote
4)Mo Dewji
5) Bakhresa
Waulize watakujuza vizuri.
Kuhusu kuondoa vikwazo vya biashara, Hilo kwa wakenya Wala lisikupe matumaini yoyote, hakuna vikwazo vyovyote vya biashara kati ya Kenya na Uganda, lakini Kenya wanaamua tu kuzuia bidhaa za Uganda bila kufuata taratibu za makubaliano.
Mkuu jipe muda vizuri wa kuwajua wakenya, usifurahie maneno na maandishi Kama hayo ya kwenye magazeti, inapofika kwenye utekelezaji, wakenya wanaangalia maslahi Yao, kamwe hawajali Kama kulikua na makubaliano yoyote, Kenya ni "man eat man society", never trust them.
Ndio maana Afrika haiwezi kuendelea na inashindwa kufanya biashara inavyostahili baina yake Kwa sababu ya mawazo na hisia za kipuuzi kama hizo za kutoaminiana etc..
Kwa nini iwe rahisi kufanya biashara na Nchi za Mbali kuliko Afrika Kwa Afrika? Huoni Kuna shida hapo? Matokeo yake ni umaskini wa Kutolea Kwa sababu watu wengi hawawezi fikia masoko ya mbali plus lugha nk nk.