Kwa hiki kiangazi kilichotukumba, mngekua na akili mngejituma mpige hela ya kweli, maana tunanunua mahindi hadi mbali.
Msikilizeni huyu jamaa






Anajifanya hajui kama kwa ss hakuna balance ktk biashara baina ya Tz na Kenya, kwa taarifa yako tu pesa tunazopata kutoka kwenu ndio zinafanya tufanye miradi mikubwa ambayo kwenu ni ndoto za alinacha.
kwa mfano tunajenga bwawa kubwa la umeme ambalo ni miongoni mwa mabwawa makubwa yaliyojengwa na binadamu duniani na tunajenga kwa pesa za ndani, sasa jiulize pesa tunatoa wapi.
Tumejenga electrifitried SGR kutoka Dar to Moro kwa pesa za ndani.
Tunajenga BRT system ndefu zaidi Afrika na miongoni mwa network ndefu za BRT duniani ikiwa pesa zetu pia zinahusika.
Tunajenga infrastructures nyingi za kisasa, hujiulizi pesa zinatoka wapi? Madaraja ya kisasa (cable stayed bridges) ambayo nyie hamna hata moja na hamuwezi kuwa nayo kwa miaka mingi ijayo.
Tunajenga masoko, bus terminals, meli kubwa, tunanunua ndege kubwa, tumeunganisha vijiji vyote na umeme, barabara mitaani zenye taa (hii battle ya barabara za mitaani hatushikiki uliza wenzako pia nadhani na wewe umeona).
Tunajenga Dodoma mpya ambayo imewashtua sn na bado inaendelea kuwashangaza, tunajenga Ikulu kubwa pale Dodoma japo tunayo nyingine Dar, nyie mpk leo hamuna uwezo wa kujenga Ikulu, Rais wenu mpk kesho anakaa kwenye nyumba iliyojengwa na mkoloni.
Tunajenga ports na Airports za kisasa, nyie hamna uwezo huo, mnafanya ku renovate airport iliyojengwa na mkoloni.
Tumewazidi mambo mengi na vyote hivyo tumefanya kwa pamoja and in less than ten years (from 2015 up to now) hiyo pekee inatosha kukuonesha nguvu ya kiuchumi iliyonayo Tz.
Nikushauri tu we baki na GDP ya mchongo lkn ukitaka twende ground sisi sio size yenu kabisa na hatupaswi kulinganishwa na nyie tena, najua mnaumia ila vumilieni, hii ndiyo Tz mpya ambayo kwa sasa inawafanya muwe na adabu, huoni hata wewe umebaki kuongea maneno yale yale ya 2005 huna maneno mapya ni yale yale ya GDP but tukiingia ground huna la kuongea msee














