7seven
JF-Expert Member
- Mar 27, 2022
- 3,744
- 8,065
Unachosema ni kweli kaka kuna mambo yanafanyiwa kazi ambayo huwa yanaongelewa humu.Yani hawa wapuuzi hii thread inasaidia Tz pekee mana tangu kuanzishwa kwake mabadiliko makubwa yametokea Tz kuanzia viongozi mpk raia, watu wanazidi kustaarabika, imebaki kitu kimoja tu UJENZI HOLELA ambayo nayo tunakwenda kuikomesha, lkn kwa upande wa hawa jamaa hii thread haijawasaidia chochote.
Sasa hivi Kilimanjaro kuna sheria kali imetungwa huwezi kukata mti bila idhini ya mamlaka, kabla hujachukua hatua yoyote lazima mamlaka iarifiwe ndipo unaruhusiwa, iwe mjini au kijijini lazima upate kibali kutoka Manispaa/Wilaya.
Binafsi ninawapongeza sana kwa hatua hii maana itasaidia kuondoa ukame na kutengeneza mandhari nzuri sana.
Hata mikoa mingine Tanzania ingewaiga watu wa Kilimanjaro kwa hili wanalolifanya.
Dodoma pia wanakuja vizuri kwenye upandaji miti, Kuna siku mkuu wa mkoa aliwaagiza watendaji wake wasimamie serikali za mitaa kuhakikisha wanapanda miti na kuhakikisha inakua.
Ni hatua nzuri sana, nchi nzima kuwa ya kijani ni suala la muda tu iwapo kama wataendelea na huu usimamizi wa sheria wa kupanda miti, kuitunza na kuzuia ukataji wa miti wa hovyo hovyo.


