Ndiyo maana nikasema, ni jinsi tuu sheria ilivyoandikwa katika nchi husika. Tanzania sheria imesema wazi kuwa serikali chini ya Rais ndiyo mmiliki wa ardhi. Katika nchi nyingi sheria haijatamka wazi kuwa ndiye mmiliki ila serikali zao zina njia nyingi ya kuichukua hiyo ardhi wakati wowote itakapotaka.
Hata Tanzania serikali haiwaondoi watu kwenye ardhi yao hovyo hovyo, ni pale tuu kunapokuwa na sababu ya muhimu kwa manufaa ya umma, mfano ujenzi wa reli, bomba la mafuta, sababu za kiusalama (ardhi kutitia) n.k. Serikali ikiomba watu kuondoka, wanatakiwa kupata fidia.