Ii
Kinachonishangaza ni kwamba wanasema mama anamwaga pesa, sasa kama anamwaga pesa mbona miradi inasuasua?
Sasa hivi husikii stendi wala masoko yakianza kujengwa bado wanahangaika na ile aliyoacha Magu for almost 2yrs now.
Miradi iliyokuwa ianze ya ujenzi wa meli mpya kimyaa.
SGR Isaka Mwanza wanajenga kambi tu kwa muda wa miaka 2 sasa.
Hakuna mradi mpya uliobuniwa mpaka sasa baada ya kifo cha Magu. Jamaa alikuwa anataka barabara za kuingia na kutoka miji yote mikubwa ziwe njia nne kwa 50km, alikuwa aanze na Dom Toka afe kimyaa.
Treni za Dar kimyaa, stendi ya Arusha kimyaa, ya moshi imeachwa ijiozee.
Miaka 2 hakuna hata tetesi za mradi mpya.
Nasubiri miradi ya TACTIC ianze mwezi wa tisa nione kama itasimamiwa ipasavyo.
Kipindi kile Ummy Mwalimu alikuwa busy hasa, sasa hivi yuko karelax sababu mkubwa wake hana vision.
Kipindi cha Magu niligundua watz wana akili sana wakipata kiongozi mzuri, ulikuwa ukisikia viongozi wa mashirika mbalimbali wanaelezea vitu in details mpaka unafurahi,
Sasa hivi wamegeuka kuwa chawa.
Kule kanda ya ziwa waganda wameanza kununua mpunga ukiwa shambani wanaenda kukoboa kwao wameanza kutuuzia mchele tuliolima.
Nb.
Magufuli alikuwa na mapungufu yake ila yale mazuri tulipaswa kuendelea nayo.
Kwanza unapayuka mambo usiyo na uhakika nayo,kwamba sgr ya Mwanza ni Kambi tuu si ndio? Umeolewa gongo wewe..
Hakuna miradi mipya unamdanganya nani? Sgr ya Kakutopora to Tabora sio mradi mpya?..
Eti husikii stand Wala masoko 😜😜,hujaona soko la Kariakoo likijengwa? Hujaona masoko ya machinga yakijengwa Dom na Dar? Soko lingine la machinga linajengwa Iringa,Kigoma, Kigamboni nk kote masoko yanajengwa?..ukiacha hiyo Masoko sio kipaombele kwa sasa na hayana return kubwa kusema yajengwe Kila mahali.
Sikia huyu kima eti treni za Dar zipi? Kama ni zile za Mwakyembe zinafanya Kazi,zile za Arusha zinafanya Kazi tena route na mabehewa mapya yameongezwa..
Tangu lini mpunga uliachwa kununuliwa ukiwa shambani? Kuna shida gani ukinunuliwa shambani? Hawalipi Ushuru? Soko la Mazao ni huria na sheria imeruhusu exports kokote kwenye Soko ndio maana Mchele uliingiza pesa nyingi kuliko zao lolote msimu ulioisha na hii sera haibadiliki,subirieni mpate taahira mwingine ndio mje kubadili..
Sasa mashirika yapi ambayo hayaelezi vitu in details? Kama hufuatilii na uko less informed hiyo ni shida yako,juzi tuu hapo umeona nhc wakisema wanataka kujenga nyumba 5,000 Nchi nzima na taarifa imetolewa..
Mwisho Serikali ya Sasa haina mbwembwe za kijinga kama waliopita kama ni miradi mipya iko mingi Sana na mingi inaanza kwenye bajeti hii sasa wewe ulitaka vipi miradi ianze mwaka aliopokea SSH wakati Uchumi ulianguka na miradi ilikuwa stalled ikiwemo hiyo hiyo aliyoanzisha Mwendazake..
Kama huna taarifa baadhi ya miradi mipya ni Msalato Airport, barabara za mzunguko Dom hazikuwa zimeanza,ujenzi wa meli mpya kwenye maziwa yote ikiwemo kufufua Mv Ilemba,Upanuzi wa njia 4 wa barabra ya TANZAM,miradi ya maji ya Bwawa la farkwa Dom,Kidunda Dar,miradi ya maji miji 28 zaidi Til.1,Upanuzi wa Vyuo vikuu zaidi ya til.1,barabara mpya kwa mfano mkoa niliko kuna Wachina wanajenga barabara mpya 2 bila shaka iko hivyo mikoa yote,miradi ya grid ya Taifa ya umeme Kam TAZA, hospital ya Rufaa ya Kanda ya Magharibi, hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma na Lindi,bandari ya Uvuvi Kilwa,brt awamu ya 3, hospital mpya 28 na vituo vya afya 252 vimejengwa,miradi ya scheme za Umwagiliaji zaidi ya 27 tayari nk.nk
Kilichobadiloka hapa ni makelele,pambio na chuki binafsi tuu nothing else maana kama ni mapesa mama anayamwaga kweli kweli kuanzia maji hadi kilimo..
Saizi ukiingia porta ya ajira imejaa matangazo ya Kazi ,kungekuwa hakuna pesa Serikali ingeshindwa kuajiri kama alivyoshindwa yule Mwendazake layman wa Uchumi..👇