Ii
Sio kdg ni sana mana 99% ya mambo yote mapya tunayoringia humu muasisi ni Magu usibabaike na maneno ya wavimba macho wanaojifanya hawakubali legacy lkn akipost kitu Muasisi ni yule yule.
Kinachonishangaza ni kwamba wanasema mama anamwaga pesa, sasa kama anamwaga pesa mbona miradi inasuasua?
Sasa hivi husikii stendi wala masoko yakianza kujengwa bado wanahangaika na ile aliyoacha Magu for almost 2yrs now.
Miradi iliyokuwa ianze ya ujenzi wa meli mpya kimyaa.
SGR Isaka Mwanza wanajenga kambi tu kwa muda wa miaka 2 sasa.
Hakuna mradi mpya uliobuniwa mpaka sasa baada ya kifo cha Magu. Jamaa alikuwa anataka barabara za kuingia na kutoka miji yote mikubwa ziwe njia nne kwa 50km, alikuwa aanze na Dom Toka afe kimyaa.
Treni za Dar kimyaa, stendi ya Arusha kimyaa, ya moshi imeachwa ijiozee.
Miaka 2 hakuna hata tetesi za mradi mpya.
Nasubiri miradi ya TACTIC ianze mwezi wa tisa nione kama itasimamiwa ipasavyo.
Kipindi kile Ummy Mwalimu alikuwa busy hasa, sasa hivi yuko karelax sababu mkubwa wake hana vision.
Kipindi cha Magu niligundua watz wana akili sana wakipata kiongozi mzuri, ulikuwa ukisikia viongozi wa mashirika mbalimbali wanaelezea vitu in details mpaka unafurahi,
Sasa hivi wamegeuka kuwa chawa.
Kule kanda ya ziwa waganda wameanza kununua mpunga ukiwa shambani wanaenda kukoboa kwao wameanza kutuuzia mchele tuliolima.
Nb.
Magufuli alikuwa na mapungufu yake ila yale mazuri tulipaswa kuendelea nayo.