Wachaga wamejaa nairobi na nakuru sana.
siku zote huwa nasema vijana wa kenya elimu yenu haijawasaidia kitu, kwasababu ujinga bado haujawatoka kichwani.
let me volunteer in giving you a short lecture.
sio jambo linalo hitaji mjadala kwa wachaga kupatikana nairobi.
ni kawaida kwa jamii zinazoishi jirani na mipaka ya nchi ku-interact au ku - intertrade pamoja.
nitakupa mifano hai:
watu wa mkoa wa mbeya wana interact/intertrade sana na watu wa nchi ya zambia na malawi kwa sababu mkoa wa mbeya umepakana na hizo nchi mbili kiasi cha kurahisisha maingiliano ya kiuchumi/kijamii na watu wa nchi hizo mbili.
watu wa mkoa wa mtwara wana interact/intertrade sana watu wa nchi ya mozambique kwasababu mkoa wa mtwara upo kusini mwa tanzania jirani na mpaka wa kuingia mozambique.
hata daraja la umoja lilijengwa kwa ushirikiano wa serikali ya tanzania na mozambique ili kurahusisha maingiliano ya kiuchumi/kijamii kwa watu wa nchi zote mbili.
watu wa mkoa wa kagera,wana interact/intertrade sana na watu nchi ya uganda,rwanda na burundi kwasababu mpaka ya mkoa wa kagera unapakana na nchi nilizo taja.
ukienda kigali au kampala utakuta kuna watanzania wengi tu walio wekeza katika miji hiyo.
sababu hizo hizo ndio zilizo sababisha wachaga kupatikana kwa wingi nairobi,watu wa mombasa kupatikana kwa wingi mkoa wa tanga na wajaruo wa migori kupatikana kwa wingi tarime,musoma na mkoa wa mwanza.