Ni Wazaramo, Wandengereko, Wazigua wanaopakana na Wilaya ya Handeni mkoa wa Tanga, Warufiji, Wakwere (kabila la Kikwete).
Miji yake ni kama Bagamoyo, Kibaha, Chalinze n.k.
Shughuli zao ni kama Uvuvi, Kilimo kama vile mananasi ukanda wa Bagamoyo eneo la Kiwangwa hapa ndio mahali pake, mpunga bonde la mto Ruvu kilimo cha mihogo na matikiti maji.
Huu ukanda ndio wenye viwanda vingi kuliko sehemu yoyote ile Tanzania. Kuna baadhi bado vinajengwa ambavyo havijaanza kufanya kazi.
Watu wake ni wakarimu sana kwa wageni hawana ubaguzi wowote ule. Wanapenda burudani ya ngoma za asili na taarabu, vijana Singeli na Bongo flavour.
Ongezea na miji ya Mkuranga, Kisarawe, Kibiti, Ikwiriri pamoja na kisiwa Cha Mafia, Jaja, kwale na koma.
Makabila yake mengine ni Wanyagatwa, Wakojani, Wajaja na Wanyangalio.
Bandari zao muhimu ni Bagamoyo, Kisiju pwani na Boza.
Watu maarufu ni Jakaya Mrisho Kikwete, Ally Hassan Mwinyi, Dr Hussein Mwinyi, Mbwana Samata, Shaban Robert, Adam Malima , 20%, Kingwendu.
Shughuli kubwa ni uvuvi kutokana na eneo kubwa bahari.
Kilimo hasa Cha mihogo, matunda ya aina zote ikiwemo mananasi , mafenesi, embe za kila namna.
Shughuli za viwanda hasa wilaya ya kibaha na Mkuranga.
Kilimo Cha mpunga kule mhoro na wilaya ya Rufiji
Shughuli ya utalii katika Mali kale za Bagamoyo,
Utalii wa fukwe katika kisiwa Cha Mafia, Mkuranga, Bagamoyo
Ni hayo tu.